Kesi ya Mbowe na wenzake, Serikali isitese watu bila sababu

Kesi ya Mbowe na wenzake, Serikali isitese watu bila sababu

Hamatan

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2020
Posts
3,197
Reaction score
7,677
Hatuingilii mwenendo wa Mahakama lakini kuna mambo yapo dhahiri ambayo, laiti kama Jaji angekuwa makini, Mawakili wa Serikali wasingekuwa wanaichezea Mahakama kama wanavyofanya.

Mathalani, leo mawakili wa Serikali wanasema eti shahidi hawezi kuendelea na kuhojiwa kwa sababu ameshauriwa na daktari kupumzika kwa siku mbili. Tuamini kuwa habari hii ya kutengenezwa ni ya kweli.

Halafu wanasema, hata kesho hawawezi kuleta shahidi mwingine kwa sababu wanaweza wasimpate. Mambo ya kujiuliza:

1) Kama shahidi asingeugua jana, huenda Kibatala angemaliza cross examination jana, na leo serikali ingetakiwa kuwa na shahidi mwingine. Kwa maelezo ya hawa mawakili wa serikali kuwa hawana shahidi ambaye yupo tayari kuja kesho kutoa ushahidi wake, ina maana hata kama Kibatala angemaliza cross examination jana, leo wasingeleta shahidi mwingine? Au walifahamu toka mwanzo kuwa shahidi angeugua jana?

2) Baada ya shahidi kuugua jana, na kisha kwenda hospitali, ilitegemewa leo angekuja mahakamani. Na kama angekuja mahakamani, basi Kibatala huenda angemaliza cross examination yake leo, na kesho serikali ingehitajika kuleta shahidi mwingine. Hawa mawakili wa serikali wanaosema hawana shahidi wa kumleta kesho ili kesi iendelee, ina maana hata kama Kibatala angemaliza cross examination leo, kesho wasingeweza kumleta shahidi mwingine?

Au walijua toka jana au juzi kuwa shahidi angeugua jana, leo angeambiwa na daktari apumzike kwa siku 2, na hivyo cross examination isingemalizika leo, na hivyo kutokuwepo umuhimu wa kuandaa shahidi mwingine?

Polisi na Mawakili wa Serikali wasiichezee mahakama na wasiwafanye watanzania wote ni wajinga. Wafahamu kuwa huku nje ya polisi na nje ya Serikali, kuna watu wana akili na weledi hata wa kuwazidi wao maradufu.
 
Ingekuwa jambo zuri kuundwa kwa tume huru kuchunguza mienendo ya task forces zilizokuwepo na kuchunguza watu kama kina Swila, Goodluck , Jumanne, Mahita pamoja na watu waliokuwa wakiwapa orders.
 
Wanapata tumbo la kuvuruga zaidi baada ya kufahamu kama mswaada was Kinga ya umbambikiaji na kesi michongo hautapita Ili kuwalinda na madhambi Yao. Hapa wameanza kuwaza huko tiendako itakuwaje, yasije kuwa ya saambovu na kondaboy🤔.
 
Wanapata tumbo la kuvuruga zaidi baada ya kufahamu kama mswaada was Kinga ya umbambikiaji na kesi michongo hautapita Ili kuwalinda na madhambi Yao. Hapa wameanza kuwaza huko tiendako itakuwaje, yasije kuwa ya saambovu na kondaboy🤔.
Kesi hii ikiisha Swila , Boaz na Kingai wanapaswa kushtakiwa kwa kutesa watu kwa undercover operation ya mchongo.
 
Nadhani Rais alikuwa mgeni walipomdanganya na kumtisha sasa ameshazoea na kujua ukweli muda ni mwalim mzuri na mkuu
Rais hakudanganywa kwa Sababu yeye ndiye aliamulu Mbowe akamatwe kisa na mkasa ni katiba mpya. Hangaya alidai wasubili asimamishe uchumi akina Mbowe wakakataa hivo Rais akaona kama vile kazalauliwa. Mama akaamua kutumia mamlaka kumdhibiti Mbowe.
 
Rais hakudanganywa kwa Sababu yeye ndiye aliamulu Mbowe akamatwe kisa na mkasa ni katiba mpya. Hangaya alidai wasubili asimamishe uchumi akina Mbowe wakakataa hivo Rais akaona kama vile kazalauliwa. Mama akaamua kutumia mamlaka kumdhibiti Mbowe.
Muda ni mwalimu mzuri ....
 
Rais hakudanganywa kwa Sababu yeye ndiye aliamulu Mbowe akamatwe kisa na mkasa ni katiba mpya. Hangaya alidai wasubili asimamishe uchumi akina Mbowe wakakataa hivo Rais akaona kama vile kazalauliwa. Mama akaamua kutumia mamlaka kumdhibiti Mbowe.
Huo Ndio ushetani.Kama ni Kweli ndio Maana hatuwezi kuendelea.Haki huinua Taifa.
 
1644555758548.png
 
Kiukweli kinacho watokea Jamhuri kwenye hii kesi, ni aibu tu na ambayo hawakuitarajia hata kidogo.

Na wafahamu fika Watanzania wengi tunaifuatilia hii kesi kwa umakini mkubwa, ili kujua mwisho wake.
 
Rais hakudanganywa kwa Sababu yeye ndiye aliamulu Mbowe akamatwe kisa na mkasa ni katiba mpya. Hangaya alidai wasubili asimamishe uchumi akina Mbowe wakakataa hivo Rais akaona kama vile kazalauliwa. Mama akaamua kutumia mamlaka kumdhibiti Mbowe.
Angeachwa Mbowe azunguke tu angechoka mwenyewe kuliko nguvu waliyoitumia inaharibu utalii nchini kuwa na ugaidi.
 
Ingekuwa jambo zuri kuundwa kwa tume huru kuchunguza mienendo ya task forces zilizokuwepo na kuchunguza watu kama kina Swila, Goodluck , Jumanne, Mahita pamoja na watu waliokuwa wakiwapa orders.
Kwa nchi zilizoendelea hii hufanyika.
 
Huyo wakili wenu mnamwita msomi ndio anarefusha kesi kwa maswali ya kipuuzi
.
Wakili:siku flani ulikula wali nyama
Shahidi:ndiyo
Wakili:na maji?
Shahidi:ndiyo
Wakili:yanaitwaje?
Shahidi sikumbuki
Wakili:ulipewa ndizi?
Shahidi hapana
Wakili:kwanini hukupewa?
Bla , blaah ,blaah blaa
Kesi imeahirishwa.
Lmao wtf.
 
Back
Top Bottom