Kero tunazokutana nazo kwenye vibanda umiza

Kero tunazokutana nazo kwenye vibanda umiza

Heshima kwenu wakuu,

Awali ya yote tunamshukuru Mungu kwa kutupa nafasi ya kusonga mbele haswa pale tulipoona kipa anageuzwa tegemeo na wachezaji wote kumi. Mvinyo unapozidi kukaa ndipo unapozidi kuwa mtamu, kongole kwa Juma K. Juma. Kwa kuonesha umwamba na bado unaweza kuwa tegemeo kwa timu na taifa kwa ujumala.niende kwa mada

Kwenye vibanda umiza(vibanda vya kuangalizia mpira) kuna mambo mengi sana mengine yanafurahisha na mengine yanakarahisha.

Yanayokera ni pamoja na kelele nje yakibandaumiza,nilipokuwa-nangalizia kibanda umiza kimetenganishwa na ukuta unaotenganisha kibanda na garage ya magari, basi wale mafundi hupanda kwa juu kuangalia mpira coz juu pako wako wazi, mwenye kibanda umiza akiwa timua, basi wale mafundi wataenda kugonga machuma hata kama hawana kazi ili mradi tu watukere.

Pale ni kahama, nilipohamia pia kero zippo haziepukiki nakomaa nazo, hapa papya mwenye kibanda ni shabiki wa simba basi simba ikifungwa atakosa raha na hata mwishowe anakuwa hayupo active mfano simba ilipotolewa caf jamaa alikuwa hata kuwasha TV on time ni shida kwa mechi zilizofata.

Kingine ni wapo jamaa wana mtindo wa wakunywa soda nakubakiza nusu ndani ya chupa, kisha wanaitegesha kwenye bench, ukija kichwa kichwa ukiimwaga watakuganda uilipe.


Kingine ni wale back benchers, hawa wengi wao wanaingia huku wanasikiliza radio, goli halijaingia kwenye TV wao tayari wanashangilia, sometimes wanakera ila kama ni timu yako imeshinda utawapenda.

Na wewe tiririka kero ya kwako.
#KongoleTaifastaz#
Kero ingine ni pale unapokaa karibu na mtu mwenye midadi. Mpaka mpira uishe unaweza kutoka na ngeo na manundu ya kutosha.
 
Nilipo mimi kero ndogondogo hazikosi lakin ni kibanda umiza poa sana.
Kuna wakati unahisi uko london kabisa kumbe hapahapa kwa Juma Pondamali Mensah.
 
Kinachonikera mimi, watu wanajamba sana, kingine unakuta kuna sreen kama mbili au tatu. Kila mshabiki wa timu labda United au city kila m1 wanataka kuona timu yake. Wakati muda huo kuna game ya kufa mtu kati ya Rojiblanco na Barcelona.

Kingine mashabiki wengi wa aseno wananuka midomo maana hawaongei kwa muda mrefu sababu hawana furaha.

Mwisho kabisa kila tv imefunguliwa sauti tunasikia matangazo ya aina mbili tofauti.
 
Hahaha ananuka mdomo, bila shaka wa man u ananuka kwapa
Kinachonikera mimi, watu wanajamba sana, kingine unakuta kuna sreen kama mbili au tatu. Kila mshabiki wa timu labda United au city kila m1 wanataka kuona timu yake. Wakati muda huo kuna game ya kufa mtu kati ya Rojiblanco na Barcelona.

Kingine mashabiki wengi wa aseno wananuka midomo maana hawaongei kwa muda mrefu sababu hawana furaha.

Mwisho kabisa kila tv imefunguliwa sauti tunasikia matangazo ya aina mbili tofauti.
 
Pole sana mkuu ndio kero yenyewe hiyo
Nimewahi kwenda kagera wilaya ya kyerwa kuna sehemu panaitwa nkwenda....yani ulikua ukiingia kwenye kibanda umiza watu wote wanaongea kinyambo tu..nilikua nakwazika sana yani
 
Ulikuwa masaki nn mkuu kwa vigogo
Kibanda umiza cha hapa mtaan sijaona kero yake aisee hapa huwa Ni full mbilingembilinge za hatar humo ndani burudani safi sana
Projector 2
TV lg 3
game zote live.,, omba timu yako isiwe inapigiwa mpira utataman ukimbie humo ndan !! Nyimbo za hatar

Man u afe, afee [emoji2]

Aagh weekend huwa kunawaka moto mle ndan[emoji2][emoji2]
Missing those moments AF
 
1. Linakuja limtu lireefu wewe umeshakaa na ka nafasi cha uangalia screen umejiwekea linakuziba kabisa

2. Linakuja lingine limevaa kofia linakaa mbele yako huoni tena

3. Lingine linakuja linavua shati kikwapa sasa

4. Linakuja lingine linapiga kelele mwanzo mwisho hata maneno ya mtangazaji husikii

5. Lingine linajifanya linaelekeza wachezaji namna ya kucheza kwa kunyoonya mikono utafikiri picha inamwelewa mwisho wa siku anakuwa anawaziba

6. Lingine linawasha sigara halafu eti linajifanya linapulizia mbali wakati upepo unazunguka mwishowe anawavutisha na wengine

7. Kuna wale wajasiriamali wa kuuza karanga au uji wanapita mbeleyako unakuta ndio kipindi muhuimu anakuziba
 
1. Linakuja limtu lireefu wewe umeshakaa na ka nafasi cha uangalia screen umejiwekea linakuziba kabisa

2. Linakuja lingine limevaa kofia linakaa mbele yako huoni tena

3. Lingine linakuja linavua shati kikwapa sasa

4. Linakuja lingine linapiga kelele mwanzo mwisho hata maneno ya mtangazaji husikii

5. Lingine linajifanya linaelekeza wachezaji namna ya kucheza kwa kunyoonya mikono utafikiri picha inamwelewa mwisho wa siku anakuwa anawaziba

6. Lingine linawasha sigara halafu eti linajifanya linapulizia mbali wakati upepo unazunguka mwishowe anawavutisha na wengine

7. Kuna wale wajasiriamali wa kuuza karanga au uji wanapita mbeleyako unakuta ndio kipindi muhuimu anakuziba
Ha ha ha u make ma day, kiufupi kibanda umiza ni kero, mi najipanga Tu niwe na tv langu nchi 53, na dstv naangalia hme na wife...aaah kibanda umiza hapana Kwa kweli mwishowe unaugua pumu hvi hvi
 
Dstv wameshusha bei funga kwako mkuu, hizi kero zinaboa sana
Hahahha. Home ni hny njoo ukae na mimi au hny nisaidie kuleta kitu chumbani au baba weka katuni au baba huku amekaa mbele ya macho yako .... ndo kero yenye raha yake. Ikiwa timu yako imeshinda, sasa ukifungwa na ni kipind cha kwanza hahahahah
 
Kibanda umiza cha hapa mtaan sijaona kero yake aisee hapa huwa Ni full mbilingembilinge za hatar humo ndani burudani safi sana
Projector 2
TV lg 3
game zote live.,, omba timu yako isiwe inapigiwa mpira utataman ukimbie humo ndan !! Nyimbo za hatar

Man u afe, afee [emoji2]

Aagh weekend huwa kunawaka moto mle ndan[emoji2][emoji2]
Missing those moments AF
Huku unakuta Man U ikifungwa goli watu wanaimba "Maguire kaliwa" au utasikia "Piga Magwaya haoooo!!". Kama ni mshabiki Wa Man U inabidi ubaki unatabasamu tu japo unaumia.
 
Heshima kwenu wakuu,

Awali ya yote tunamshukuru Mungu kwa kutupa nafasi ya kusonga mbele haswa pale tulipoona kipa anageuzwa tegemeo na wachezaji wote kumi. Mvinyo unapozidi kukaa ndipo unapozidi kuwa mtamu, kongole kwa Juma K. Juma. Kwa kuonesha umwamba na bado unaweza kuwa tegemeo kwa timu na taifa kwa ujumala.niende kwa mada

Kwenye vibanda umiza(vibanda vya kuangalizia mpira) kuna mambo mengi sana mengine yanafurahisha na mengine yanakarahisha.

Yanayokera ni pamoja na kelele nje yakibandaumiza,nilipokuwa-nangalizia kibanda umiza kimetenganishwa na ukuta unaotenganisha kibanda na garage ya magari, basi wale mafundi hupanda kwa juu kuangalia mpira coz juu pako wako wazi, mwenye kibanda umiza akiwa timua, basi wale mafundi wataenda kugonga machuma hata kama hawana kazi ili mradi tu watukere.

Pale ni kahama, nilipohamia pia kero zippo haziepukiki nakomaa nazo, hapa papya mwenye kibanda ni shabiki wa simba basi simba ikifungwa atakosa raha na hata mwishowe anakuwa hayupo active mfano simba ilipotolewa caf jamaa alikuwa hata kuwasha TV on time ni shida kwa mechi zilizofata.

Kingine ni wapo jamaa wana mtindo wa wakunywa soda nakubakiza nusu ndani ya chupa, kisha wanaitegesha kwenye bench, ukija kichwa kichwa ukiimwaga watakuganda uilipe.


Kingine ni wale back benchers, hawa wengi wao wanaingia huku wanasikiliza radio, goli halijaingia kwenye TV wao tayari wanashangilia, sometimes wanakera ila kama ni timu yako imeshinda utawapenda.

Na wewe tiririka kero ya kwako.
#KongoleTaifastaz#
Kero kubwa ni Ushuzi.
 
[emoji3][emoji3][emoji3] yote kwa yote ndio raha ya bandani.
Kuna wengine mpira unaisha sauti imemkauka kuongea. Ukipigwa eti dakika ya 80 ukiinuka wanakuzuia hakuna kuondoka.[emoji23][emoji23]
1. Linakuja limtu lireefu wewe umeshakaa na ka nafasi cha uangalia screen umejiwekea linakuziba kabisa

2. Linakuja lingine limevaa kofia linakaa mbele yako huoni tena

3. Lingine linakuja linavua shati kikwapa sasa

4. Linakuja lingine linapiga kelele mwanzo mwisho hata maneno ya mtangazaji husikii

5. Lingine linajifanya linaelekeza wachezaji namna ya kucheza kwa kunyoonya mikono utafikiri picha inamwelewa mwisho wa siku anakuwa anawaziba

6. Lingine linawasha sigara halafu eti linajifanya linapulizia mbali wakati upepo unazunguka mwishowe anawavutisha na wengine

7. Kuna wale wajasiriamali wa kuuza karanga au uji wanapita mbeleyako unakuta ndio kipindi muhuimu anakuziba
 
Back
Top Bottom