Kero: Msemaji wa timu ya Yanga hatufai

Kero: Msemaji wa timu ya Yanga hatufai

Kuwa msemaji wa timu sio lazima uwe talkative muda wote kwa mambo mengne yasio ya msingi
Mkuu mbona hata kwenye yale ya msingi kama Kuhamasisha mashabiki kuhusu michango na kufika uwanjani na kutoa updates za wachezaji tetesi za migomo na mambo yahusuyo Club hatumuoni akiwa mbele mbele. Huwezi amini %kubwa yetu wa Yanga hatupati taarifa kutoka kwake. Hakuna updates zozote za upcoming games na ufafanuzi wa games zetu sanjari na kuwapa moyo mashabiki. Mkuu sisi inatuuma sana wasione tupo kimya.
 
SIMBA NA YANGA NI TIMU ZA USWAHILINI NI ZA KISWAHILI

1. Lazima awepo tajiri mwenye uwezo wa kununua wachezaji kuwalipa mshahara na pesa nyingine kwa ajili ya kuwapa " WAZEE WA TIMU" ambao hawana kazi ila siku usipowapa fedha utakipata
Inategemea na uongozi uliokuwapo na hali ya mfumo wa kiuchumi. wakati wa enzi za ujamma (Nyerere), Yanga na Simba zilikuwa na connections na wafanyakazi wa mashirika na taasisi za serikali, na wachezaji wake wengi walikuwa wanapatiwa kazi (wanaajiriwa) na kulipwa mshahara ilhali wakiwa kwenye likizo za michezo kama vile ligi kuu, shimuta umishumta etc..
pia, timu ikishinda, wanapewa asilimia 50% ya mapato ya getini wagawane ikifungwa 20%, droo 30-35%.
Wakati huo, mapato ya getini ni mapato hasa, siyo kama siku hizi.
Pamoja na hayo, kulikuwa na wafadhili wahindi na waarabu wafanyabiashara ambao wakichangia timu au kufadhili hupata dili kutoka serikalini na mashirika ya umma.
Safari ya Simba ya Brazil kwa mfano, ni 10% ya wabrazil waliokuwa wakijenga barabara ya Moro - Dodoma chini ya waziri Sitta.
2. Lazima wawepo watu/kamati ambayo kazi yao ni kuzunguka na kutafuta waganga wa kienyeji ambao wakati mpira unachezwa wao watakuwa amba wamewabebesha wachezaji furushi la makorokoro ya ajibu ama watakuwepo uwanjani wenyewe wakiwa wamejificha sehemu wakiendelea na vimbwanga vyao, zamani walikuwa ni wazee lakini siku hizi ni vijana wadogo sana
Hii ni kweli na kamati ya utendaji huwa chini ya Mwenyekiti wa klabu. Mwenyekiti na makamu mwenyekiti shughuli zao huwa zipo tofauti na sekretariati. kazi zao siyo za mshahara na huwa hawana sauti kwenye mapato ya kila siku ya klabu. Imetokea tu siku hizi mwenyekiti anakuwa muhindi mfadhili na anahusika na fedha. Kamati ya utendaji (uchawi) huwa inatafuta fedha zake za waganga nje ya day to day club operations.
3.Lazima kuwepo na msemaji ambaye hatumii ethics za uanahabari bali ni mipasho na michambo kama inayoendelea sasa kati ya zari na mange, ili kutengeneza hamasa kwa wachezaji na mashabiki nje ya uwanja kabla ya mechi , sasa hivi Yanga imekosa mtu wa namna hiyo baada ya jeri kuondolewa na kabaki manara mwenyewe anatamba atakavyo hana mtu wa kumjibu na inafikia wanataka kumrushia vijembe kocha ili awajibu raha yao itimie
Haya mambo yamekuja siku hizi, hasa kuanzia enzi za JK. Hawa wasemaji ni watu wa siasa tu na ndiyo wanaoharibu mpira wa Tanzania. Hawa wasemaji mara nyingi wanakuwa ni wanasiasa uchwara wanaotumika kupoza madhambi kama ya kuhonga marefa. Simba walijitokeza kwa wingi uwanjani siyo kwa sababu ya Manara, ila kwa sababu timu yao inafanya vizuri hata Manara angepiga kelele vipi, kama timu haifanyi vizuri, watu hawaendi uwanjani.

Wasemaji wa klabu walikuwa ni watu wa heshima sana kwa mfano Yanga walikuwa na Abdul Masoud (RIP) ambaye alikuwa mtangazaji maarufu wa Radio tanzania. Pia amepitia Peter Hassan (RIP) ambaye alikuwa Sports Club Villa ya Uganda kama kiongozi kabla ya kuja Yanga chini ya katibu Bocco.
Kitengo cha usemaji (PR) Yanga kilikuwa na support kubwa kutoka kwa waandishi na watangazaji kama vile Omar Jongo (RIP) na James Nhende kutoka Mfanyakazi. Usiombee ufungwe na Yanga kwenye enzi zao. kitengo cha PR Yanga kilikuwa deep.

Nakwambia haya, ili uondoe dhana kuwa hizi timu ni wahuni waswahili tu wasio na kazi. La hasha, hizi timu huwa zinapangwa na kuendeshwa kiutalaam zaidi ya ujuavyo sema tu kuna watu siku hizi wameuingilia mpira na kuuharibu.
 
Huyo D10 anajidai kuwa anafanya kazi ki-professional eti hataki kuongea hovyo hovyo, hahahha anasahau hizi timu ni za Wazaramo! Siku moja anauliza eti uliwahi kumsikia msemaji wa Barcelona au Liverpool?..

Yaani huyu bwana ni mshamba na hajui anachotakiwa afanye kwa lugha nyepesi ni DHAIFU, mafanikio ya Simba kuingiza mashabiki na kujaza uwanja siyo kwa sababu wana kikosi kizuri au pesa ila hamasa ya Manara kwa mashabiki. Ila D10 yeye kila siku anakaa kuwaza jezi mpya (bure kabisa).

Siku moja nilipata nafasi ya kuingia kwenye vyumba vya kubadilishia nguo vya timu ya Yanga kabla ya mchezo wa ligi kuu. Kuna kiongozi wa Yanga alisema "Tuna msemaji bubu"..

Siku Yanga ikipata njia ya mafanikio huyo D10 atatupwa kama mpira wa kiume uliotumika.

D10 hizi timu zinaendeshwa na roporopo hata ukijidai kuwa unafanya kazi wa professional husaidii lolote, kuna muda unatakiwa utumie taaluma yako kusaidia jamii.

Usemaji wa timu tu shida je kwa mke wake ataongea kweli.
 
Msemaji wenu Zahera hawafai? Sasa nani atakaye wafaa? Basi mumrudishe Muro Jerry
 
Mkuu mbona hata kwenye yale ya msingi kama Kuhamasisha mashabiki kuhusu michango na kufika uwanjani na kutoa updates za wachezaji tetesi za migomo na mambo yahusuyo Club hatumuoni akiwa mbele mbele. Huwezi amini %kubwa yetu wa Yanga hatupati taarifa kutoka kwake. Hakuna updates zozote za upcoming games na ufafanuzi wa games zetu sanjari na kuwapa moyo mashabiki. Mkuu sisi inatuuma sana wasione tupo kimya.
Msemaji anapokea kutoka juu kwa mwenyekiti na kuyafanyia analysis kisha kuyatokea publicity sasa yanga imepwaya iko iko tu ndio maana unamkuta msemaji yuko kimya tusubir baada ya uchaguzi tarehe 5may na yanga kuwa mfumo mzuri nini atafanya sasa hv wako bize na maandaliz ya uchaguzi
 
Msemaji wa Yanga Dismas Ten ndiyo bora kabisa. Enzi za kishenzi na uswahiliswahili wa akina Haji Manara na Jerry Muro sio wakati wake huu. Uswahiliswahili tuwaachie mtaa wa pili.
Dunia ya sasa sio kubwatabwata bila hoja za msingi.
 
Ndugu zangu mm ni mwanaYanga tangu kuzaliwa yaani huyu msemaji wa timu yetu yupo kimya na hamna hamasa zozote kwa timu mimi sioni kazi anayofanya huyu jamaa Mara kumi akapewa Kijana anayejitahidi kuitetea timu na kumpa presha yule mlopokaji wa simba, huyu Dismas ajitafakari sisi tunaichangia club ili ipate maendeleo lkn yy hata kuhamasisha watu kuja uwanjani hakuna.

1. Hatumsikii hata akihamasisha
2. Hatumsikii hata akiongea maendeleo ya timu
3. Hatumsikii hata akihamasisha michango

7 hata kwenye yale ya msingi kama Kuhamasisha mashabiki kuhusu michango na kufika uwanjani na kutoa updates za wachezaji tetesi za migomo na mambo yahusuyo Club hatumuoni akiwa mbele mbele. Huwezi amini %kubwa yetu wa Yanga hatupati taarifa kutoka kwake. Hakuna updates zozote za upcoming games na ufafanuzi wa games zetu sanjari na kuwapa moyo mashabiki. sisi inatuuma sana wasione tupo kimya.
AONDOLEWE
Si mlimsifia anaendesha mambo kisomi??Usomi wa ulaya ktk mazingira ya kizaramo haviendani ndio maana mwisho wa siku mnarudi kusifia Hamshahamsha LA Kizaramo LA Manara.
 
Wasemaji Wa timu ktk nchi zilizoendelea huwa wako ktk staili hyo,wanaongea pale wanapopaswa kuongea hasa ktk mambo muhimu,sema wewe umeshazoea uropokaji na siasa nyingi kama ilivyo hapa bongo. Ushawahi msikia au kumsoma msemaji Wa Man United,Chelsea,Liverpool, n.k? Unadhani hizo timu hazina hao watu? Wapo ila wanajali miiko ya kazi yao na hawapayuki ktk kila jambo. Kuna mambo ya kiutawala zaidi ndipo wanapaswa kuongea zaidi. Bongo hapa msemaji sehemu ya meneja,ni sehemu ya daktari Wa timu,ni sehemu ya HR,ni sehemu ya washabiki na wanachama,ni sehemu ya bodi ya usajili n.k Hata Zahera nae ni mropokaji tu anakosea Mara nyingi
 
Ndugu zangu mm ni mwanaYanga tangu kuzaliwa yaani huyu msemaji wa timu yetu yupo kimya na hamna hamasa zozote kwa timu mimi sioni kazi anayofanya huyu jamaa Mara kumi akapewa Kijana anayejitahidi kuitetea timu na kumpa presha yule mlopokaji wa simba, huyu Dismas ajitafakari sisi tunaichangia club ili ipate maendeleo lkn yy hata kuhamasisha watu kuja uwanjani hakuna.

1. Hatumsikii hata akihamasisha
2. Hatumsikii hata akiongea maendeleo ya timu
3. Hatumsikii hata akihamasisha michango

7 hata kwenye yale ya msingi kama Kuhamasisha mashabiki kuhusu michango na kufika uwanjani na kutoa updates za wachezaji tetesi za migomo na mambo yahusuyo Club hatumuoni akiwa mbele mbele. Huwezi amini %kubwa yetu wa Yanga hatupati taarifa kutoka kwake. Hakuna updates zozote za upcoming games na ufafanuzi wa games zetu sanjari na kuwapa moyo mashabiki. sisi inatuuma sana wasione tupo kimya.
AONDOLEWE
Msemaji wa Man U, Arsenal, Man city umewahi sikia wakipiga vijembe
 
Dismas hatufai ndugu zangu mashabiki wa Yanga tumekuwa qakiwa sana mpaka tunaanza kumkumbuka Jerry Muro
We unaonekana umekulia kwa mtogole unapenda maneno ya shombo
Hovyo sana wewe
Fuatilia afsa habari wa timu kubwa km manchester united au barcelona uone tifauti
 
Mleta mada hivi unajua vyema kazi na job discrimination ya Public Relation Officer???


Acheni kulinganisha taaluma za darasani na hao wakimbia umamde Muro na Manara
 
Msemaji wa Man U, Arsenal, Man city umewahi sikia wakipiga vijembe
Yanga ni timu ya kiafrika lazima iendeshwe kiafrika, usiifananishe na arsenal au man u timu zenye washabiki dunia nzima, msemaji wa yanga hafai
 
Mleta mada hivi unajua vyema kazi na job discrimination ya Public Relation Officer???
Acheni kulinganisha taaluma za darasani na hao wakimbia umamde Muro na Manara
dismas ten hafai, hata updates ya kinachoendelea yanga hatoi
 
Njaa Ndugu Yangu, Dismas Sauti Imekata...
Manara wakati ule wachezaji wa Mikia Wana Hali mbaya hata mikoani wanaenda na basi mbona alikuwa anapiga makelele. .ohh tunaenda FIFA..anakuja na TV kwenye press
 
Mleta mada hivi unajua vyema kazi na job discrimination ya Public Relation Officer???


Acheni kulinganisha taaluma za darasani na hao wakimbia umamde Muro na Manara
Jerry Muro ana Masters Degree
 
Back
Top Bottom