Kesi ya Mbowe: Madai Mahakamani yathibitishwe Kisayansi

Kesi ya Mbowe: Madai Mahakamani yathibitishwe Kisayansi

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Leo kumekuwapo shahidi mahakamani kuonyesha Ling'wenya hakuwahi kufikishwa Tazara Polisi.

Shahidi huyu ana anayodai kuwa ni detention register kama ushahidi. Baadhi ya kurasa zake zimenyofolewa na nyingine zimeongezwa.

Si mageni kusikia polisi wamebambikizia watu kesi, wamewaweka watu rumande kwa majina bandia au hata bila kuwaandikisha kabisa.

Yamewakuta kina Mdude, kina Ulimboka na wengi wengine. Yumkini kina Ben, Lijenje au hata Azory ni hali hizo hizo. Ni hakika kwa maneno ya Sirro kuwa:

"Polisi hawa siyo malaika."

Haki za watu haziwezi kuendelea kuchezewa hivi.

Kwa maana halisi ya haki, kwa nini ushahidi wa kisayansi uliopo usitumike kutenganisha mbivu na mbichi hizi?

Ushahidi wa ma CCTV lukuki yaliyoko sehemu mbalimbali na pia kutokea kwenye makampuni ya simu za mkononi mbona upo?

Kwa vile ushahidi huu ni bora zaidi, hazipo sababu ya kutokuuhitaji ili kutumika mahakamani?

Nyendo kamili za Kingai, Mahita, Jumanne, Goodluck na timu nzima tokea RAU hadi Mbweni ni muhimu kuhakikiwa zaidi ya maneno yao.

Mahakamani kusifanywe kuwa kichaka cha kupitishia uongo dhidi ya watu wengine.

Maneno ya mtu dhidi ya mwingine, kwa "litmus paper" ipi kuthibitisha mwongo ni yupi?
 
Hawataki kutumia ushahidi wa aina hiyo kwasababu wanajua wataumbuka, ndio maana kwenye lile pingamizi la mwanzo kabisa jaji aliyekuwepo aligoma kuchukua ushahidi wa majeraha aliyokuwa nayo mmoja kati ya watuhumiwa (sikumbuki vizuri alikuwa yupi kati ya Lijenje au Adamoo), akijua fika kwa kumpeleka hospitali akapimwe ingeonekana kweli alipigwa akiwa mikononi mwa polisi.
 
CCM kwa mgongo wa Jamuhuri wanaiabisha Tanzania!

Hata kwenye mkutano wa njia ya video tumepigwa chini kama Rwanda, Zimbabwe, Mozambique, Burundi na Uganda.

Kenya, Malawi, Zambia na Afrika Kusini kwa hakika si wenzetu.

Kisa na mkasa - rekodi yetu haki, usawa na demokrasia kwetu ni mali ya watawala.

Kwa uonevu na uongo wa dola kama tunaouona kwenye kesi hii kwa hakika wanatuangusha sana kama nchi.
 
Hawataki kutumia ushahidi wa aina hiyo kwasababu wanajua wataumbuka, ndio maana kwenye lile pingamizi la mwanzo kabisa jaji aliyekuwepo aligoma kuchukua ushahidi wa majeraha aliyokuwa nayo mmoja kati ya watuhumiwa (sikumbuki vizuri alikuwa yupi kati ya Lijenje au Adamoo), akijua fika kwa kumpeleka hospitali akapimwe ingeonekana kweli alipigwa akiwa mikononi mwa polisi.

Kwanini Mawakili wa utetezi wasishinikize ushahidi huu kuletwa mahakamani?

Kwanini Mawakili wa utetezi wasishinikize kuwepo ushahidi wa daktari kuhusiana na hali za washitakiwa?

Kama mawili haya hayakubaliki kuna haja gani ya kuendelea na kesi hii?
 
Kwanini Mawakili wa utetezi wasishinikize ushahidi huu kuletwa mahakamani?

Kwanini Mawakili wa utetezi wasishinikize kuwepo ushahidi wa daktari kuhusiana na hali za washitakiwa?

Kama mawili haya hayakubaliki kuna haja gani ya kuendelea na kesi hii?
Kama ni mfustiliaji mzuri, wanahoji sana haya mambo
 
Hata kwenye mkutano wa njia ya video tumepigwa chini kama Rwanda, Zimbabwe, Mozambique, Burundi na Uganda.

Kenya, Malawi, Zambia na Afrika Kusini kwa hakika si wenzetu.

Lisa na mkasa - rekodi yetu haki, usawa na demokrasia kwetu ni mali ya watawala.

Kwa uonevu na uongo wa dola kama tunaouona kwenye kesi hii kwa hakika wanatuangusha sana kama nchi.
Yote kwa yote mimi nasema siku zote,wananchi ndio waoga sana nchi hii. Hii kesi imekaa vizuri sana kuwatoa ccm barabarani
 
Kama ni mfustiliaji mzuri, wanahoji sana haya mambo

Mkuu nimfutiliaji mzuri wa kesi hii.

"I am not in anyway belittling what they are doing in such very difficult circumstances."

Utetezi wasifunge ushahidi bila CCTV, mobile phones operators records na/au ripoti ya daktari.
 
Kwanini Mawakili wa utetezi wasishinikize ushahidi huu kuletwa mahakamani?

Kwanini Mawakili wa utetezi wasishinikize kuwepo ushahidi wa daktari kuhusiana na hali za washitakiwa?

Kama mawili haya hayakubaliki kuna haja gani ya kuendelea na kesi hii?
Amri ya jaji ndio inayowezesha haya kufanyika, tofauti na hapo itakuwa ngumu, jaji akiwa kama baba mwenye nyumba ndie mwenye maamuzi ya mwisho nini kifanyike ndani ya nyumba yake.

Mawakili wa utetezi hawawezi kulazimisha kuwapeleka watuhumiwa hospitalini kwa uchunguzi bila amri ya jaji kuamuru hivyo kwa askari magereza, watuhumiwa hawataruhusiwa kutolewa gerezani kwa ajili hiyo.
 
Yote kwa yote mimi nasema siku zote,wananchi ndio waoga sana nchi hii. Hii kesi imekaa vizuri sana kuwatoa ccm barabarani

Si sahihi kusema wananchi ni waoga.

Kwani wananchi ni nani?

Pana haja ya kuliangazia hili kikamilifu.

Wananchi hawawezi kutegemewa ku "rise spontaneously from nowhere" bila ya uwapo mikakati thabiti.

Uongozi una gharama zake kama yalivyo na marupurupu yake.

Tusipende marupurupu peke yake.
 
Amri ya jaji ndio inayowezesha haya kufanyika, tofauti na hapo itakuwa ngumu, jaji akiwa kama baba mwenye nyumba ndie mwenye maamuzi ya mwisho nini kifanyike ndani ya nyumba yake.

Mawakili wa utetezi hawawezi kulazimisha kuwapeleka watuhumiwa hospitalini kwa uchunguzi bila amri ya jaji kuamuru hivyo kwa askari magereza, watuhumiwa hawataruhusiwa kutolewa gerezani kwa ajili hiyo.

Kwanini mawakili wa utetezi wasiwasilishe maombi rasmi kuhusu haya 3 tumwone Jaji ataamua vipi?

Detention register (za kustukiza) za Moshi na Mbweni zilikuwa muhimu kwa kesi hii pia.
 
Leo kumekuwapo shahidi mahakamani kuonyesha Ling'wenya hakuwahi kufikishwa Tazara Polisi.

Shahidi huyu ana anayodai kuwa ni detention register kama ushahidi. Baadhi ya kurasa zake zimenyofolewa na nyingine zimeongezwa.

Si mageni kusikia polisi wamebambikizia watu kesi, wamewaweka watu rumande kwa majina bandia au hata bila kuwaandikisha kabisa.

Yamewakuta kina Mdude, kina Ulimboka na wengi wengine. Yumkini kina Ben, Lijenje au hata Azory ni hali hizo hizo.

Haki za watu haziwezi kuendelea kuchezewa hivi.

Kwa maana halisi ya haki, kwa nini ushahidi wa kisayansi uliopo usitumike kutenganisha mbivu na mbichi hizi?

Ushahidi wa ma CCTV lukuki yaliyoko sehemu mbalimbali na pia kutokea kwenye makampuni ya simu za mkononi upo.

Kwa vile ushahidi huu ni bora zaidi, haipo sababu ya kutokuuhitaji ili kutumika mahakamani.

Nyendo kamili za Kingai, Mahita, Jumanne, Goodluck na timu nzima tokea RAU hadi Mbweni ni muhimu kuhakikiwa zaidi ya maneno yao.

Mahakamani kusifanywe kuwa kichaka cha kupitishia uongo dhidi ya watu wengine.

Maneno ya mtu dhidi ya mwingine, kwa "litmus paper" ipi kuthibitisha mwongo ni nani?
Ila imefumbua fumbo la wasiojulikana ambao sasa tunawajua hata kwa majina
 
Hiyo kesi nimeacha kufatilia kila ukiangalia unaona ni vitu vya kutunga tuu hakuna shahidi akasimama akaongea kitu cha maana wote ni upuuzi mtupu ila Mh Jaji anakubaliana nao inaonekana wanajua hii kesi itaishia vip maana kama Mahakama ingekua inaheshimika wangefutilia mbali huo upuuzi ila naamini haya mambo ya kuharibiana maisha yataisha tuu hakuna kitu kibaya kinachodumu milele.
 
Hiyo kesi nimeacha kufatilia kila ukiangalia unaona ni vitu vya kutunga tuu hakuna shahidi akasimama akaongea kitu cha maana wote ni upuuzi mtupu ila Mh Jaji anakubaliana nao inaonekana wanajua hii kesi itaishia vip maana kama Mahakama ingekua inaheshimika wangefutilia mbali huo upuuzi ila naamini haya mambo ya kuharibiana maisha yataisha tuu hakuna kitu kibaya kinachodumu milele.

Ni nia yao tuache kufuatilia. Kumbuka mizengwe na maneno ya Sirro kuhusu kwenda mahakamani.
 
Leo kumekuwapo shahidi mahakamani kuonyesha Ling'wenya hakuwahi kufikishwa Tazara Polisi.

Shahidi huyu ana anayodai kuwa ni detention register kama ushahidi. Baadhi ya kurasa zake zimenyofolewa na nyingine zimeongezwa.

Si mageni kusikia polisi wamebambikizia watu kesi, wamewaweka watu rumande kwa majina bandia au hata bila kuwaandikisha kabisa.

Yamewakuta kina Mdude, kina Ulimboka na wengi wengine. Yumkini kina Ben, Lijenje au hata Azory ni hali hizo hizo. Ni hakika kwa maneno ya Sirro kuwa:

"Polisi hawa siyo malaika."

Haki za watu haziwezi kuendelea kuchezewa hivi.

Kwa maana halisi ya haki, kwa nini ushahidi wa kisayansi uliopo usitumike kutenganisha mbivu na mbichi hizi?

Ushahidi wa ma CCTV lukuki yaliyoko sehemu mbalimbali na pia kutokea kwenye makampuni ya simu za mkononi upo.

Kwa vile ushahidi huu ni bora zaidi, haipo sababu ya kutokuuhitaji ili kutumika mahakamani.

Nyendo kamili za Kingai, Mahita, Jumanne, Goodluck na timu nzima tokea RAU hadi Mbweni ni muhimu kuhakikiwa zaidi ya maneno yao.

Mahakamani kusifanywe kuwa kichaka cha kupitishia uongo dhidi ya watu wengine.

Maneno ya mtu dhidi ya mwingine, kwa "litmus paper" ipi kuthibitisha mwongo ni nani?
Hakika. Ingawa kwa mahakama iliyo huru, hadi hapo hii kesi imeonyesha ni ya kutengeneza na hata huu ushahidi wa kuungaunga umeshindwa ku "prove beyond reasonable doubts"

Ni kumpa taabu tu Judge kuweza kutoa uamuzi.
 
Hawataki kutumia ushahidi wa aina hiyo kwasababu wanajua wataumbuka, ndio maana kwenye lile pingamizi la mwanzo kabisa jaji aliyekuwepo aligoma kuchukua ushahidi wa majeraha aliyokuwa nayo mmoja kati ya watuhumiwa (sikumbuki vizuri alikuwa yupi kati ya Lijenje au Adamoo), akijua fika kwa kumpeleka hospitali akapimwe ingeonekana kweli alipigwa akiwa mikononi mwa polisi.
Labda una maana ya Ling'wenya na Adamoo. Huyo Lijenje hajawahi kupatikana.
 
Back
Top Bottom