Kero kuhusu ajira za muda kwa watumishi wa umma, hususan walimu

Kero kuhusu ajira za muda kwa watumishi wa umma, hususan walimu

Jamaa Fulani Mjuaji

Senior Member
Joined
Jul 25, 2020
Posts
155
Reaction score
278
Katika hali ya sasa ambapo ukosefu wa ajira kwa vijana nchini Tanzania unazidi kuongezeka mwaka hadi mwaka, inasikitisha kuona kwamba serikali bado inaajiri watumishi wa umma, hususan walimu, kushiriki kwenye ajira za muda kama vile kusimamia uchaguzi, sensa, au kuandikisha majengo. Hii imekuwa kero kubwa kwa sababu ifuatavyo:

KERO ZILIZOPO
1. Kuwanyima Fursa Vijana Wanaohitaji Ajira:

Walimu na watumishi wa umma wengine tayari wana ajira na wanapokea mishahara. Kuwapa nafasi za ajira za muda kunawanyima vijana waliohitimu vyuo vikuu, ambao wengi wamekaa mtaani kwa zaidi ya miaka 10 bila ajira, fursa ya kupata kipato kidogo kupitia nafasi hizi. Ni dhahiri kuwa mfumo huu unakosa haki kwa wahitaji wa kweli.

2. Shule na Vituo vya Afya Kuathirika Kipindi cha Ajira za Muda:
Msimu wa kazi hizi za muda, vituo vya Afya Vinakosa watoa huduma na shule nyingi zinaachwa bila walimu wa kutosha kwa sababu baadhi yao wanaondoka shule kwa muda kushiriki katika kazi hizi. Kuna shule ambapo walimu wote, pamoja na wakuu wa shule, wanaacha shule tupu, hususan maeneo ya vijijini ambayo mara nyingi hayafikiwi na wakaguzi wa elimu kwa urahisi. Hii inazorotesha utoaji wa elimu kwa wanafunzi.

3. Kutothamini Ualimu na Taaluma:
Serikali inaonekana kuwachukulia walimu kama watu wenye "njaa kali" na wasiothamini nafasi zao kwa kugombania ajira za muda. Wanapewa nafasi hizi za muda kwa ujira mdogo wa elfu 30,000 kwa siku mbili Baadhi ya maeneo bila kuzingatia athari kwa taaluma yao na elimu kwa ujumla. Walimu wanaoendekeza hali hii wanadidimiza heshima ya taaluma ya ualimu, hali inayosababisha taaluma hiyo kuonekana ya ovyo mbele ya jamii.

MAPENDEKEZO
1. Ajira za Muda Zitolewe kwa Vijana Wasio na Ajira:
Serikali iache mara moja kuajiri watumishi wa umma, hasa walimu Kwa kazi za muda. Badala yake, nafasi hizi zitolewe kwa vijana waliohitimu vyuo vikuu na ambao hawana ajira. Vijana hawa wanastahili nafasi ya kushiriki katika shughuli kama hizi, kwani itawasaidia kupata kipato kidogo na kuwapa matumaini ya maisha.

2. Shule na Vituo vya Afya Vilindwe Kipindi cha Ajira za Muda:
Ni muhimu kuwe na kanuni inayozuia walimu, hasa wale wa shule za msingi na sekondari, kushiriki kwenye ajira za muda. Hii itahakikisha shule zinaendelea kutoa elimu kwa wanafunzi bila kukatizwa. Wakuu wa shule pia wawe mfano kwa kuzingatia wajibu wao wa kuongoza shule zao badala ya kuacha shule tupu.

3. Walimu Wathaminiwe Pengine Waongezewe "POSHO" ili Waache Kufanya Kazi za Muda:
Walimu na watumishi wa umma, hasa wale wa sekta ya afya na elimu, wanapaswa kuelewa thamani yao katika nafasi zao za kazi. Badala ya kuendekeza kazi za muda kwa ujira mdogo, wanapaswa kujitahidi kuboresha taaluma zao na heshima ya taaluma yao Watafute Hata Vyanzo Mbadala Vya kipato Kuepusha Aibu za aina Hii. Serikali pia inapaswa kuimarisha maslahi yao badala ya kuwategemea kushiriki kwenye kazi za muda zisizo na tija kwa taaluma yao.



 
Sijalenga kumkejeli mtu bali nimesimamia ukweli uliopo

Unavyosema njaa kali, kukosa dira au viposho

Sidhani kama ni maneno sahihi, kulikuwa na namna nzuri ya kuwasilisha hoja yako pasi na kutumia kauli hizo.

Mwisho wa siku hakutakuwa na mjadala hapa zaidi ya malumbano na kutusiana.

Subiri uone.
 
Unavyosema njaa kali, kukosa dira au viposho

Sidhani kama ni maneno sahihi, kulikuwa na namna nzuri ya kuwasilisha hoja yako pasi na kutumia kauli hizo.

Mwisho wa siku hakutakuwa na mjadala hapa zaidi ya malumbano na kutusiana.

Subiri uone.
Oohoo kumbe hayo maneno ni matusi
 
k
Katika hali ya sasa ambapo ukosefu wa ajira kwa vijana nchini Tanzania unazidi kuongezeka mwaka hadi mwaka, inasikitisha kuona kwamba serikali bado inaajiri watumishi wa umma, hususan walimu, kushiriki kwenye ajira za muda kama vile kusimamia uchaguzi, sensa, au kuandikisha majengo. Hii imekuwa kero kubwa kwa sababu ifuatavyo:

KERO ZILIZOPO
1. Kuwanyima Fursa Vijana Wanaohitaji Ajira:

Walimu na watumishi wa umma wengine tayari wana ajira na wanapokea mishahara. Kuwapa nafasi za ajira za muda kunawanyima vijana waliohitimu vyuo vikuu, ambao wengi wamekaa mtaani kwa zaidi ya miaka 10 bila ajira, fursa ya kupata kipato kidogo kupitia nafasi hizi. Ni dhahiri kuwa mfumo huu unakosa haki kwa wahitaji wa kweli.

2. Shule na Vituo vya Afya Kuathirika Kipindi cha Ajira za Muda:
Msimu wa kazi hizi za muda, vituo vya Afya Vinakosa watoa huduma na shule nyingi zinaachwa bila walimu wa kutosha kwa sababu baadhi yao wanaondoka shule kwa muda kushiriki katika kazi hizi. Kuna shule ambapo walimu wote, pamoja na wakuu wa shule, wanaacha shule tupu, hususan maeneo ya vijijini ambayo mara nyingi hayafikiwi na wakaguzi wa elimu kwa urahisi. Hii inazorotesha utoaji wa elimu kwa wanafunzi.

3. Kutothamini Ualimu na Taaluma:
Serikali inaonekana kuwachukulia walimu kama watu wenye "njaa kali" na wasiothamini nafasi zao kwa kugombania ajira za muda. Wanapewa nafasi hizi za muda kwa ujira mdogo wa elfu 30,000 kwa siku mbili Baadhi ya maeneo bila kuzingatia athari kwa taaluma yao na elimu kwa ujumla. Walimu wanaoendekeza hali hii wanadidimiza heshima ya taaluma ya ualimu, hali inayosababisha taaluma hiyo kuonekana ya ovyo mbele ya jamii.

MAPENDEKEZO
1. Ajira za Muda Zitolewe kwa Vijana Wasio na Ajira:
Serikali iache mara moja kuajiri watumishi wa umma, hasa walimu Kwa kazi za muda. Badala yake, nafasi hizi zitolewe kwa vijana waliohitimu vyuo vikuu na ambao hawana ajira. Vijana hawa wanastahili nafasi ya kushiriki katika shughuli kama hizi, kwani itawasaidia kupata kipato kidogo na kuwapa matumaini ya maisha.

2. Shule na Vituo vya Afya Vilindwe Kipindi cha Ajira za Muda:
Ni muhimu kuwe na kanuni inayozuia walimu, hasa wale wa shule za msingi na sekondari, kushiriki kwenye ajira za muda. Hii itahakikisha shule zinaendelea kutoa elimu kwa wanafunzi bila kukatizwa. Wakuu wa shule pia wawe mfano kwa kuzingatia wajibu wao wa kuongoza shule zao badala ya kuacha shule tupu.

3. Walimu Wathaminiwe Pengine Waongezewe "POSHO" ili Waache Kufanya Kazi za Muda:
Walimu na watumishi wa umma, hasa wale wa sekta ya afya na elimu, wanapaswa kuelewa thamani yao katika nafasi zao za kazi. Badala ya kuendekeza kazi za muda kwa ujira mdogo, wanapaswa kujitahidi kuboresha taaluma zao na heshima ya taaluma yao Watafute Hata Vyanzo Mbadala Vya kipato Kuepusha Aibu za aina Hii. Serikali pia inapaswa kuimarisha maslahi yao badala ya kuwategemea kushiriki kwenye kazi za muda zisizo na tija kwa taaluma yao.

Katika hali ya sasa ambapo ukosefu wa ajira kwa vijana nchini Tanzania unazidi kuongezeka mwaka hadi mwaka, inasikitisha kuona kwamba serikali bado inaajiri watumishi wa umma, hususan walimu, kushiriki kwenye ajira za muda kama vile kusimamia uchaguzi, sensa, au kuandikisha majengo. Hii imekuwa kero kubwa kwa sababu ifuatavyo:

KERO ZILIZOPO
1. Kuwanyima Fursa Vijana Wanaohitaji Ajira:

Walimu na watumishi wa umma wengine tayari wana ajira na wanapokea mishahara. Kuwapa nafasi za ajira za muda kunawanyima vijana waliohitimu vyuo vikuu, ambao wengi wamekaa mtaani kwa zaidi ya miaka 10 bila ajira, fursa ya kupata kipato kidogo kupitia nafasi hizi. Ni dhahiri kuwa mfumo huu unakosa haki kwa wahitaji wa kweli.

2. Shule na Vituo vya Afya Kuathirika Kipindi cha Ajira za Muda:
Msimu wa kazi hizi za muda, vituo vya Afya Vinakosa watoa huduma na shule nyingi zinaachwa bila walimu wa kutosha kwa sababu baadhi yao wanaondoka shule kwa muda kushiriki katika kazi hizi. Kuna shule ambapo walimu wote, pamoja na wakuu wa shule, wanaacha shule tupu, hususan maeneo ya vijijini ambayo mara nyingi hayafikiwi na wakaguzi wa elimu kwa urahisi. Hii inazorotesha utoaji wa elimu kwa wanafunzi.

3. Kutothamini Ualimu na Taaluma:
Serikali inaonekana kuwachukulia walimu kama watu wenye "njaa kali" na wasiothamini nafasi zao kwa kugombania ajira za muda. Wanapewa nafasi hizi za muda kwa ujira mdogo wa elfu 30,000 kwa siku mbili Baadhi ya maeneo bila kuzingatia athari kwa taaluma yao na elimu kwa ujumla. Walimu wanaoendekeza hali hii wanadidimiza heshima ya taaluma ya ualimu, hali inayosababisha taaluma hiyo kuonekana ya ovyo mbele ya jamii.

MAPENDEKEZO
1. Ajira za Muda Zitolewe kwa Vijana Wasio na Ajira:
Serikali iache mara moja kuajiri watumishi wa umma, hasa walimu Kwa kazi za muda. Badala yake, nafasi hizi zitolewe kwa vijana waliohitimu vyuo vikuu na ambao hawana ajira. Vijana hawa wanastahili nafasi ya kushiriki katika shughuli kama hizi, kwani itawasaidia kupata kipato kidogo na kuwapa matumaini ya maisha.

2. Shule na Vituo vya Afya Vilindwe Kipindi cha Ajira za Muda:
Ni muhimu kuwe na kanuni inayozuia walimu, hasa wale wa shule za msingi na sekondari, kushiriki kwenye ajira za muda. Hii itahakikisha shule zinaendelea kutoa elimu kwa wanafunzi bila kukatizwa. Wakuu wa shule pia wawe mfano kwa kuzingatia wajibu wao wa kuongoza shule zao badala ya kuacha shule tupu.

3. Walimu Wathaminiwe Pengine Waongezewe "POSHO" ili Waache Kufanya Kazi za Muda:
Walimu na watumishi wa umma, hasa wale wa sekta ya afya na elimu, wanapaswa kuelewa thamani yao katika nafasi zao za kazi. Badala ya kuendekeza kazi za muda kwa ujira mdogo, wanapaswa kujitahidi kuboresha taaluma zao na heshima ya taaluma yao Watafute Hata Vyanzo Mbadala Vya kipato Kuepusha Aibu za aina Hii. Serikali pia inapaswa kuimarisha maslahi yao badala ya kuwategemea kushiriki kwenye kazi za muda zisizo na tija kwa taaluma yao.



kwa uelewa wangu me naamini kwenye hizi ajira za muda kuna maslahi fulani yanalindwa kwasababu kuna upande unanufaika na shughuli hizo au kazi za muda ambazo mara kadhaa nimezishuhudia kama issue ya kazi za muda za sensa, uandikishwaji na uboreshwaji wa daftari la uchaguzi wa serikali za mitaa, sensana nyinginezo zinahitaji mtu ambae anaweza kuwa subjective kwa mfumo uliopo. Kwa mfano issue ya uchaguzi unakuta kwakuwa halmashauri inaundwa na serikali ya chama kikuu kwaiyo watataka uchaguzi usimamiwe na watu ambao wanaweza kupokea na kutekeleza maelekezo sasa hawawezi wakakuajiri wewe ambae hauna ajira kwasababu hawana wanapoweza kukukabia ili uwe somehow subjective to the system, specifically mwalimu anaweza kuambiwa bwana ukihakikisha kitu flani kutokea utapandishwa cheo au wanaambiwa je serikali ipi imekuajiri? je unataka aingie mpinzani ambae hujui atakuja na mfumo upi kwako ambao unaweza kuharibu kula yako kwaiy waalimu au watumishi ni lazima waingie kwenye mfumo wavuruge mambo. Lkn pia waalimu na watumishi wengine kumbuka ni elites yaani wanaujuzi fulani kwaiy hata semina za mafunzo yao huwa haziwasumbui kwasababu wanajua tyr hawa wana uelewa tofauti mkubwa tofauti na mtu ambae yupo mtaani for long period ujuzi umeanza kupungua hivyo kuhitaji seminar ndefu na maelekezo mengi. Naomba kuwasilisha
 
Back
Top Bottom