Kesi ya Mbowe na Wenzake Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi yaahirishwa. Kuendelea Jumatatu ya tarehe 27/09/2021

Kama Mtanzania mwenye Moyo nimeumizwa sana na yale niliyoyasikia Mahakamani leo.

Kwa yanayoendelea kwenye kesi ya Mbowe na
wenzake itoshe tu kusema Wanzania tuwe makini sana na Polisi wetu.

1. Kuna kuwekewa madawa ya kulevya

2. Kupewa kesi ya UGAIDI

3. Kuchukuliwa pesa zako mfukoni.

4. Mateso ya KINYAMA.

5. Kushinda na NJAA hali ya kuwa mahabusu.

Polisi sio watu tena wa kulinda RAIA NA MALI ZAO BALI NI KUTESA RAIA NA KUCHUKUA MALI ZAO.

SIASA SIASANI...
 
lakini je kama amesemahayoili kujiokoa nakesi ? jaji ndiyo ataamua maana kila mtu hapo anataka kuponya roho yake polisi nao kama wakishindwa kesi tayari wana lakujibu maana itaonekana walifanya kweli usalama wao washindekesi wakishindwa ni ndani tu hapo sasa karata za kisheria zichezwe vizuri
 
Mungu ingilia Kati kwa kweli kwa ushahidi wa mtuhumiwa inaonyesha kuwa yote walioongea ni uongo tupu kuwa hawakuwapiga,pia kuwa walikuwa nao sehemu mbalimbali wakimtafta mtuhumiwa mwingine.mithali 14:34 haki huinua Taifa.
Hivi kwa akili za kawaida tu mwizi wa kuku tu ameiba na amekamatwa na kidhibiti anakataa sembuse komandoo!!!

Hao wasingeweza kukiri bila kibano cha msingi kinachotafutwa hapo walikuwa na nia ofu au laah mengine hapo ni blah blah tu
 
Kiko limezima tumbaku imeisha na uhondo unaendelea - mwenye tumbaku tafadhali anikopeshe niliwashe tena.


Yaani ni kwamba Afande huyo Jumanne anayetajwa walikuja naye mahakamani asubuhi, wakaingia chumba cha mawakili wa serikali, hatuelewi nini kimetokea wakamkataa asitoe ushahidi wake, wakampandisha dinga akasepa zake. Walipofika Mahakamani wakasema wanafunga ushahidi.
 
Hivi ndo kusema Magufuli na watu wake ni kweli kabisa alikuwa amedhamiria kumfanya kitu mbaya hasimu na mkosoaji wake Mkubwa Tundu Lissu?

Kama ni hivyo, basi huyu jamaa alikuwa power monger wa hatari kabisa. Ni vyema kuwa Mungu aliamua kuzuia mipango yake miovu kwa kumwondoa duniani...!!
 
Bongo upuuzi mwingi sana.
Yani upumbafu tu kila siku kesi na huyo bwege,either mfungeni au mumwache.
Kesi gani hii kila siku mpunga unapigwa hela zetu za kodi zinaenda.
 
hii kesi ni ya kisiasa, ni uhasama wa kumkomoa Mbowe na CDM kwa ujumla. CCM wana dhambi kubwa mno hawana utu kabisa.
 
Bongo upuuzi mwingi sana.
Yani upumbafu tu kila siku kesi na huyo bwege,either mfungeni au mumwache.
Kesi gani hii kila siku mpunga unapigwa hela zetu za kodi zinaenda.
ndo naisoma salary slip yangu hapa - PAYE wamelamba 30% - Hiyo NET yangu nikienda madukani nitakutana na VAT 18% - Bado TOZO zipo mgogoni mwangu - maisha gani haya wajemeni.
 
Polisi na vyeo vyenu na mnasema mna elimu ya chuo kikuu mnawafanyia binadamu wenzenu vitendo vya kinyama kisa kuwafurahisha watawala. Mungu na awalaani kama kweli mliyatenda hayo. Kwani kuwa polisi ndo ubinadamu ukutoke? Mbona mnadharirisha na familia zenu? Piga picha watoto wenu wanakuja kujua hayo matendo yenu ya kitalebani?
 
Jaji: Subiri kidogo, Shahidi ukiona kichwa kinapata moto unaeeza kuomba maji, naona unayo uongezwe maji

Shahidi: Ndiyo niongezewe mheshimiwa
 
Wakuu, nikili kuwa nmefuatilia kwa karibu Sana kesi ya m/kiti wa CHADEMA Mh. Freeman Mbowe na wenzake toka ianze mpaka Leo, kipindi chote hicho nlikua naelewa kilichokuwa kikiendelea na namna ambavyo safu zote ( yaani upande wa mashtaka na upande wa utetezi walivyotupa taswira ya mambo).

Lakini Leo, baada ya wakili msomi Peter Kibatala kumaliza kumhoji mshitakiwa Adamoo na Jaji kumpa uskani wakili wa serikali (mashtaka), kwa kweli nmetoka kapa, nadhan hata mshtakiwa mwenyewe alikua haelewi maswali ndo maana alikua anaomba yarudiwe, Jaji nae vivyo hivyo!

Kwa kuwa tunazidiana uwezo wa kufikiri, je , Wenzangu mmemuelewa wakili wa serikali alikua anauliza Nini?
Kama uliipata picha ya ndugu wakili, tujuzane hapa tafadhar!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…