Kesi ya Mbowe kesho: Kisutu hapatatosha, maandalizi yanaogofya

Kesi ya Mbowe kesho: Kisutu hapatatosha, maandalizi yanaogofya

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Kesho tarehe 5/8/2021, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, itatajwa kesi ya jinai inayomjumuisha Mwenyekiti wa Taifa CHADEMA Ndugu Freeman Aikaeli Mbowe. Mbowe pamoja na wenzake watatu wanashtakiwa kwa makosa mbalimbali ya kijinai.

Kwake binafsi, Mbowe anashtakiwa kwa mashtaka ya kula njama na kufadhili vitendo vya kigaidi. Washtakiwa wenzake walianza kupandishwa kizimbani huku Mbowe akiunganishwa baadaye.

Maandalizi ya tukio la kesho yameshafanyika na kukamilika. Magereza alipo, wamejipanga na kupangika kuhakikisha kuwa Mbowe na wenzake wanafikishwa na kurejeshwa salama salmini gerezani.

Polisi wamejipanga, kuanzia nchi kavu hadi anga, kuimarisha ulinzi bila ulanzi kuhakikisha usalama usio na lawama mahakamani hapo. Polisi wamejiandaa 'kuwahi' mapema sehemu ya tukio ili 'kukagua' na 'kudhibiti' wanaoingia mahakamani hapo.

Mawakili wa pande zote mbili wamejipanga bila mapanga kutetea pande zao za mashtaka na utetezi kusiko na utelezi. Mawakili wa Serikali wamejiandaa kuthibitisha makosa ya Mbowe na wenzake watatu huku wa CHADEMA wakijiandaa kumtetea kisheria Mbowe na kumnasua kwenye kesi hiyo.

Vyombo vya habari vya ndani na nje vitafurika hadi kufunika Kisutu. Nasi wananchi wa Dar es Salaam tutajongea kushuhudia 'kipute' hiki kitakachoanza kesho.

Amini nawaambia, Kisutu kwa kila siku Mbowe atakayoletwa na hata akianza kupelekwa Mahakama Kuu, hapatatosha. Mahakamani, pumba na mchele vitatenganishwa. Tukutane Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kesho.

Pumzika kwa amani mtani na mdogo wangu Elias Kwandikwa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Kesho tarehe 5/8/2021, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, itatajwa kesi ya jinai inayomjumuisha Mwenyekiti wa Taifa CHADEMA Ndugu Freeman Aikaeli Mbowe. Mbowe pamoja na wenzake watatu wanashtakiwa kwa makosa mbalimbali ya kijinai.
Baba yangu Mzee Tupatupa shikamoo.

Kwa sasa nchi ingejikita kuwaleta Toyota au Suzuki ili wafungue kiwanda cha low cost, and lowly priced autos hapa nchini ili kuongeza FDIs. Kesi ya mbowe inatuchafua tu kwa potential foreign investors unnecessarily.

Fatma,
Kwa sasa Doha.
 
Baba yangu Mzee Tupatupa shikamoo.

Kwa sasa nchi ingejikita kuwaleta Toyota au Suzuki ili wafungue kiwanda cha low cost, and lowly priced autos hapa nchini ili kuongeza FDIs. Kesi ya mbowe inatuchafua tu kwa potential foreign investors unnecessarily.

Fatma,
Kwa sasa Doha.
Hata kwenye issue za Ndege mlianza hivi hivi,

Oooh! Rwanda wana Ndege ila sisi hatuna,sasa mmeona kiwanda cha VW huko Rwanda,mnaanza tena mnataka na Bongo kifunguliwe kiwanda cha magari,

Sio mbaya ila hata kikifunguliwa kiwanda mtakuja tena kukipinga hicho kiwanda kama mnavyozipinga Ndege,

Hua hamueleweki mnachokitaka ni nini hasa,kingine kila nchi hua na mipango yake,sio kwavile Rwanda wana hicho kiwanda cha magari basi ni lazima na Tz iwe na kiwanda cha magari.
 
Hata kwenye issue za Ndege mlianza hivi hivi,

Oooh! Rwanda wana Ndege ila sisi hatuna,sasa mmeona kiwanda cha VW huko Rwanda,mnaanza tena mnataka na Bongo kifunguliwe kiwanda cha magari,

Sio mbaya ila hata kikifunguliwa kiwanda mtakuja tena kukipinga hicho kiwanda kama mnavyozipinga Ndege,

Hua hamueleweki mnachokitaka ni nini hasa,kingine kila nchi hua na mipango yake,sio kwavile Rwanda wana hicho kiwanda cha magari basi ni lazima na Tz iwe na kiwanda cha magari.
Sisi ndiyo tulikuwa wa kwanza kutaka kuanzisha kiwanda, nakumbuka ilikuwa Suzuki, huko Dodoma. Mipango ilikwenda vizuri. Wapuuzi wachache wakaishauri serikali iache maana itakosa kodi za ku-import magari. Poor us!
 
Baba yangu Mzee Tupatupa shikamoo.

Kwa sasa nchi ingejikita kuwaleta Toyota au Suzuki ili wafungue kiwanda cha low cost, and lowly priced autos hapa nchini ili kuongeza FDIs. Kesi ya mbowe inatuchafua tu kwa potential foreign investors unnecessarily.

Fatma,
Kwa sasa Doha.
I blame tiss to allow this stupidity! Una brand taifa lako kwa ugaidi??? Ndio Tz mpya ya Mama Samia??? Madam Mulamula msitue MAMA! International media watarusha wengi hawafatilii details only heading! " Tanzania main oppotion leader charged with terror charges..."
Tunahitaji vifaa tiba maboma ya JPM, jumuia za kimataifa zipo tayari.Tuache ujinga na mzaha wa ajabu.
 
Nitakuja kipalestina manati marumaru au goroli mfukoni ole wao nisikie mlio .
 
Back
Top Bottom