Kesi ya uchochezi inayomkabili Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA) kunguruma leo

Kesi ya uchochezi inayomkabili Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA) kunguruma leo

R.B

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2012
Posts
6,296
Reaction score
2,575
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Arusha, leo inaanza kusikiliza kwa siku tatu mfululizo kesi ya uchochezi inayomkabili Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA).

Lema anadaiwa kutoa kauli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, alikwenda kwenye Chuo cha Uhasibu Arusha kama anakwenda kwenye sherehe za kuaga mtoto wa kike ‘sendoff'. Shauri hilo linalovuta hisia za wengi linasikilizwa na Hakimu Mkazi, Devotha Msofe, ambapo Juni 10, mwaka huu Wakili wa Serikali, Elianenyi Njiro, wakati akisoma maelezo ya awali alidai kuwa wanatarajia kuleta mashahidi tisa akiwamo Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), John Nanyaro na Mkuu wa Jeshi la Polisi wilayani Arusha (OCD), Gillis Mroto.

Mashahidi wengine ni maofisa wa Jeshi la Polisi akiwamo Mkaguzi Bernard Nyambanya na mwenzake aliyetajwa kwa jina moja la Jane, PC Godfrey, Joachim Mahanyu na wengine kutoka Chuo cha Uhasibu, Faraji Mnepe, Benjamin Simkanga na Naibu Hamidu.
Katika kesi hiyo, Lema akiwa eneo la Freedom Square ndani ya Chuo cha Uhasibu, anadaiwa kutoa maneno ya uchochezi yaliyosababisha uvunjifu wa amani.

Maneno hayo yanayodaiwa kutamkwa na Lema ni kinyume cha kifungu cha 390 sura ya 35 cha sheria ya kanuni ya adhabu marejeo ya mwaka 2002. "RC anakuja (Chuo cha Uhasibu), kama anaenda kwenye sendoff, hajui chuo kilipo wala mauaji ya mwanafunzi wa chuo hicho … (RC), ameshindwa hata kuwapa (wanafunzi) pole kwa kufiwa na amesema hawezi kuongea na wanafunzi wasio na nidhamu," alinukuu baadhi ya maneno yanayodaiwa kutamkwa na Lema siku ya tukio.

Wakili Njiro alidai mahakamani hapo kuwa kauli hizo zilipandisha hasira za wanafunzi ambao walianza kumrushia mawe na chupa Mkuu wa Mkoa, Mulongo alipokuwa akiwahutubia kuhusiana na tukio la kifo cha mwanafunzi, Henry Koga, kilichotokea Aprili 23,
 
Nikisikiaga jina la Magessa Mulongo hua nahisi hasira hasira hivi
 
Naomba kuuliza, tuliambiwa kwamba mashitaka ya uchochezi hayana dhamana, na ndio maana kina Sheikh Ponda hawana dhamana. Imekuaje Lema akaachiwa?
 
..Hivi, muuaji wa huyo mwanafunzi alishakamatwa?au..? Kama alishakamatwa, status ya kesi yake ikoje?
 
RC anakuja (Chuo cha Uhasibu), kama anaenda kwenye sendoff, hajui chuo kilipo wala mauaji ya mwanafunzi wa chuo hicho … (RC), ameshindwa hata kuwapa (wanafunzi) pole kwa kufiwa na amesema hawezi kuongea na wanafunzi wasio na nidhamu," alinukuu baadhi ya maneno yanayodaiwa kutamkwa na Lema siku ya tukio.

SASA HAPO NDIO KACHOCHEA NINI ? hawa wasaidizi wa mzee wa msoga shida sana
 
Mkuu wa Mkoa leo atakuja mahakamani huku anakata kiuno kama anaingia kwenye Send Off

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Sio kwenye sendoff, kwenye mchiriku ndo tunakataga viuno bwana. Hivi ile kesi ya mauaji ya mwanafunzi nayo imefikia wapi, au yunalinda kwanza heshima ya mkuu wa mkoa?
Mkuu wa Mkoa leo atakuja mahakamani huku anakata kiuno kama anaingia kwenye Send Off

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Maneno hayo yanayodaiwa kutamkwa na Lema ni kinyume cha kifungu cha 390 sura ya 35 cha sheria ya kanuni ya adhabu marejeo ya mwaka 2002. “RC anakuja (Chuo cha Uhasibu), kama anaenda kwenye sendoff, hajui chuo kilipo wala mauaji ya mwanafunzi wa chuo hicho … (RC), ameshindwa hata kuwapa (wanafunzi) pole kwa kufiwa na amesema hawezi kuongea na wanafunzi wasio na nidhamu,” alinukuu baadhi ya maneno yanayodaiwa kutamkwa na Lema siku ya tukio.

Jamani hivi sisi Watanzania hatuwezi kuwa SERIOUS hata na jambo ndogo!. Je mambo makubwa kama ya gasi, madini etc tutayaweza?!.

Hata kama ni kumtumikia KAFILI upate UJIRA wako, lakini ndiyo hata basi ukose BUSARA kidogo, uongozwe na TUMBO STREET.

With all due respect in a neutral position kweli maneno hayo hapo juu yana qualify kuwa maneno ya UCHOCHEZI?!!.

Au bado wanasheria waliofungua kesi hiyo wanaishi STONE AGE ambapo MFALME hata kama yuko UCHI haruhusiwi kuambiwa MFALME uko uchi. Bali atadanganywa kwamba MFALME nguo uliyovaa IMEKUPENDEZA!

Watanzania ni mabigwa wa kupoteza kwanza kodi na mda wa mahakama kwa kesi hizi zisizo na kichwa wala miguu!
 
Mkuu wa Mkoa leo atakuja mahakamani huku anakata kiuno kama anaingia kwenye Send Off

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

leo ataingia mahakamani huku anakata mauno kama anaenda kwenye unyago..
 
Hii serikali kweli sio sikivu,,,kuna kesi nyingi sana ambazo wananchi tunatakiwa kupewa report nakufanyiwa kazi,,kama ya huyo mwanafunzi aliyefariki,,lakini baadhi ya viongozi wanazifanya mahakama kuwa busy kwa vitu ambavyo sio vya msingi,,kiukweli unapoenda sehemu yenye msiba ,,vyeo vyako unaweka pembeni,,,sasa unaleta utemi kwenye majonzi,,
 
kweli ukickia serikali ya kikwete imechoka ndo hapa. hivi kumbe bdo lile lengo la kumdhibit bwana lema bado wanalo hawa magamba? wajiangalie maana wataambulia patupu.
 
Sio kwenye sendoff, kwenye mchiriku ndo tunakataga viuno bwana. Hivi ile kesi ya mauaji ya mwanafunzi nayo imefikia wapi, au yunalinda kwanza heshima ya mkuu wa mkoa?

wako busy kwanza na hii kesi wakimaluza ndiyo wataanza upelele wa aliyemuua kijana wa uhasibu..
 
hakuna jipya hapo kwani hizo kelele za kina mulongo zinakera masikioni petu... tufanye shughuli nyingine za maendeleo kwa ustawi wetu na jamii kwa ujumla.
 
SERIKALI YA CCM SASA IMEAMUA KUDILI NA LEMA NA KUACHA WAUAJI WANAENDELEA KULA BATA MTAANI CHA KUSHANGAZA NA HUENDA MSICHOKUFAHAMU NI KUWA.

BAADA YA MWANACHUO KUZIKWA KAKA WA MAREHEMU ALIFUNGA SAFARI KUTOKA IRINGA NA KUJA ARISHA KWAAJILI YA KUFATILIA KILICHOMTOKEA MDOGO WAKE,ALIKAA ARUSHA MIEZI MIWILI NA USHEHE LAKINI HAKUFANIKIWA NA HII NI BAADA YA POLISI KUMPIGA DANADANA KILA KUKICHA.

SASA BADALA YA KUTAFUTA WAUWAJI WA MWANACHUO WAO WAMEAMUA KUMSAKAMA MB,LEMA
NA CHAKUSHANGAZA ZAIDI KATIKA KESII HII HAKUNA MWANACHUO YOYOTE ATAKAE TOA USHAHIDI BALI WAMEJICHAGUA VIGOGO WA SERIKALI TU????????!.


Arusha. Mkuu wa Chuo cha Uhasibu cha Arusha, John Nanyaro na Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Arusha, Gillis Mroto, leo wanaanza kutoa ushahidi katika kesi ya tuhuma za uchochezi inayomkabili Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.


Mashahidi wengine katika kesi hiyo ni, Mkaguzi wa Polisi Bernard Nyambanyana na mwenzake aliyetajwa kwa jina moja la Jane.

Hali kadhalika PC Godfrey na Joachim Mahanyu . Wakili wa Serikali, Elinenya Njiro, alitaja mashahidi wengine watakaotoa ushahidi wao mahakamani kuwa Faraji Mnepe, Benjamin Simkanga na Naibu Hamidu, wote kutoka Chuo cha Uhasibu.

Lema anadaiwa kutoa maneno ya uchochezi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magessa Mulongo, alikwenda katika Chuo cha Uhasibu cha Arusha, mithili ya mtu aliyekwenda kwenye send-off na kwamba hajui chuo hicho kilipo wala mauaji ya mwanafunzi wa chuo hicho.

Wakili Njiro alidai kuwa mbunge huyo alitenda kosa hilo Aprili 24 mwaka huu, akiwa katika eneo la Freedom Square ndani ya Chuo cha Uhasibu na kwamba kitendo hicho kinapingana na kifungu cha 390 sura ya 35 ya sheria ya kanuni ya adhabu
 
SERIKALI YA CCM SASA IMEAMUA KIDILI NA LEMA NA KUACHA WAUAJI WANAENDELEA KULA BATA MTAANI CHA KUSHANGAZA NA HUENDA MSICHIKUFAHAMU NI KUWA.

BAADA YA MWANACHUO KUZIKWA KAKA WA MAREHEMU ALIFUNGA SAFARI KUTOKA IRINGA NA KUJA
ARISHA KWAAJILI YA KUFATILIA KILICHOMTOKEA MDOGOWAKE,ALIKAA ARUSHA MIEZI MIWILI NA USHEHE LAKINI HAKUFANIKIWA NA HII NI BAADA YA POLISI KUMPIGA DANADANA KILA KUKICHA.

SASA BADALA YA KUTAFUTA WAUWAJI WA MWANACHUO WAO WAMEAMUA KUMSAKAMA MB,LEMA
NA
CHAKUSHANGAZE ZAIDI KATIKA SEKI HII HAKUNA MWANACHUO YOYOTE ATAKAE TOA USHAHIDI BALI WAMAJICHAGUA VIGOGO WA SERIKALI TU????????!.


Arusha. Mkuu wa Chuo cha Uhasibu cha Arusha, John Nanyaro na Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Arusha, Gillis Mroto, leo wanaanza kutoa ushahidi katika kesi ya tuhuma za uchochezi inayomkabili Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.


Mashahidi wengine katika kesi hiyo ni, Mkaguzi wa Polisi Bernard Nyambanyana na mwenzake aliyetajwa kwa jina moja la Jane.

Hali kadhalika PC Godfrey na Joachim Mahanyu . Wakili wa Serikali, Elinenya Njiro, alitaja mashahidi wengine watakaotoa ushahidi wao mahakamani kuwa Faraji Mnepe, Benjamin Simkanga na Naibu Hamidu, wote kutoka Chuo cha Uhasibu.

Lema anadaiwa kutoa maneno ya uchochezi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magessa Mulongo, alikwenda katika Chuo cha Uhasibu cha Arusha, mithili ya mtu aliyekwenda kwenye send-off na kwamba hajui chuo hicho kilipo wala mauaji ya mwanafunzi wa chuo hicho.

Wakili Njiro alidai kuwa mbunge huyo alitenda kosa hilo Aprili 24 mwaka huu, akiwa katika eneo la Freedom Square ndani ya Chuo cha Uhasibu na kwamba kitendo hicho kinapingana na kifungu cha 390 sura ya 35 ya sheria ya kanuni ya adhabu

Mimi nimefanikiwa kuona hayo tu kwenye rangi nyekundu na nimechoka mwingine aendelee kusahihisha labda mada italeta maana.
 
Dont worry ,,mungu akiwa upande wako nani atakaetuweza.?
 
ndio vizuri wajiachague wasiohusika kutoa ushahidi ili hukumu iweze kuwa nzuri
hakutakua na balance of probabilities na case hiyo itaishia kuwa lema hana kesi ya kujibu..
hawataweza kuprove beyond reasoable doubt......ndivo wanavosema wanasheria
yaani kesi hii hitathibitika pasipo kuwa na mashakama,, ni ubabaishaji tu wa CCM
 
naomba kuuliza, tuliambiwa kwamba mashitaka ya uchochezi hayana dhamana, na ndio maana kina sheikh ponda hawana dhamana. Imekuaje lema akaachiwa?

dhamana iko wazi ktk kesi za uchochezi isipokua ponda wanamkomoa
 
Back
Top Bottom