Kesi ya Mbowe: Commando Mhina, Shahidi Mwaminifu na Rafiki wa Kweli

Kesi ya Mbowe: Commando Mhina, Shahidi Mwaminifu na Rafiki wa Kweli

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Komando Mhina popote pale alipo na apokee salamu za kheri kutoka kwetu tunaoyaishi machungu yao.

Akiwa mtu huru, Commando Mhina alifika mahakamani kufanya sehemu yake ya kuuanika ukweli.

"Kwani nani anapenda kufika kwa ridhaa yake polisi au katika mahakama zinazosifika kwa dhuluma?"

"Kwa nini Commando Ling'wenya au awaye yote ahukumiwe kwa ushahidi wa uongo?"

Kama ilivyokuwa kwa ma Commando Ling'wenya, Adamoo, Malema, Urio, na Lijenje, Commando Mhina pia alikamatwa na kundi la akina Kingai, Jumanne, Mahita na Goodluck.

"Akihojiwa na wakili msomi Peter Kibatala 5/11/2021," Mahita Omar Mahita alikiri:

IMG_20211203_155048_030.jpg


Kwa maelezo ya Commando Mhina, kulikuwa na convoy kubwa kwenye kukamatwa kwake iliyokuwapo hapo bila kujihusisha moja kwa moja. Ikiwa tayari tayari kama angejaribu kujitetea.

Kwenye mazingira kama hayo haipo namna ambayo Commando Lijenje angeweza kutoweka RAU madukani.

IMG_20211015_144814_546.jpg


Commando Mhina alikamatwa akielekea Pub akapelekwa Central Polisi Tabora, moja kwa moja kwenye kinyumba nyuma ya jengo kuu (main block) kwenda kuteswa.

Baada ya kipigo kikali (cha masaa yasiyopungua 3) alipelekwa mahabusu Tabora Railways alikokaa kwa siku 2, kabla ya kuhamishiwa Nzega polisi mahabusu, alikokaa kwa siku 3.

Nzega, Mhina alikutana pia na Commando Malema aliyekuwa kaletwa hapo mahabusu polisi kwenye mazingira kama aliyofikishwa nayo hapo, yeye.

Makomando wawili hawa walisafirishwa kuja Dar chini ya ile ile himaya pendwa ya akina Kingai, Jumanne, Mahita, na Goodluck, ambako walifikishiwa 23/9/2020 moja kwa moja mahabusu Polisi Tazara.

Tokea 19/9/2020 Commando Mhina alipokamatwa na kufungwa pingu, hakuwahi kufunguliwa pingu hizo wala kupewa chakula hadi alipopelekwa mahakamani kisutu 25/9/2020.

Katika kipindi chote hicho hakuwahi kusajiliwa katika kitabu au register yoyote popote.

Wana nini cha kumwambia nani dhidi ya nani kina Kingai, Mahita, Jumanne au Goodluck naye akawaamini?

Bila shaka ni watu hawa hawa walio mkamata pia Mh. Mbowe usiku usiku Mwanza na kumsafirisha kuja naye Dar kibazazi wakimwahidi kuwa safari hii hachomoki.

Wapongezwe wote wanaokuwa na ujasiri wa kusimama imara kuufichua uongo dhidi ya ukweli.

Maisha na haki za watu haziwezi kuchezewa kwa kisingizio cha jina "serikali" kwa kiwango hiki. Kwani serikali hiyo itakuwa ina mwakilisha nani?

Nani kama Commando Mhina?

"Kudos Commando Mhina. Kwa hakika wewe ni shahidi wa haki na Rafiki mwema."

"Kwa hakika wapenda haki wote tutasimama nanyi kuona haipo haki yenu moja itakayopotea."

-----------
Sauti na Zipazwe Zaidi:

"Wako wapi makomando wetu. Wako wapi Urio, Malema na Lijenje ambao tunajua mara ya mwisho walikuwa mikononi mwa Kingai."
 
Nimehuzunika zaidi nilipohisi hata wakati huu ninapokusoma hapa brazaj inawezekana wapo wengi wanaoteswa kwa namna hii uliyoandika hapa na hawana mtetezi.

Hawa makomandoo walikamatwa na kuteswa tangu mwaka jana, hivi kama sio Mbowe kuunganishwa nao baada ya kumkera yule bosi mwenye jinsia ya kike wangeendelea kuteswa mpaka lini?
 
Umeandika nini sasa hapo? Huyo Komando uchwara ni unfit kwa wale wako jeshini watajua vizuri maana ya Unfit. Ndiyo maana alifukuzwa Jeshini na ndiyo maana tena akalengeshwa na Urio kwa Gaidi Mbowe.

Komando kweli kweli hafukuzwi Jeshini akifanya makosa ya nidhamu anafungwa huko huko Jeshini na ikibidi kama bado anazigua anapelekwa vitani akakione chamoto, nafikiri unajua ninaposema vitani!!

Makomando walikuwa wakina Tamimu hata ukamataji wao ulikuwa kimbembe siyo hao wanakamatwa Rau sokoni hahahahaha... hapo kuna shield kibao tena wanakamatwa na askari watatu tu mmmmmh. Hao ni unfit commandos!!

Madawa ya kulevya yalishawamaliza stamina pamoja na uwezo wa akili zao za kufikiria ndio maana Urio akamwingiza mkenge Gaidi Mbowe.
 
Nimehuzunika zaidi nilipohisi hata wakati huu ninapokusoma hapa brazaj inawezekana wapo wengi wanaoteswa kwa namna hii uliyoandika hapa na hawana mtetezi.

Hawa makomandoo walikamatwa na kuteswa tangu mwaka jana, hivi kama sio Mbowe kuunganishwa nao baada ya kumkera yule bosi mwenye jinsia ya kike wangeendelea kuteswa mpaka lini?

Kama ilivyo katika uzi huu:

Kesi ya Mbowe: Yatokanayo, yasipuuziwe

Ifanyike sensa kulifahamu ukubwa na kulitanzua tatizo hili.
 
Mimi nawasifu makomandoo hawakukubali kuingia mkenge. Maana wangesema wajibu mapigo wangeuwawa halafu ingetangazwa ni magaidi.

Kwa hivyo kesi ya mbowe ingekuwa ngumu maana ingeonekana walikuwa na mpango muovu na kukata kukamatwa.

Kitendo Cha makomandoo kukubali kukamatwa na polisi bila kujibu mapigo, ni ushindi mkubwa na ishara ya kwamba hawakuwa na Nia mbaya.

Big up makomandoo mlicheza vizuri Sana ndio maana kesi imekuwa ngumu kwao mpaka wameomba msaada wa Jaji.
 
Polisi wana kinga?
RC na DC wana kinga?
Zakutokushitakiwa?

Sabaya alijua ipo siku radiocall zitakuwa over?
Sabaya alijua wakili wa serikali ndiye atakuja mkandamiza?
Sabaya alijua mawakili wakujitegemea watakuwa msaada kwake?
Usimtumikie mwanasiasa,itumikie jamii kwa mujibu wa sheria za Nchi
 
Mimi nawasifu makomandoo hawakukubali kuingia mkenge. Maana wangesema wajibu mapigo wangeuwawa halafu ingetangazwa ni magaidi. Kwa hivyo kesi ya mbowe ingekuwa ngumu maana ingeonekana walikuwa na mpango muovu na kukata kukamatwa. Kitendo Cha makomandoo kukubali kukamatwa na polisi bila kujibu mapigo, ni ushindi mkubwa na ishara ya kwamba hawakuwa na Nia mbaya. Big up makomandoo mlicheza vizuri Sana ndio maana kesi imekuwa ngumu kwao mpaka wameomba msaada wa Jaji.

Dalili ya kuwa makomando hawa wako highly disciplined wala hawakuwa na cha kufanya na kitu kinaitwa ugaidi.

Hawa walikuwa wanajitafutia ajira wakiwa wametelekezwa na nchi yao wenyewe.

Ifanyike sensa kwa demobilized commandos wote:

Kesi ya Mbowe: Yatokanayo, yasipuuziwe

Kwenye viroba kunatia shaka:

IMG_20211202_092804_863.jpg
 
Vp we mjane mbna umechanganyikiwa hv?????yule iblis ndio ameshakufa na analamba udongo
Umeandika nini sasa hapo? Huyo Komando uchwara ni unfit kwa wale wako jeshini watqjua vizuri maana ya Unfit. Ndiyo maana alifukuzwa Jeshini na ndiyo maana tena akalengeshwa na Urio kwa Gaidi Mbowe. Komando kweli kweli hafukuzwi Jeshini akifanya makosa ya nidhamu anafungwa huko huko Jeshini na ikibidi kama bado anazigua anapelekwa vitani akakione chamoto, nafikiri unajua ninaposema vitani!! Makomando walikuwa wakina Tamimu hata ukamataji wao ulikuwa kimbembe siyo hao wanakamatwa Rau sokoni hahahahaha... hapo kuna shield kibao tena wanakamatwa na askari watatu tu mmmmmh. Hao ni unfit commandos!! Madawa ya kulevya yalishawamaliza stamina pamoja na uwezo wa akili zao za kufikiria ndio maana Urio akamwingiza mkenge Gaidi Mbowe.
 
Umeandika nini sasa hapo? Huyo Komando uchwara ni unfit kwa wale wako jeshini watqjua vizuri maana ya Unfit. Ndiyo maana alifukuzwa Jeshini na ndiyo maana tena akalengeshwa na Urio kwa Gaidi Mbowe. Komando kweli kweli hafukuzwi Jeshini akifanya makosa ya nidhamu anafungwa huko huko Jeshini na ikibidi kama bado anazigua anapelekwa vitani akakione chamoto, nafikiri unajua ninaposema vitani!! Makomando walikuwa wakina Tamimu hata ukamataji wao ulikuwa kimbembe siyo hao wanakamatwa Rau sokoni hahahahaha... hapo kuna shield kibao tena wanakamatwa na askari watatu tu mmmmmh. Hao ni unfit commandos!! Madawa ya kulevya yalishawamaliza stamina pamoja na uwezo wa akili zao za kufikiria ndio maana Urio akamwingiza mkenge Gaidi Mbowe.
Sawa ni unfit commandos lakini huo u unfit waliupatia wapi? Wakati wanaingia jeshini walikuwa unfit? Anyway at least wametumia sehemu ya maisha yao kwenye ulinzi wa taifa letu maana wengine wameenda mpaka Congo na Sudan kwenye peacekeeping mission. Wewe una lipi umefanya kwa taifa hili zaidi ya kudandia hoja za hapa na pale ili utupiwe mifupa utafune??
 
Sawa ni unfit commandos lakini huo u unfit waliupatia wapi? Wakati wanaingia jeshini walikuwa unfit? Anyway at least wametumia sehemu ya maisha yao kwenye ulinzi wa taifa letu maana wengine wameenda mpaka Congo na Sudan kwenye peacekeeping mission. Wewe una lipi umefanya kwa taifa hili zaidi ya kudandia hoja za hapa na pale ili utupiwe mifupa utafune??
Mpuuze huyo mkuu namjua vizur tu anaishi kwa dada yake chumba na sebule Mwananyamala.
 
Back
Top Bottom