Kesi maarufu zilizowahi kutokea ndani ya Tanzania

Kesi maarufu zilizowahi kutokea ndani ya Tanzania

Mchochezi

JF-Expert Member
Joined
Feb 29, 2012
Posts
10,962
Reaction score
7,830
Habari za muda huu wana JF, Naomba tupeane habari kuhusu baadhi ya kesi maarufu zilizowahi kutokea ndani ya Tanzania ambazo kwa kiasi fulani zilitikisa na sasa zinatumika katika maamuzi ya kesi nchini.

Mfano:

Saidi Mwamwindi vs Republic (1972) HCD, Ambayo mkulima Saidi Mwamwindi alimuua mkuu wa mkoa Iringa Dr. Kleruu na kuhukumiwa kifo.

Bi Hawa Mohamed Vs Ally Sefu [1983] TLR 32,


Ni hukumu muhimu na maarufu kuliko zote pale linapokuja suala la migogoro ya wana-ndoa wanaotaka kutalikiana na pia suala zima la ugawanaji mali pale mahakama inaporidha talaka itolewe na ndoa hiyo ihesabike kwamba imeshindwa kuhimi mikikimikiki ya kutoelewana. nazungumzia hapo tamu inayogeuka kuwa shubiri baadaye.

Hukumu huu ilitolewa mwaka 1983 na Jopo la Majaji Watatu wa Mahakama ya Rufaa Tanzania (Jaji Mkuu Nyalali, kama alivyokuwa wakati ule, Jaji Lewis Makame na Jaji Robert Kisanga). Mengi yalizungumzwa humo na kinachoskikitisha hata baadhi ya wanasheria wameilewa vibaya hukumu hii kwa kutoisoma kwa umakini neno kwa neno, aya kwa aya. Inatosha tu kusema kuwa kikubwa kilichoelekezwa hapo ni kwamba mama wa nyumbani anastahili kupata mgawo katika mali iliyochumwa na wanandoa hata kama kazi alizofanya ni za nyumbani tu na mumewe haijalishi alikuwa akikesha akirusha ndege, katika vikao vya mawaziri, kwenye dili kubwa ama safari za ki-biashara ana kazi nyinginezo, iweza kitaalam ama za suluba. Nikumbushe tena, jambo hili lisieleweke kijumla jumla tu hivyo, mahakama ilitoa ufafanuzi zaidi katika hili na sitaweza kutazungumza yote hapa.

Kesi hii ni muhimu kwa vile Mahakama hii ikiwa ni ya Juu zaidi Kikatiba na ambayo hukumu zake zapaswa kufuatwa na mahakame zote chini yake (katika tafsiri ya sheria husika). Ndiyo kusema,Jaji wa Mahakama Kuu, Hakimu wa Mahakama ya Wilaya au Ilala na wengineo wanatarajiwa kuzingatia msingi uliwekwa hapo.


Wakuu naomba tuongeze nyingine.
 
Legal and Human Rights Center and 210 Others Vs Attorney General And others ni moja Wapo mkuu! Maarufu kama nyamuma case
 
habari za muda huu wana JF, Naomba tupeane habari kuhusu baadhi ya kesi maarufu zilizowahi kutokea ndani ya Tanzania ambazo kwa kiasi fulani zilitikisa Nchi, Mfano: Kesi ya Mkulima Mwamindi kumuua RC wake Dr. Kleruu. Karibuni wadau ili tuelimishane...

Naunga mkono hoja, hii kesi napenda sana kuijua, mwenye kujua msaaada plz!!
 
habari za muda huu wana JF, Naomba tupeane habari kuhusu baadhi ya kesi maarufu zilizowahi kutokea ndani ya Tanzania ambazo kwa kiasi fulani zilitikisa Nchi, Mfano: Kesi ya Mkulima Mwamindi kumuua RC wake Dr. Kleruu. Karibuni wadau ili tuelimishane...

Kesi ipo hivi SAID MWAMWINDI V/R(1977)
 
Kesi ya mauaji ya kamanda LIEUTENANT GENERAL kombe na maafisa wa polisi ambao ni juma nswa na mattab, JUMA NSWA&MATTABA V/R(1995) , na kuna kesi ya mke wa kamanda kombe ya kudai fidia dhidi ya kifo cha mumewe inaitwa ROSSELEEN KOMBE AS THE ADMINISTRATIX OF THE ESTATE OF THE LATE LIEUTENANT GENERAL IMRAN HUSSEIN KOMBE V/S ATTONEY GENERAL(1999)
 
naunga mkono hoja, hii kesi napenda sana kuijua, mwenye kujua msaaada plz!!

Kuna kesi nyingine ya KABULUNGU JUMA V/S REPUBLIC huyu jamaa alikuwa mganga wa kienyeji alimlaghai mwanamke ambaye alikuwa anataka kupata mtoto afanye nae mpenzi ndio atapata mtoto
 
Kesi ya mauaji ya kamanda LIEUTENANT GENERAL kombe na maafisa wa polisi ambao ni juma nswa na mattab, JUMA NSWA&MATTABA V/R(1995) , na kuna kesi ya mke wa kamanda kombe ya kudai fidia dhidi ya kifo cha mumewe inaitwa ROSSELEEN KOMBE AS THE ADMINISTRATIX OF THE ESTATE OF THE LATE LIEUTENANT GENERAL IMRAN HUSSEIN KOMBE V/S ATTONEY GENERAL(1999)
Hii kesi naitafuta sana walau nipate dondoo nini kilijiri
 
Kuna kesi nyingine ya KABULUNGU JUMA V/S REPUBLIC huju jamaa alikuwa mganga wa kienyeji alimlaghai mwanamke ambaye alikuwa anataka kupata mtoto afanye nae mpenzi ndio atapata mtoto

mkuu funguka sana, maana tunahitaji kuyajua haya mambo, plz ukipata muda funguka mkuu
 
hii kesi naitafuta sana walau nipate dondoo nini kilijiri

nimerudi nlipigwa ban! haya ngoja tuijadili kesi ya JUMA NSWA&MATTABA V/S REPUBLIC(1995),hawa walikuwa maofisa wa jeshi la polisi walitumwa kutoka dar kwenda moshi kutafuta/kufuatilia gari aina ya NISSAN PATROL mali ya mfanyabiashara anayeitwa MR.LADWA lililokuwa limeibiwa na majambazi jijini dar na kukimbia nalo mkoani kilimanjaro sasa basi jeshi la polisi mkoani dar likawatuma maofisa wa polisi wawili ambao ni MR.JUMA NSWA na MATTABA ili kwenda mkoani KILIMANJARO kuungana na polisi wengine watatu kutoka mkoani KILIMANJARO sasa wakati wanafuatilia lile gari lililoibiwa na majambazi kuna gari jingine ambalo alikuwa anaendesha LIEUTENANT GENERAL,IMRAN HUSSEIN KOMBE na ROSSELEEN KOMBE(mkewe) sasa lile gari la KAMANDA KOMBE lilikuwa linafanana sana na lile liloibiwa na majambazi dar hivyo maofisa wa polisi wakalipiga risasi wakidhan ndio la majambazi hivyo kamanda kombe akatoka nje na kujisalimisha lakin akapigwa risasi
 
mkuu funguka sana, maana tunahitaji kuyajua haya mambo, plz ukipata muda funguka mkuu

Kesi ya KABULUNGU JUMA V/S REPUBLIC huyu alikuwa mganga wa kienyeji sasa kulikuwa na mwanamke ambae alikuwa hanauwezo wa kuzaa(mgumba) hivyo basi akaenda kwa mganga ili amsaidie apate mtoto (azae) hivyo huyo mganga wa kienyeji(KABULUNGU) akamwambia yule mwanamke kwamba ili awe na uwezo wa kuzaa itabidi afanye nae ngono ili apate mtoto kwa sababu alikuwa na uhitaji mkubwa sana wa mtoto sasa wakafanya mapenzi mwanamke baada ya kuona hamna mimba akaenda akaripoti kwamba amebakwa na mganga wa kienyeji KABULUNGU JUMA akashitakiwa kwa kosa la ubakaji
 
Back
Top Bottom