Kesi ya Mbowe: Wapelelezi wanatakiwa kumsaidia Rais kuithibitishia dunia Mbowe ni Gaidi na sio kucheza na majaji wetu pekee itatuweka kubaya

Kesi ya Mbowe: Wapelelezi wanatakiwa kumsaidia Rais kuithibitishia dunia Mbowe ni Gaidi na sio kucheza na majaji wetu pekee itatuweka kubaya

Sirro na mama Samia watakua wanaona aibu sana kukurupuka kuizungumzia hii kesi na kusema ushahidi upo..
 
Kinachonifikirisha ni kwa nini mtuhumiwa wa kosa kubwa kama hili aliachwa huru wakati washirika wake wamekamatwa! Hivi hakujua kuwa washirika wake wamekwisha kamatwa na dili limebunguluka?

Kwa nini alikuwa anaenda nchi za nje na kurudi alijiamini nini? Au walikuwepo washirika wakubwa zaidi waliokuwa wanampa ujasiri na asichukue hatua yeyote kujilinda?

Kwa nini alipewa nafasi kwenye sherehe kule Mwanza kuongea mbele ya Rais? Ngoja nisubiri mashahidi wengine pengine nitapata jibu, la sivyo kwangu ni ngumu kumeza.
Ndugu yangu,
baada ya maofisa wazito Mahita na Kingai kuchemsha kisawasawa kuna dalili zote kuwa HUKO hakuna tena kitu cha ziada.
Hao ndio walikuwa tumaini lao kuu lililobakia, baada ya yule dhalimu wa Burigi kwenda zake.
Mie kwa sasa nasubiri kwa hamu kubwa futuhi la ushahidi wa Sirro ambae anatakiwa upande wa utetezi. AMEN
 
Vikao kila siku jinsi ya kujikwamua na hii aibu inayoipata jamhuri. Kiufupi waliobuni hawakujipanga, walitegemea mgongo wa jiwe kwa ubabe na ujeuri wake juu ya mhimili wa mahakama kuwafunga kina Mbowe.

Walitegemea kwa uwepo wa jiwe kesi ingeendeshwa kimya kimya (bila mahudhurio ya waandishi wa habari na namba ndogo ya wahudhuriaji esp ndugu) na nguvu kubwa kwenye media na matamko ya viongozi wa juu kuuaminisha umma juu ya ugaidi wa Mbowe na kufutwa kwa CHADEMA (Upinzani kufa rasmi TZ)

HAKIKA AKIWAZACHO BINADAMU SI MUNGU AKIWAZACHO. MUNGU ni fundi na hakika ana njia zake za kuitetea HAKI
AMEN, AMEN.
 
Polisi anayesemekana ndio aliye wapekua watuhumiwa na kuwakuta na bastola na kete ndio huyo huyo kafukuzwa kazi kwa kutaka kumbambikia mzee mmoja meno ya tembo.

Shahidi wa upekuzi ni mama muuza pombe ya mbege ambaye kila amuuziaye tangu asubuhi lazima aonje yeye Kwanza.
Vitu vingine vya kijinga sana
Mama Mbege ;Niliwaona wakiwa wamekaa ,wakinywa pombe na kusajili laini za simu.
Afande Mahita; Hawakuwa wamekaa walikuwa wanatembea kuelekea tuliko sisi.
 
Wacha niendelee kutafakari, bastola moja risasi tatu, washitakiwa wanne, hata wakigawana risasi hazitoshi, bastola sijui pia watazimana? Heri wangewakabidhi mapanga ili kila mmoja awe ana silaha. Sasa ugaidi unabidi utafsiriwe vizuri zaidi, kumhusisha mwanasiasha kwenye hii suala, mngelipanga vizuri zaidi, najua polisi kesi zipo kibao wanatafutwa tu watuhumiwa!
Halafu sh 600,000 ambazo hazitoshi kununua hata chain saw moja ya kuangushia hayo magogo.
 
Back
Top Bottom