PROF.MUHONGO "WATANZANIA NI WAVIVU WA KUFIKIRI, WAVIVU KUSOMA NA WASHAMBA WA UWEKEZAJI"
WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, ameingia katika mgogoro mwingine wa uzembe wa matumizi ya ulimi. Hilo lilitokea juzi katika ukumbi wa Classic Ubungo Plaza mbele ya viongozi wa dini kutoka kote nchini ambapo waziri huyo alikuwa akiwahutubia viongozi hao kuhusiana na sekta nzima ya madini na rasilimali za nchi. Kongamano hilo liliandaliwa na Kamati ya Kudumu ya viongozi wa dini inayojishughulisha na utetezi wa rasilimali za nchi na haki za wananchi.
Viongozi waliohudhuria walitoka Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata), Tume ya Kikristo Tanzania (CCT) na Baraza la Maaskofu Katoliki (TEC) pamoja na asasi za kiraia za haki madini, Policy Furum, Norwegian Church Aid, Ongea na wawakilishi wa taasisi za elimu ya juu hapa nchini.