Viol
JF-Expert Member
- Dec 15, 2009
- 25,420
- 18,298
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta,amesema kuwa
hawezi kuhudhuria kikao alichoagizwa kuhudhuria
na mahakama ya kimataifa ya ICC mwezi ujao
kutokana na kazi nyingi aliyonayo.
Mahakama hiyo ilimtaka afike mbele yake kujibu
madai kuwa serikali yake imekataa kuwasilisha
shatakabadhi zinazohitajika na mahakama hiyo
katika kesi inayomkabili.
Kenyatta kupitia kwa mawakili wake ameitaka
mahakama ya ICC kuahirisha kikao hicho.
Alikuwa ameamrishwa kufika mbele ya kikao hicho
cha siku mbili baada ya upande wa mashitaka
kulalamika kuwa rais huyo amekataa kuwasilisha
ushahidi mbele ya makahama hiyo.
Hata hivyo mawakili wa rais Kenyatta wameitaka
mahakama hiyo sasa kumruhusu mteja wao imma
ashiriki kikao hicho kupitia video ama skype, au
wao wajibu masuali kwa niaba yake.
Rais Kenyatta amesema kuwa yeye yuko na
shughulio n yingi sana kuweza kuhudhuria kikao
hicho mwezi ujao.
Amesema kuwa mikutano miwili muhimu ya
kiserikali ilikuwa imeshapangwa kufanyika nchini
Uganda katika tarehe hizo wanazoitisha
mahakama.
Rais huyo na naibu wake William Ruto
wanakabiliwa na mashtaka ya kupanga mauaji ya
kikabila wakati wa machafuko yaliyozuka nchini
Kenya baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka wa
2007.
Kesi hiyo tayari imechelewehwa kwa muda mrefu
huku mashahidi wakuu wakijiondoa na pia
kumekuwa na malalamiko kuwa baadhi ya
mashahidi hao wame tolewa vitisho kubadilisha
ushahidi wao au kuondoa kabisa.
Mwendesha mashtaka mkuu Fatou Bensouda na na
mawakili wa waathiriwa wamesalia na siku tatu
sasa kujibu ombi hilo la Rais Kenyatta la
kuahhirisha kikao hicho.
Mawakili wa rais Kenyatta wame kuwa wakisisitiza
kila mara kuwa kesi hhiyo iondolewe kabisa
kutokana na kile wanachodai kuwa ukosefu wa
ushahidi dhidi yake.
Hakuna aliye shitakiwa hadi leo nchini Kenya kwa
kuhusika na kupanga machafuko hayo yaliyoizonga
Kenya mwishoni mwa mwaka wa 2007
BBC Swahili
hawezi kuhudhuria kikao alichoagizwa kuhudhuria
na mahakama ya kimataifa ya ICC mwezi ujao
kutokana na kazi nyingi aliyonayo.
Mahakama hiyo ilimtaka afike mbele yake kujibu
madai kuwa serikali yake imekataa kuwasilisha
shatakabadhi zinazohitajika na mahakama hiyo
katika kesi inayomkabili.
Kenyatta kupitia kwa mawakili wake ameitaka
mahakama ya ICC kuahirisha kikao hicho.
Alikuwa ameamrishwa kufika mbele ya kikao hicho
cha siku mbili baada ya upande wa mashitaka
kulalamika kuwa rais huyo amekataa kuwasilisha
ushahidi mbele ya makahama hiyo.
Hata hivyo mawakili wa rais Kenyatta wameitaka
mahakama hiyo sasa kumruhusu mteja wao imma
ashiriki kikao hicho kupitia video ama skype, au
wao wajibu masuali kwa niaba yake.
Rais Kenyatta amesema kuwa yeye yuko na
shughulio n yingi sana kuweza kuhudhuria kikao
hicho mwezi ujao.
Amesema kuwa mikutano miwili muhimu ya
kiserikali ilikuwa imeshapangwa kufanyika nchini
Uganda katika tarehe hizo wanazoitisha
mahakama.
Rais huyo na naibu wake William Ruto
wanakabiliwa na mashtaka ya kupanga mauaji ya
kikabila wakati wa machafuko yaliyozuka nchini
Kenya baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka wa
2007.
Kesi hiyo tayari imechelewehwa kwa muda mrefu
huku mashahidi wakuu wakijiondoa na pia
kumekuwa na malalamiko kuwa baadhi ya
mashahidi hao wame tolewa vitisho kubadilisha
ushahidi wao au kuondoa kabisa.
Mwendesha mashtaka mkuu Fatou Bensouda na na
mawakili wa waathiriwa wamesalia na siku tatu
sasa kujibu ombi hilo la Rais Kenyatta la
kuahhirisha kikao hicho.
Mawakili wa rais Kenyatta wame kuwa wakisisitiza
kila mara kuwa kesi hhiyo iondolewe kabisa
kutokana na kile wanachodai kuwa ukosefu wa
ushahidi dhidi yake.
Hakuna aliye shitakiwa hadi leo nchini Kenya kwa
kuhusika na kupanga machafuko hayo yaliyoizonga
Kenya mwishoni mwa mwaka wa 2007
BBC Swahili