Kenya Yaishinikiza Tanzania Kupitia EAC Kufungua Ushoroba Mpya wa Barabara ya Mombasa-Holili-Singida Kwa faida ya Bandari ya Mombasa

Kama kuna mahali Tanzania ilipo lala usingizi wa pono na kujisalimisha ni katika ushushushu wa kuishikilia iwe sehemu ya uchumi wa nchi ya Kenya.
Sidhani kuwa huu ulikuwa ni mpango walio fanya Kenya wenyewe; Kenya imetumiwa tu kwa vile ni koloni la hao wahujumu wenyewe wanao shikilia uchumi wa nchi hiyo.

Katika maswala ya aina hii, hapo ndipo natamani kuwa na kiongozi kichaa kama Magufuli. Hawa wapumbavu hata wasinge thubutu kuyahimiza haya.
Kwa huyu 'Chura Kiziwi', hii ndiyo fursa yao kuu ya kufanya ujinga huo.
 
Kama hatuna watu wanaojielewa pande hizo unategemea nini?

Watu waliopo ni wale ambao walimwambia Jiwe ukijenga Barabara ya Sumbawanga -Kasanga na Mpanda-Karema utaondoa foleni ya malori Tunduma 😂😂

Hao watu Huwa wanapayuka na hawajui chochote kuhusu jiografia Wala geopolitics au economic landscape ya Nchi.

Hao hao ndio walishauri kujenga Sgr eti itapunguza gharama za maisha na blaa blaa kama hizo.Nasubiria Kwa hamu sana kuona zitakavyopungua ndio nitatia neno (hakuna kitakachopungua am sure 100%) na hiyo Sgr ni tembo mweupe wa kupigia picha tuu za Kisiasa.
 
Ndio hatufungui Sasa (geofencing) wakashitaki basi
Kukimbia tatizo siyo njia ya kutatua tatizo, Dar port iboreshwe pia kodi zipungwe utashangaa mizingo mingi inaingia Dar port.
Ukisema hivyo basi UK na France wasingejenga tunnel ya kuziunganisha hizo nchi.
Usipende kushauri serikali kujifungia badala ya kuzifanyia kazi mapungufu badala ya kuweka mpira kwapani.
Dunia ni kijiji.
 
Ukweli ni kuwa ni jambo la kusikitisha kufikiri kuwa vi-inchi hivi kama Rwanda na Burundi vinaweza kulilia kupitisha mizigo yao Mombasa!
Hawa wana mizigo kiasi gani, na itakuwa nafuu vipi kwao kwenda kote huko?
Hizi kelele zinazo sikika ni sehemu ya propaganda tu na ajenda za hawa Kenya wakishirikiana kutuhujumu Tanzania.

Huu ni mpango endelevu wa mapambano kati ya Tanzania na hawa majirani. Tanzania inao uwezo wa kuwanyamazisha Kenya katika maswala kama haya, kwa sababu eneo tulipo inaruhusu sana.

Badala ya kupapatikia ujinga kama huu, juhudi zifanyike haraka, hasa kuijenga bandari ya Bagamoyo (kama DP World hajaweka pingamizi, kama tulivyo jikabidhi kwake); halafu SGR ikamilike haraka. Nani tena atahitaji kwenda Mombasa na malori? Hizo barabara bado tunalipia mikopo, kwa hiyo hayo malori kwa sasa yachangie gharama hizo kwa bei stahili.
Bandari ya Tanga nayo ipo pale, ni hazina. Kwa nini tusitumie raslimali zetu tulizo nazo kukomesha ujinga wa namna hii?
Kama kawaida yetu, tunabaki tunalialia kama hatuna akili kichwani?

Huu unao fanywa hapa ni uchokonozi wa maksudi kabisa, kuhusu mataifa hayo.
 
Biashara ni ushindani uwezi kuwa defensive, hiyo ni ishara ya uzembe (kitu ambacho watanzania tumezoea).

Wafanyabiashara wanataka option rahisi kwao, kwa sababu nchi yetu ina geographical advantages aina maana tufanye biashara za nchi nyingine kuwa ngumu.

Magari yanayopita Tanzania kutoka nchi jirani bado yanalipia road fees, kwa hivyo bado kuna mapato.

Lakini Uwezi kuwa mzembe kutoa mizigo, utaki kujirekebisha; halafu uwaazibu wengine kisa una geographical.

Msingi wa capitalism ni kujifunza kila siku wa-Japan wanaita (KAIZAN) na hiyo nadharia ndio imekuza uchumi wao na kuboresha kila sector ya taifa lao.

Uwezi kuwapa watu wasio na maarifa sector za mipango halafu udhani utasogea mbele.

Kwetu sisi kila kitu rahisi tu na solution zetu ni nyepesi, lakini huo utaratibu wetu costly kwa majirani zetu.

Mijitu ukiisikia haina uwezo kabisa, halafu wanaongoza sector sensitive.

Wapi duniani umeona civil services au wizara inaita watu kujadili dira na kusikiliza michango ya kijinga.

Surely kwenye biashara na uchumi watu wanatumia data ku-analyse, use that information to do strategic planning na kupanga sera.

Ukiona mtu anaitisha mdahalo wa kujadili mipango ya serikali elewa ni ujinga mtupu hamna kitu kichwani na aelewi namna ya kuandaa strategy ya sera za biashara na uchumi.

Ndio ukweli wenyewe, hata kama amuupendi.

Siwezi nikamsikiliza poyoyo kama Mafuru ni financial or economists zaidi ya mpuuzi mwingine ambae unajiuliza kafika vipi pale; huyo Kitila ndio salaleh.
 
Watu waliopo ni wale ambao walimwambia Jiwe ukijenga Barabara ya Sumbawanga -Kasanga na Mpanda-Karema utaondoa foleni ya malori Tunduma
Ukiondoa siasa na upotoshaji katika maswala kama haya maandishi yako yanakuwa na uzito wa kutosha. Sasa niambie, ni kweli ujenzi wa barabara hizo sababu kuu ilikuwa ni kuondoa "foleni Tunduma"? Mimi sijui, lakini nahisi hapo haupo sahihi.
Swala la SGR, kama ilivyo kwa mambo mengi mengine, kama RBT Dar, ni lazima kutenganisha umuhimu wa miundo mbinu hizo na uendeshaji wa hiyo miradi kwa ufanisi. Katika kuona utekelezaji wa uendeshaji wa hiyo SGR unavyo kwenda kwa sasa, sina matumaini makubwa sana juu yake. Sioni tofauti yake na BRT, na miradi mingi mingine muhimu tuliyo wahi kuibuni hapa nchini na kuishia kuiharibu. Hadi hapo tutakapo toka katika hii hali ya ubovu wetu kiutendaji kila sehemu, hapo ndipo mambo yataanza kuonekana kuwa sawa.
Lakini najuwa, kutegemea ufanisi sehemu yoyote katika nchi yetu hii ni kama kujaribu kuunda chombo cha kwenda mwezini; uwezo ambao Tanzania kwa sasa hatuna.
 
Ukisema hivyo basi UK na France wasingejenga tunnel ya kuziunganisha hizo nchi.
Na bado UK wakaamua kujiondoa EU; na viboti vya wakimbizi ndipo vikashika moto! Au haya huyajui?

Hakuna anayekataa ushirikiano, lakini ushirikiano wa kuwa 'taken advantage of', huo ni upumbavu.
 
Tatizo lako wewe siku zote ni lilelile, kudhani kwamba hiyo fani (taaluma) uliyo nayo wewe ndio ufunguo wa matatizo yote yanayoikabili Tanzania!
Haya yote uliyo eleza hapa ni upuuzi. Katika kupanga mipango ya maendeleo ya nchi huwezi kujifungia ofisini na vidigrii vyako (sijui katika nini), halafu na kuwasilisha kuwa ndiyo ramani inayotakiwa kufuatwa.
Huu utakuwa ni zaidi ya ujinga.

Lakini ninakubaliana na wewe kuhusu hao ulio wataja hapo kwenye andiko lako; hata kama na wewe sioni kuwa na utofauti na wao.
 
Huwa sipotoshi chochote
 
Wewe Huwa unadhani una akili kushinda woote ,huu nao ni aina ya ugonjwa wa akili 😆😆

Mwisho hakuna maslahi binafsi ya mfanyabiashara yatakuwa mbele at expense ya maslahi ya Nchi tena mfanyabiashara mwenyewe atanufaisha jirani.
 
Bado ni ujinga kuzuia njia. Dunia ni kijiji. Hizi ndio sababu zinapelekea jumuia kuvunjika.
Hakuna njia ikezuikiwa,do it at your own risk , Serikali haiwezi fanya geofencing kwenye route ambayo haiwanufaishi.
 
Mawazo ya KIMASKINI na Upeo MDOGO
 
Huu ushoroba wa Mombasa-Voi-Holili-Moshi-Arusha ni muhimu mno kwa uchumi wa Tanzania na Kanda ya Kaskazini ni vizuri ushoroba huu ukafunguliwa haraka sana.
 
Hakuna njia ikezuikiwa,do it at your own risk , Serikali haiwezi fanya geofencing kwenye route ambayo haiwanufaishi.
Lakini sasa makubaliano ya ushirika yatalazimisha, ndiyo maana ya kelele hizo nyingi.

Dawa pekee iliyopo, kama kweli tungetaka kuwakomesha hawa vidomo domo ni kuhakikisha kwamba gharama za kwenda Mombasa ni hasara kuliko kwenda Dar au kutumia Tanga baada ya kuiboresha zaidi.
Hakuna sababu kabisa, hata ndogo ya kuifanya Burundi na Rwanda waende Mombasa kuchukuwa mizigo yao, iwe ni kwa kupitia Tanzania, au huko Uganda. Hakuna.
 
Ndugu strategic decisions ni data sio porojo.

Makongamano in research methodology ni sawa interview quality ya michango inategemea na level of knowledge ya wachangiaji.

Sasa not long ago mwaka huu huu JF kulikuwa na mada ya mfanyabiashara mkubwa mwenye mafanikio mzigo wake uliungua kwenda kudai insurance anaambiwa evidence ya import VAT hana. Baada ya hapo anaita media nakuanza kulaumu shipper aliemtolea mzigo, yeye mwenyewe hajui hata evidence gani anatakiwa kuwa nazo kibiashara.

Sasa ushakliza ujinga wa midahalo ya kibiashara ni vitu senseless kabisa.

Ushaona report za specialised businesses and marketing consultant wa kimataifa (zile ambazo unalipia) zisizotumia marketing data za nchi husika kwenye interpretation zao.

Strategic planning ni data za serikali sio upuuzi mwingine, wanaitana kwa masaa ukumbi imejaa halafu asilimia 90% ya michango ukisikiliza upuuzi mtupu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…