Kero za muungano zinaongezeka. Majimbo Z'bar yanawakilishwa na watu wawili bunge la katiba

Kero za muungano zinaongezeka. Majimbo Z'bar yanawakilishwa na watu wawili bunge la katiba

Njaare

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2010
Posts
1,081
Reaction score
275
Wana JF,

Kila kukicha tunaaminishwa kuwa Serikali mbili ndiyo muafaka wa muungano na kero zake zinaweza kushughulikiwa. Ila mimi naona kila kukicha kero hizo zinaongezeka.

Kwenye bunge la katiba Majimbo ya uchaguzi ya Zanzibar yanawakilishwa na watu wawili wawili. Watanganyika wengi wanayaona majimbo ya Zanzibar kuwa yana ukubwa sawa na kata au vijiji vya upande wa Tanganyika.Hata hivyo la kukera zaidi ni kuwa katika bunge la katiba jimbo moja Zanzibar linawakilishwa na mbunge pamoja na mjumbe wa baraza la wawakilishi wakati pamoja na ukubwa wake, majimbo ya Tanganyika yanawakilishwa na mbunge tu.
 
Rasimu ya Judge Warioba ndio mwarobaini wa hayo matatizo. Inalenga kupunguza matatizo mengi yanayoibua kero katika Muungano huo wa Tanganyika na Zanzibar. Poleni sana Watanzania ndio ukubwa huo lakini!
 
Wana JF,

Kila kukicha tunaaminishwa kuwa Serikali mbili ndiyo muafaka wa muungano na kero zake zinaweza kushughulikiwa. Ila mimi naona kila kukicha kero hizo zinaongezeka.

Kwenye bunge la katiba Majimbo ya uchaguzi ya Zanzibar yanawakilishwa na watu wawili wawili. Watanganyika wengi wanayaona majimbo ya Zanzibar kuwa yana ukubwa sawa na kata au vijiji vya upande wa Tanganyika.Hata hivyo la kukera zaidi ni kuwa katika bunge la katiba jimbo moja Zanzibar linawakilishwa na mbunge pamoja na mjumbe wa baraza la wawakilishi wakati pamoja na ukubwa wake, majimbo ya Tanganyika yanawakilishwa na mbunge tu.

Ulitaka iweje mwenzetu kwani hata hivyo bado kutoka Tanganyika ni wengi!
 
Wana JF,

Kila kukicha tunaaminishwa kuwa Serikali mbili ndiyo muafaka wa muungano na kero zake zinaweza kushughulikiwa. Ila mimi naona kila kukicha kero hizo zinaongezeka.

Kwenye bunge la katiba Majimbo ya uchaguzi ya Zanzibar yanawakilishwa na watu wawili wawili. Watanganyika wengi wanayaona majimbo ya Zanzibar kuwa yana ukubwa sawa na kata au vijiji vya upande wa Tanganyika.Hata hivyo la kukera zaidi ni kuwa katika bunge la katiba jimbo moja Zanzibar linawakilishwa na mbunge pamoja na mjumbe wa baraza la wawakilishi wakati pamoja na ukubwa wake, majimbo ya Tanganyika yanawakilishwa na mbunge tu.

Napita njia tu......
 
Napita njia tu......

Nami napita tu, kwa kuwa jua linanichona nasikia kiu, napumzika kivulini nachangia kidogo: kwa kuwa Zanzibar wametunga Katiba kinyemela, wenzao wa Tanganyika imewakera, hivyo nayo ni kero mpya ya Muungano. Napita, naendelea na safari yangu sasa!
 
Wabunge wa ccm wameshakaririshwa cha kusema wawepo kwenye bunge la katiba! Wabunge wa ccm wanakisemea chama chao na sio watanzania wawapo bungeni! Wote wamekaririshwa watetee serikali mbili . Mfumo wa serikali mbili ni wa kuibembeleza zanzibar na kuitokomeza tanganyika!
 
katika bunge la katiba wao kila jimbo znz lina wajumbe 20 walio katika bunge la katiba,wakati kwa uwiano wa idadi ya watu ni kwamba jimbo moja znz unakuja pata wapiga kura elfu 3 wakati kata ya mbagala peke yake ina wapiga kura 4700,kata ya genge ina wapiga kura 2700,je kwanini tanganyika isirudi tukaweka usawa?
 
Yaani. Imagine hayo maneno kama ingekuwa kinyume chake. Ingekuwaje kama bara wangekuwa na wawakilishi wa2 toka kila jimbo? Wangechongaje kama majimbo ya uchaguzi yangekuwa makubwa ( per area and population)? Ingekuwaje kama wao wangetoa rais 1 kati ya hawa waliopo sasa 5, na wa4 watoke Bara? Ingekuwaje marais wote 5 ,. Kikwete hadi akina Seif wangekuwa wote Wakristo.? Basi kwa hayo tuwaombe sana ndugu zetu waache kulalamika kwani wanafaidi muunguno zaidi. Tuishi kwa kuvumiana na uelewa mkubwa.
 
Huu muungano ni kielelezo pekee cha ujinga wa Watanzania kilichobaki hai...
 
Yaani. Imagine hayo maneno kama ingekuwa kinyume chake. Ingekuwaje kama bara wangekuwa na wawakilishi wa2 toka kila jimbo? Wangechongaje kama majimbo ya uchaguzi yangekuwa makubwa ( per area and population)? Ingekuwaje kama wao wangetoa rais 1 kati ya hawa waliopo sasa 5, na wa4 watoke Bara? Ingekuwaje marais wote 5 ,. Kikwete hadi akina Seif wangekuwa wote Wakristo.? Basi kwa hayo tuwaombe sana ndugu zetu waache kulalamika kwani wanafaidi muunguno zaidi. Tuishi kwa kuvumiana na uelewa mkubwa.

Hiyo bara ndio nchi gani?
 
Ni ujinga wa watanganganyika,wazanzibar tunajielewa.

Mngekuwa mnajielewa msingekubali kuwa parasite. Kupe... tena kupe aliyeshika kwenye perennial region. Kama hujui maana ya hilo neno google...
 
Zanzibar wamechukuliwa mpaka wanafunzi wa sekondari kujaza nafasi. Katiba tia maji tia maji.
haya ndio mamabo yanayowashushia sana heshima watawala wa zenj, na kupelekea zenj kuwa n ahatama mbaya sana.Hawajazi nafasi kwa competente persona,na mbaya zaidi hawataki kubali kuwa kuna wakristu wazuri na wenye alimu bora ingawa ni wachache sana. ubaguzi utawatafuna sana
 
Ni lazima kabisa na nadhani wanatunyonya na waende. Hii ni nyumba ndogo sumbufu
 
Huo muungano kwanini tanganyika waung'ag''anie?

Mke mwenyewe tasa! Kupewa talaka hataki! Na kumruhusu mume kuongeza mke pia hataki!

Duhh ama kweli Tanganyika nuksi!
 
Back
Top Bottom