Kesi ya Mbowe na wanasheria wa Tigo na Airtel ikumbushe wenye mamlaka kutunza siri za wateja ni muhimu kujenga sekta imara ya benki na mawasiliano

Makampuni mengi ya simu yana bahati ya kufanya kazi katika nchi zenye watu wengi wajinga ila ingekuwa kwenye nchi zilizoendelea leo tigo hisa zao zingeshuka tu kumbe kwao suala la privacy siyo kipaumbele chao kbsa kwa mteja wao shame on them

jiepusheni na uhalifu aisee.

kesho utaibiwa simu,halafu tutataka amri ya mahakama ili kukabidhi mwenendo wake kwa polisi.hapo ndio utajua nyeupe na nyeusi sio rangi.
 
Kuna mahali popote nimeandika wanyimwe taarifa wewe kichwa panzi?
Hao watu (mamlaka) wanaopewa taarifa ni kwa mujibu wa sheria zilizopo.
Kuna mamlaka hazinyimwi hizo taarifa
sheria zipo zinazi guide hivyo vitu
 
Yaweza kuwa uoga wa kubambikiwa Kodi, kubwa ili isiwe hivyo Bora kuungana na adui.
 
jiepusheni na uhalifu aisee.

kesho utaibiwa simu,halafu tutataka amri ya mahakama ili kukabidhi mwenendo wake kwa polisi.hapo ndio utajua nyeupe na nyeusi sio rangi.
Kwan kweny mwenendo wa hii kesi wewe umesikia kwamba shahidi alipata hyo order ya mahakama kutoa hizo taarifa ? Kama angefuata taratibu za kisheria zinavyotaka wala hakuna shida mkuu tusifanye kazi kwa mashinikizo bali kwa sheria na miongozi yetu
 
Ni kweli ndio wamesema hivyo au unasingizia mkuu.?
 
Sheria inasema taarifa inaweza kutolewa kama mtumiaji wa simu anatuhumiwa kutenda kosa fulani. Lakini uthibitisho uliotolewa leo ni kwamba polisi hawaelezi hata sababu, na tigo hata hawaulizi taarifa inahitajika kwa sababu gani.

Wakili Fred kaulizwa kama alitajiwa tuhuma za huyo mteja akasema hapana. Akaulizwa alivojibu alitaja tuhuma akasema hapana!
Muhimu alichosema ni kuwa kwao Tigo compliance (utii) ni muhimu kuliko Siri za mteja wao. Japokuwa alikuwa na uwezo wa kuhoji na kumtaka polisi mtaka taarifa kutumia vifungu vingine vya sheria hiyo hiyo..
 
wewe unalijua leo?

mie nilinunua simu ya wizi siku nakuja kudakwa jamaa walikuwa na karatasi kama 50 zilizojaa pages zenye mesages zangu zote,
 
Faragha ya mtu siyo uhalifu tu. Au kwako, hata serikali au kampuni wakisema hii ni confidential au classified information, basi ni ugaidi?
Bora umueleweshe anadhani confidential na classified info ni taarifa za ugaidi au ujambazi...

Kwa kuangalia fasta fasta majibu ya huyu staff wa Tigo kuna mambo hayapo sawa..

Ni kama ame impair bila kujua image ya mwajiri wake. Ukiangalia tigo wanatumia billions of money kujenga brand yao halafu jamaa anaichafua just like that..

Kuna namna ya kutoa responses ambazo zipo diplomatic, especially kwenye nyakati unapogusa maslahi ya muajiri wako.. nahisi amekurupuka

Aisee hawatamwacha, sioni huyu jamaa akiwa kwenye ajira yake mpaka December.
 
Sasa alshabaab wabataka kupoiga mabomu Vyombo vya Simu vifiche tu safi sana. Siri siri siri za nini kama hamtaki kufanya mambo mabaya!
 
Mpuuzi huyo yani mtu afanye uhalifu alaf atunziwe faragha
 
Yaani inanishangaza simple logic eti watu wanatoka mapovu. Tanzania kuendelea ni mwaka 1000
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…