Tunapenda sana kujitutumua lakini kiuhalisia Kenya ipo mbali sana ukilinganisha na Tanzania. Siyo kwa sababu wana pesa nyingi, siyo kwa sababu ni matajiri sana bali wamebahatika kuwa na uongozi mzuri na wenye maono, na kuwa na watu ambao, wengi wao siyo wanafiki.
Tanzania tuna short sighted leadership na watu ambao tumejaa unafiki, mahaba ya kiuwendawazimu na ushabiki wa kijinga. Tunafurahia kubishana hata kwenye mambo ambayo ni dhahiri.
Nani anaweza kuamini kuwa kwenye jamii ya watu wenye akili na uongozi wenye maono, Bunge mpaka sasa lingekuwa linaendelea? Mpaka sasa 3 wameanguka na kupoteza maisha, lakini waliobakia wanawaona waliofariki, labda walikuwa na ubinadamu nusu, ila wao kwa kuwa wana ubinadamu kamili, hawawezi kuambukizwa wala kufa. Na hawa wenye akili za inzi ni viongozi, je hali ipoje kwa wananchi wa kawaida.
Tumekuwa kama inzi. Inzi 100 wakiwa kwenye mzoga, unaweza kuua 50, waliobakia watarukaruka, baadaye watarudi tena. Utaua 40, waliobakia 10 watarukaruka, kisha watarudi tena. Hata ukiua 9, aliyebakia mmoja atarukaruka na kurudi tena. Mpaka uwamalize wote.
Rasilimali kubwa ya nchi siyo fisi wa kwenye mbuga za wanyama, dhahabu au gas iliyopo ardhini BALI ni nini watu wake wamebeba ndani ya vichwa vyao.
Sent using
Jamii Forums mobile app