Kenya Yafungua Tawi La Bandari Kigali Rwanda


umesahau kuwa siyo reli tu na barabara zipo. kwa sasa barbr inatumika sn kuliko reli
 
kenya are trying to win back wateja waliowapoteza mombasa na kuhamia tanzania in the past 18 months, lakini kuwin wateja si kufungua office tu kigali au kampala au bujumbura au bukavu au goma au lumbumbashi, tanzania wanamalizia kujenga vituo vya pamoja mpakani(one stop border posts) kwenye mipaka yake na nchi jirani, pia wanakaribia kuanza kujenga vituo vya ukaguzi vya pamoja njiani (one stop inspection stations) kwa ajili ya magari ya transit kwa lengo la kuyapunguzia muda wa safari kutoka bandari ya dar kwenda nchi husika, mipaka inayonufaika mpaka sasa ni rusumo(na rwanda), mutukula(na uganda), kabanga(na burundi), tunduma/makonde(zambia). namanga(kenya), horiri/taveta(kenya) lengo ni kutumia masaa 48 tu kutoka bandarini kwenda nchi husika, then hizo office zitafunguliwa kwa sasa kinachofanyika ni Dar port marketing stategy kwa wateja wa nje ya nchi, na wiki tatu zilizopita tanzania wamezindua system ya kusaidia kupunguza vikwazo na kutambua wakwamishaji wa usafirishaji kati ya bandari/ticts/weigh bridges/police/immigration na clearing agents.........
 
Tatizo letu ni nini hasa?
Ni kuchelewa kuchukua maamuzi?
Ni kukosa wataalamu? maana humu ndani walisema wasomi wetu hawauziki.
Ni kukosa ushirikiano ndani na nje ya nchi?
Ni upeo wa viongozi kugota?
Ni utaniutani badala ya kufanya kazi?
Ni mfumo mbovu wa ccm na Serikali? (ILANI)

TUCHUKUE HATUA HATA MUNGU ALIWAPIGA CHINI WAFALME VIHIYO NA KUSIMIKA IMARA.
 
sidhan kama DRC na burundi wanaweza pitisha mizigo yao kupitia mombasa!!!! ila its a good move ktk kuondoa ubabaushaj kwa kua na office huko!!!

Burundi zambia congo wataendelea kuwa wateja wetu wanahangaika na ujio wa bagamoyo port,
 
Burundi zambia congo wataendelea kuwa wateja wetu wanahangaika na ujio wa bagamoyo port,

issue siyo bandari tuu pia wanajenga standard guage railway itakoyounganisha mombasa,uganda hadi kigali. Mizigo itafika kigali chini ya masaa 24.
 
kama kawaida tutaendelea kuiita Rwanda 'mkoa' na dharau zingine huku tukisahau kuwa Kigali huenda ndio ikawa hub ya Kisangani, North Kivu, Bukavu nk. Vita inayoendelea huko ni swala la muda mfupi sana tu na punde hawa jamaa watafurahia maisha.


Sijui tupewe miwani ya aina gani ili tuweze kuona fursa tunazopoteza. Na hapo ni suala dogo tu la ukiritimba usio na tija. Pita mizani uone milori iliyoko kwenye foleni, ikisubiri kupima uzito, nenda mipakani milori hiyo hiyo inasubiri kuvuka, documents siku mbili zinakaguliwa. Hapo bandarini wakati wa kutoa mizigo ndio usisome, sijui hata kama zile hesabu za "Queuing theory" zina-apply huko.
 

Mkuu hivyo vizuizi vingi unavyoviona ndio vinaongeza mianya ya hawa jamaa kuendelea kula vizuri hiyo hela. Wafanyakazi wengi wa kwenye hizo weighbridge hela nyingi zinaishia mifukoni mwao. Wachunguze uone maendeleo waliyojilimbikizia binafsi. Its a shame
 

Kuita nyeusi ni nyeusi, tatizo kubwa ni hao watu waliosimama kwa hivyo vyeo ulivyotajwa. Labda tu watuhakikishie kuwa walishapeleka proposal ila ziko makabatini zinapigwa feni zenye upepo wa vumbi. Manake tukipita nje ya ofisi za gavumenti kuna makabrasha huwa tunayaona kwenye vioo, sijui ndio hizo proposal!
 
Kinachokera ni hii kauli Maarufu ya kwamba "tumefanya tathimini na upembuzi yakinifu na hela ziko tayari tunasubiri Utekelezaji tu.

Yaani ni wimbo ambao hata uutie vyombo vya aina gani, haunogi tena masikioni!
 

Nimegonga like mbili lakini zikagoma.

Kinashongaza ni huo uboreshaji wa mipakani wakati pale Bandarini penyewe ni mizengwe A to Z.

I have been a victim there. Kuna ujinga mmoja eti mkaguzi mmoja pale getini you stay there for hours waiting for your car.

grrrrrrrr!!!!!!!!!
 
Wabongo tuache uoga kenya wanajua kua tz tunajenga badar ya kisasa b/moyo so wanachokifanya ni kuimalisha masoko yao la msingi ni kumwomba mungu huo mradi utimie otherwise wakenya imekula kwao..
 
Hayo ni mapatano ya kisiasa yaliyoasisiwa na kagame na museveni kuikomoa tanzania lakini kiuchumi hawawezi kuiepuka bandari ya dar-es-salaam. Wewe subiri tu uhuru akitofautiana na sera zao za kimbari watamtolea nje namiradi yao ya alnacha. Tz inajenga miundombinu yake, watakuja bila kupenda.
 

unataka kutwambia kuwa kufungua bandali Kigali ndiyo yatakuwa maendeleo kwa Tanzania nani kakwambia kuwa bandari yetu inategemea pekee mizigo ya Rwanda,uganda na Kenya.
 
Kenya pia wametangaza tenda ya ujenzi wa high speed train railway 500km kutoka Nairobi mpaka Kisumu...

Yatupasa na sisi tuchangamke kufufua reli ya kati na kujenga fasta ile ya Mchuchuma mpaka Mtwara
 
Congrats. You have valid questions.BTW Mombasa port is being expanded into a megaport, one that has the capacity to handle the largest sea faring vessel.On completion, the port's capacity will rise to 1.7 Million TEus by 2015. The country is also planning to build a second railway line from MSa to Kisumu in order to increase speed and ease congestion at the Port. Dar- wamejipangaje?
 
issue siyo bandari tuu pia wanajenga standard guage railway itakoyounganisha mombasa,uganda hadi kigali. Mizigo itafika kigali chini ya masaa 24.

Rwanda na kenya wamekuwa na chuki na sisi siku nyingi ila contribution ya rwanda si kubwa kwenye bandari yetu kwahiyo haitutishi sana congo zambia ndiyo wenye contribution kubwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…