KESHO YA SIMBA NI BORA KULIKO LEO YA YANGA

KESHO YA SIMBA NI BORA KULIKO LEO YA YANGA

Thabit Madai

Member
Joined
Oct 8, 2024
Posts
54
Reaction score
140
FB_IMG_1729409827203.jpg
Ni kweli Simba kafungwa mechi 4 mfululizo na kapoteza ubingwa mara 3 mfululizo lakini haiondoi ukweli kwamba muelekeo wa ni sahihi na wanakaribia kuupata ule ubora wao wa misimu minne iliyopita.

Simba kwa sasa haifungwi kwa makosa ya kiufundi ya Timu nzima bali inafungwa kwa makosa ya kibinadamu ya mchezaji mmoja mmoja kitu ambacho timu yoyote inaweza kupitia hiyo hali.

Tazama magoli yaliyoikesha alama 2 za Coastal Union kisha tazama bao la jana utagundua kwamba magoli waliyofungwa sio ya kitimu.

Hii ni hatua nzuri kwa ujenzi wa Timu na wanapaswa kutulia na kuongeza wachezaji wachache sana kwenye usajili dirisha lijalo.

Ukitoa bao la kujifunga hakuna moment ambayo Simba walionekana kuzidiwa na kuonesha utofauti wa daraja la ubora kati yao na Yanga ambao wana kikosi kilichokaa pamoja kwa muda mrefu.

Wakati Simba wanaanza kushuka na Yanga kutawala soka la Tanzania hivi karibuni dalili zilikuwa hizi hizi...kutoka kushinda kwa mbwembwe hadi kuomba Mungu mechi iishe.

Siku za mashabiki wa Simba kufurahi haziko mbali...na siku za mashabiki wa Yanga kutoka kinyonge Lupaso zipo karibuni.

Inaweza isiwe leo au kesho lakini hata Yanga wenyewe wanajua kuwa Simba hii sio ya miaka miwili nyuma...wameimarika sana!

✍️Sospeter Ilagila.
 
View attachment 3130558Ni kweli Simba kafungwa mechi 4 mfululizo na kapoteza ubingwa mara 3 mfululizo lakini haiondoi ukweli kwamba muelekeo wa ni sahihi na wanakaribia kuupata ule ubora wao wa misimu minne iliyopita.

Simba kwa sasa haifungwi kwa makosa ya kiufundi ya Timu nzima bali inafungwa kwa makosa ya kibinadamu ya mchezaji mmoja mmoja kitu ambacho timu yoyote inaweza kupitia hiyo hali.

Tazama magoli yaliyoikesha alama 2 za Coastal Union kisha tazama bao la jana utagundua kwamba magoli waliyofungwa sio ya kitimu.

Hii ni hatua nzuri kwa ujenzi wa Timu na wanapaswa kutulia na kuongeza wachezaji wachache sana kwenye usajili dirisha lijalo.

Ukitoa bao la kujifunga hakuna moment ambayo Simba walionekana kuzidiwa na kuonesha utofauti wa daraja la ubora kati yao na Yanga ambao wana kikosi kilichokaa pamoja kwa muda mrefu.

Wakati Simba wanaanza kushuka na Yanga kutawala soka la Tanzania hivi karibuni dalili zilikuwa hizi hizi...kutoka kushinda kwa mbwembwe hadi kuomba Mungu mechi iishe.

Siku za mashabiki wa Simba kufurahi haziko mbali...na siku za mashabiki wa Yanga kutoka kinyonge Lupaso zipo karibuni.

Inaweza isiwe leo au kesho lakini hata Yanga wenyewe wanajua kuwa Simba hii sio ya miaka miwili nyuma...wameimarika sana!

✍️Sospeter Ilagila.
Hahaaaaaaaaaaaa.....
 
True ukizingatia quality za kina Aziz Ki, Pacome na Aucho unaona zina panda shuka muda si mrefu tutaanza kwenda nao sawa
Azizi Ki
Musonda
Chama
Bacca
Dube
Mudathir
Mzize
Diarra
Job
Abuya

Hawa wote wametoka kukipiga dhidi ya mechi ngumu za kufuzu AFCON na wamekuja mafungu mafungu wengine wamekuja siku ya mechi kutoka safarini lakini mmeshindwa kuwafunga pamoja na kuwa na fatigue pia na kukosa maandalizi ya kutosha ya mechi. Hamna kitu zaidi ya kukamia mechi tu kama wanavyofanya wakina Ken Gold tu
 
Simba tupo vizuri mno ,mambo mazuri yanakuja ,tuwe wavumilivu tu.
Yaani kipimo chenu ni Yanga, kwenye mechi ya ngao ya jamii maneno yakawa hayo hayo kuwa 'Tunaona mwanga' tunaelekea pazuri, tumecheza vizuri lakini Dodoma jiji na Coastal union wakawafanya mjitafakari na upya. Ila leo mmeibuka tena baada ya wachezaji wenu kukamia mechi dhidi ya timu inayoongelewa ina quality players
 
Yaani kipimo chenu ni Yanga, kwenye mechi ya ngao ya jamii maneno yakawa hayo hayo kuwa 'Tunaona mwanga' tunaelekea pazuri, tumecheza vizuri lakini Dodoma jiji na Coastal union wakawafanya mjitafakari na upya. Ila leo mmeibuka tena baada ya wachezaji wenu kukamia mechi dhidi ya timu inayoongelewa ina quality players
Kwamba unataka niongee kama wewe unavyotaka? Wewe ndio ujitafakari mkuu.
 
Kwamba unataka niongee kama wewe unavyotaka? Wewe ndio ujitafakari mkuu.
Kwakweli inabidi nijitafakari kwanini Simba wanafungwa mara 4 mfululizo wakati Yanga ikiwa unga na wanajitafuta kipindi hicho hakuwa wanyonge kiasi cha kukubali kuwa wateja wa kufungwa tu kila mchezo na Simba. Najitafakari sana mkuu huyu Gamondi mh!
 
View attachment 3130558Ni kweli Simba kafungwa mechi 4 mfululizo na kapoteza ubingwa mara 3 mfululizo lakini haiondoi ukweli kwamba muelekeo wa ni sahihi na wanakaribia kuupata ule ubora wao wa misimu minne iliyopita.

Simba kwa sasa haifungwi kwa makosa ya kiufundi ya Timu nzima bali inafungwa kwa makosa ya kibinadamu ya mchezaji mmoja mmoja kitu ambacho timu yoyote inaweza kupitia hiyo hali.

Tazama magoli yaliyoikesha alama 2 za Coastal Union kisha tazama bao la jana utagundua kwamba magoli waliyofungwa sio ya kitimu.

Hii ni hatua nzuri kwa ujenzi wa Timu na wanapaswa kutulia na kuongeza wachezaji wachache sana kwenye usajili dirisha lijalo.

Ukitoa bao la kujifunga hakuna moment ambayo Simba walionekana kuzidiwa na kuonesha utofauti wa daraja la ubora kati yao na Yanga ambao wana kikosi kilichokaa pamoja kwa muda mrefu.

Wakati Simba wanaanza kushuka na Yanga kutawala soka la Tanzania hivi karibuni dalili zilikuwa hizi hizi...kutoka kushinda kwa mbwembwe hadi kuomba Mungu mechi iishe.

Siku za mashabiki wa Simba kufurahi haziko mbali...na siku za mashabiki wa Yanga kutoka kinyonge Lupaso zipo karibuni.

Inaweza isiwe leo au kesho lakini hata Yanga wenyewe wanajua kuwa Simba hii sio ya miaka miwili nyuma...wameimarika sana!

✍️Sospeter Ilagila.
Ulilosema ni kweli. Bado kama mechi Tatu tu. Yanga wataifunga Simba mechi 7 mfululizo baada ya hapo Simba watapata ushindi.
 
Back
Top Bottom