Kenya Yafuzu Kwenye Robo Fainali Za Mchuano Wa Raga 7s Afrika Baada Ya Kuilaza Morroco 41-0 Kule Jemmal, Tunisia

pingli-nywee

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2015
Posts
11,923
Reaction score
13,350
Hapo awali kwenye game yao ya kwanza ya mchuano huo wa Africa Mens 7s 2018 Jemmal, Tunisia, Shujaa, timu ya Kenya raga 7s, iliigaragaza Botswana 49-0. Kenya imeibuka mshindi kwenye Pool A ambayo ina nchi tatu za Kenya, Morroco na Botwana na ikafuzu hadi robo fainali bila ya kufungwa hata bao moja. https://www.capitalfm.co.ke/sports/2018/10/13/kenya-sevens-through-to-africa-7s-quarters/
Leo kwenye robo fainali Kenya itamenyana na Zambia ambayo iliibuka ya pili kwenye Pool D. Kenya imeshinda mchuano huu wa Africa Men's 7s mara nne, mara ya mwisho ikiwa ni mwaka wa 2015.
 
Wakenya mko vizuri, sisi labda Bongo Fleva na Bongo Movies, michezo mingine zero...
Nakuambia Shujaa, timu ya Kenya raga 7s haitaki masihara kule Tunisia. Jana nilitizama game yao ya kwanza walipoicharaza Botswana 49-0 hadi siku yangu ghafla ikawa ya furaha.
 
Wenzetu hawadangi taifa lao wanaliwakilisha vyema kwenye michezo ila kuna kikundi kipya cha Wadangaji kimeibuka hapa nchini wanadanga taifa bila huruma.

[emoji35][emoji35][emoji35][emoji35][emoji35]Pumbavu zao.
Ndio kina nani hao? Ingekuwa vyema kama ungewataja kwa majina. [emoji40]
 
Updates: Tumeichapa Zambia kwenye robo fainali na Madagascar kwenye nusu fainali. Tunamenyana sasa hivi na Zimbambwe kwenye fainali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…