Kero: RITA mna matatizo gani?

Kero: RITA mna matatizo gani?

Kelela

Senior Member
Joined
Nov 7, 2020
Posts
191
Reaction score
308
Habari wana JF,

Naandika uzi huu ili kuelezea kero zangu na wengine wengi kuhusu RITA kama kuna wahusika humu walifanyie kazi.
Natoa kero hizi leo Tarehe 26-Julai-2022

1. Kero ya Kwanza: Namba ya Huduma kwa wateja ni BUTU.

Namba ya Huduma kwa wateja ya RITA haifanyi kazi, yaani ukipiga inaongea matangazo kidogo, ikifika sekunde ya 30 inajikata wenyewe. Tumeshalalamika hili katika social media zao lakini hakuna matokeo.

2. Kero ya Pili: Uchelewaji wa Kupata Cheti cha Kuzaliwa (Online Registration).
Kwa kawaida ilikuw ukiapply cheti cha kuzaliwa mtandaoni inaweza kuchukua wiki 1 hadi 2 au imezidi 3 unapata cheti chako, lakini sasa hivi unaweza kukaa hata miezi miwili na bado haujapata, unaweza kwenda ofisini kwao hata mara 5 au 6 kwa ahadi unazopewa na kila ukienda unapigwa kalenda. Na tatizo hili lipo hata katika kuhakiki vyeti vya kuzaliwa na vifo inachelewa sana siku hizi.

3. Kero ya Tatu: Changamoto ya mfumo.
Changamoto hii ipo kwenye ku-upload attachments, kama umekosea ku-upload attachment tofauti ndio basi tena hauwezi kuiondoa. Ingawa kuna option ya Remove, Lakini ukibonyeza Remove inakuletea ujumbe kuwa Error Occured.

Kama mupo wahusika humu wa RITA wayafanyie kazi hayo, watu wanahangaika, Kwa anayetaka ushahidi wa haya niliyoandika, Ingia Page ya RITA Tanzania Facebook Kisha angalia sehemu ya comments uone watu wanavyolalamika.

Wa salam!
 
Vitu sensitive kama birth certificate achana na habari za online bado hatujafika huko.

Ukienda manual unasubmit tangazo la kizazi unapewa control number ukishalipia unawakabidhi tangazo, risiti na fomu kwenye copy ya risiti wanakuandikia tarehe ya kwenda kuchukuwa cheti.

Yani umekaa subuleni unategemea huduma online bongo?
 
Wafanyakazi hapo ni wavivu,wazembe,wazito

Ova
 
Taasisi imejaa mizee,kazi yao ni kusinzia tu ofisini na kujamba hovyo.
 
Juzi kati nileenda Rita nikakuta jamaa analalamika kuwa wamekosea jina mara ya tatu na viambatanisho anawapa kila wakati jamaa alimaindi kichizi kuwa anaacha kazi anakuja Rita kufuatilia mambo yake na bado wanamletea pigo sio .
 
Mimi wameniudhi sana kwenye namba kama hawatoi hiyo huduma bora wazifute namba zao kuepusha kupotezeana muda .
 
Siyo hawa tu wako pamoja na ndugu yake NIDA yaani tatizo kweli mie kwenye kujiandikisha niliweka kila kitu ajabu kitabulisho kimekuja bila sahihi
 
Mimi wameniudhi sana kwenye namba kama hawatoi hiyo huduma bora wazifute namba zao kuepusha kupotezeana muda .
 
Siyo hawa tu wako pamoja na ndugu yake NIDA yaani tatizo kweli mie kwenye kujiandikisha niliweka kila kitu ajabu kitabulisho kimekuja bila sahihi
Mie hao nida ndio wamenichosha,mwaka wa kuzaliwa wamekosea.
 
Aiseee hizi taasisi ni kero jamani khaaa!


Hivi kinachokwamisha NIDA kutoa ID mapema ni nini?
 
Aiseee hizi taasisi ni kero jamani khaaa!


Hivi kinachokwamisha NIDA kutoa ID mapema ni nini?
Hii inchi ina mambo ya hovyo sana mimi imefika mwaka sasa bado nimeamua kuwasusia tu sijui tatizo nini mpaka kuchelewa hivi ?
 
Taasisi imejaa mizee,kazi yao ni kusinzia tu ofisini na kujamba hovyo.
Daaah,nimecheka kama mazuri,kwa hiyo kazi yao ni kuachia mashuzi tu!!!na mimi nilipeleka maombi ya Death Certificate manually nikaambiwa baada ya wiki mbili niende kitakuwa tayari,nikienda nitaleta mrejesho humu
 
Wahusika hebu fuatilieni hili la RITA, usumbufu umezidi jamani
 
Kuna kitu serikalini kinachofanyika kwa wakati na usahihi zaidi ya mshahara? Sekta nyingi za serikali zina blaah blaah sana
 
Back
Top Bottom