Kenya wapiga marufuku polisi na trafiki kukaa barabara kuu kusumbua waendesha magari kwa kuwasimamisha

Kenya wapiga marufuku polisi na trafiki kukaa barabara kuu kusumbua waendesha magari kwa kuwasimamisha

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Nimepata habari toka Kenya kuwa elekezo limetolewa kwa askari wa kawaida na trafiki kuacha mchezo wa kukaa barabara kuu kusimamisha magari ili kukagua au sijui mambo ya spidi. Wameambiwa askari wa trafiki kazi yao kubwa iwe ni kusimamia magari maeneo ya mijini sio kuvizia magari huko porini kwenye njia kuu. Na kama wakitaka kuweka kizuizi au kwenda mahali njia kuu basi lazima kuwe na sababu maalum na wapewe kibali maalum. IGP wa Kenya amesema trafiki waende kwenye maeneo ya ajali tu sio kukaa barabarani wakivizia magari.

Kwa upande wa Tanzania askari trafiki njia kuu imekuwa ni kero. Hadi wanajificha mitini. Wakati tunakubali kwamba lazima madereva waendeshe magari kwa viwango vinavyotakiwa sehemu za miji, labda serikali ifikirie utaratibu wa kuweka matuta badala ya trafiki kuvizia watu kuwa umeendesha gari 55km/hr badala ya 50km/hr. Hata mara nyingine wanakuvizia kuona kama unazidisha spidi mita 5 tu baada ya alama ya 50km/hr. Au trafiki anakusimamisha bila kuona kosa, bali akutafutie kosa baada ya kuzunguka gari kama mara tatu. Huo ni upumbavu sio tena kufuatilia sheria.

Ikumbukwe kwamba mwaka 2018 Uganda nayo ilipiga marufuku trafiki barabara kuu, pale Museveni aliposema hawafanyi lolote bali kuomba rushwa tu huko barabara kuu.

Hongera sana Kenya.na Uganda. Mnajitambua sana maana siku hizi Tanzania kuwa na gari imekuwa karaha kutokana na usumbufu wa trafiki. I wishi I kudu be in Kenya or Uganda
 
Ndio zao hizo, kuna afisa mmoja wa NTSA Kenya aling'atwa na nyoka kwenye makalio akiwa amejificha vichakani akivizia magari.
0fgjhsmdnc8tfo12s.f253204e.jpg
 
tuige hii tupige ban traffic kwa barabara
 
Bongo ishakua biashara ya makusanyo ya Serikali hatuigi NG'O kodi msilipe na fine masipigwe!! Hii miradi itaendeshwaje???

Police wanaongoza TRA wanafata
[emoji1322][emoji1322][emoji1322][emoji1322][emoji1322][emoji1322][emoji1322]
 
tuige hii tupige ban traffic kwa barabara
Tatizo ni kwamba Polisi wamewekwa barabarani kuongeza mapato ya serikali sio kusimamia usalama. Kwa hiyo ni ngumu sana wakati tunataka hela za SGR na Stiegler Gorge
 
Very good move by IG ,i've always seen this practice as illegal and predatory and in reverse gear -ati nitasimamisha gari nitafute makosa badala ya leave people alone until you find a mistake.Some judges here in the states don't entertain this nonsense they rule it was an illegal stop to begin with.
 
kwetu wakitoka njiani kila uchwao tutaokota vyuma chakavyu vya magari
 
Nimepata habari toka Kenya kuwa elekezo limetolewa kwa askari wa kawaida na trafiki kuacha mchezo wa kukaa barabara kuu kusimamisha magari ili kukagua au sijui mambo ya spidi. Wameambiwa askari wa trafiki kazi yao kubwa iwe ni kusimamia magari maeneo ya mijini sio kuvizia magari huko porini kwenye njia kuu. Na kama wakitaka kuweka kizuizi au kwenda mahali njia kuu basi lazima kuwe na sababu maalum na wapewe kibali maalum. IGP wa Kenya amesema trafiki waende kwenye maeneo ya ajali tu sio kukaa barabarani wakivizia magari.

Kwa upande wa Tanzania askari trafiki njia kuu imekuwa ni kero. Hadi wanajificha mitini. Wakati tunakubali kwamba lazima madereva waendeshe magari kwa viwango vinavyotakiwa sehemu za miji, labda serikali ifikirie utaratibu wa kuweka matuta badala ya trafiki kuvizia watu kuwa umeendesha gari 55km/hr badala ya 50km/hr. Hata mara nyingine wanakuvizia kuona kama unazidisha spidi mita 5 tu baada ya alama ya 50km/hr. Au trafiki anakusimamisha bila kuona kosa, bali akutafutie kosa baada ya kuzunguka gari kama mara tatu. Huo ni upumbavu sio tena kufuatilia sheria.

Ikumbukwe kwamba mwaka 2018 Uganda nayo ilipiga marufuku trafiki barabara kuu, pale Museveni aliposema hawafanyi lolote bali kuomba rushwa tu huko barabara kuu.

Hongera sana Kenya.na Uganda. Mnajitambua sana maana siku hizi Tanzania kuwa na gari imekuwa karaha kutokana na usumbufu wa trafiki. I wishi I kudu be in Kenya or Uganda
ipo haja ya serikali ya Tanzania kulitizama hili, unakuta wamekaa vichakani wanakagua magari, hivi mtu unaamua kutoka Dar kwenda Morogoro Dodoma hauna leseni kweli? kama sio kusumbuana ni nini? mtu ambaye hana uzoefu wa kuendesha gari ataamua kwenda Arusha akitokea Kigoma kweli?
 
Very good move by IG ,i've always seen this practice as illegal and predatory and in reverse gear -ati nitasimamisha gari nitafute makosa badala ya leave people alone until you find a mistake.Some judges here in the states don't entertain this nonsense they rule it was an illegal stop to begin with.
Name one state where cities don't supplement their quarters from traffic violations.
 
Hii poa sana, na iwe ya kuigwa hata na huko Tanzania, yaani limewahi kututokea Dar kwenda Moro, maporini tulikamatwa kisa kasi ya uendeshaji, ilibidi tunyofolewe hela ya kiwi (mkulu sizonje alisharuhusu hili la kiwi au rangi ya viatu).
 
Hii poa sana, na iwe ya kuigwa hata na huko Tanzania, yaani limewahi kututokea Dar kwenda Moro, maporini tulikamatwa kisa kasi ya uendeshaji, ilibidi tunyofolewe hela ya kiwi (mkulu sizonje alisharuhusu hili la kiwi au rangi ya viatu).
Watu wengi wamepoteza maisha kwasababu ya uendeshwaji hovyo. Naelewa kuna abuse ya mapolisi ila kuwaondoa kabisa siyo sawa. Serikali inachotakiwa kufanya ni kutengeneza mazingira ya kuhakikisha madereva wasiofuata sheria wanaadhibiwa.
 
Watu wengi wamepoteza maisha kwasababu ya uendeshwaji hovyo. Naelewa kuna abuse ya mapolisi ila kuwaondoa kabisa siyo sawa. Serikali inachotakiwa kufanya ni kutengeneza mazingira ya kuhakikisha madereva wasiofuata sheria wanaadhibiwa.

Matuta yawekwe kwenye maeneo hatari, sio huo upumbavu wa jamaa kujificha maporini na litochi lake. Ifahamike kuna sehemu inaruhusiwa kwenda kwa kasi, lakini polisi hutumia maeneo kama hayo kujipatia mtaji.
 
Back
Top Bottom