Kenya's Day of Pride; The Birth of a New Republic

Rais Kibaki ndo sasa amemaliza kukagua gwaride na sasa anasalimiana na VIPs
 
Sasa Muda wa kumtanguliza Mwenyezi Mungu; Viongozi wa dini wameanza kutoa sala na dua lao....wameanza na kiongozi wa kijadi wa kabila la kimaasai.... hao sijaambulia kitu
 
Kwa mara ya kwanza namsikia MMASAI NADHANI AKIWAKILISHA DINI ZA JADI.... Naye anatoa maombi............
 

Tumpe ushirikiano Dr Slaa na hili lawezekana na kwetu. Tena kwa ubora kuliko Kenya.
 
Sasa ni zamu ya Chief Kadhi ....kumbuka Kenya wana mahakama ya kadhia....naye anatoa sala zake kuhusu tukio la leo.
 
jamani tujifunze kwa hawa watu.

Kweli tunahitaji kukaa chini nakulifanyia kazi, chamgamoto ni je tunao watu wenye kuthubutu kutoa changamoto ya kweli..kumbuka kenya imewachukua miongo 2 ya hata kumwaga damu kufika hapo walipo leo. Natumaini kwa sifa yetu ya amani na upeo na busara za viongozi wetu tunaweza kufikia hapa wakenya walipofikia leo hii kwa amani kabisa!:smile-big:
 
Naona Karume na Bashiri wa Sudani wanafuatilia kwa makini....Je, Karume na mabadiliko ya katiba Zaznibar ni mwanzo wa kuchakachua katiba yetu au mwanzo mpya kueleka kupata katiba mpya inayokidhi kizazi cha leo na kijacho hapa JMTZ?
 
Chief Kadhi naona sasa amemaliza na anaingia kiongozi wa-anglikana kutoa sala zake.
 
really it is the rebirth of the Kenyan Republic!
 
wakenya leo wanaanza mwanzo mpya naona rais kibaki ndo anaingia uwanjani akiwa katika landrover special ya kijeshi kumtambulisha kamaamiri jeshi mkuu

kenya wlishapata uhuru sisi watanzania bado hatujawa huru. Tukiwa huru tutaunda katiba mpya , tunatakiwa kupiginia uhuru kwanza
 
Sasa muda umefika naona mwali [katiba] ndo inatolewa na chief justice wa kenya
 
Sasa Rais Kibaki na CJ ndo wamenyanyuka . Naona Mwai Kibaki anasoma kiapo cha kusaini hiyo katiba.
 
Hivi haka katoto kalikoingia na First Lady Lucy Kibaki katakuwa kajukuu kake nini?
 
Naona Mwai kibaki sasa ametangaza rasmi katiba Mpya!


sasa anazisaini

Hongereni ndugu zetu wakenya
 
Tayari Kibaki ameshatamka kupitia 'instrument of promulgation' kuwa katiba inaanza kazi leo hii. Naona sasa anatia saini yake alellujah !!!:A S 8: Uwanja wote umelipuka
 
Kumbe wakenya walikuwa bado na katiba iliyosainiwa na Malkia!

they really deserve this
 
Baada ya muhuri naona yametimia, Kibaki sasa anaionyesha kwa public, kimeeleweka sasa bado sisi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…