Kesi ya Zumaridi yakwama kusikilizwa leo Oktoba 17, 2022 kisa maumivu ya mguu

Kesi ya Zumaridi yakwama kusikilizwa leo Oktoba 17, 2022 kisa maumivu ya mguu

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Kesi inayomkabili Diana Bundala maarufu kama mfalme Zumaridi na wafuasi wake imeshindwa kuendelea leo Oktoba 17, 2022 baada ya mtuhumiwa huyo kudai kuwa ana maumivu makali ya mguu na kuomba kesi hiyo ihairishwe ili apate matibabu.

Mfalme Zumaridi alitarajiwa kuanza kujitetea leo katika kesi inayomkabili yeye na wafuasi wake ya kuwazuia maafisa wa serikali kutekeleza majukumu yao pamoja na kuwajeruhi Askari Polisi.

Washtakiwa hao wanadaiwa kutenda makosa hayo, Februari 23 mwaka huu nyumbani kwa Zumaridi katika mtaa wa Buguku kata ya Buhongwa jijini Mwanza kinyume na kifungu namba 241, 243 (b) na 114 (a) na (b) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu.

Hakimu Ndyekobora amesema mahakama imewakuta washtakiwa na kesi ya kujibu baada ya upande wa Jamhuri kufunga ushahidi kwa mashahidi 12 na vielelezo 11.
 
Kinachofanyika hapo, ni kumsumbua tu mfalme wa watu, na pia kumpotezea muda wake. Ila kiukweli mfalme Zumaridi hana kesi yoyote ile ya kujibu.

Kama akina Mwamposa na Masanja Mkandamizaji wanaruhusiwa kupiga hela za wajinga, iweje nongwa kwa mfalme Zumaridi?

Huu ni uonevu wa wazi kabisa! Serikali iache hawa wajinga waliwe, ili akili ziwakae sawa.
 
Kinachofanyika hapo, ni kumsumbua tu mfalme wa watu, na pia kumpotezea muda wake. Ila kiukweli mfalme Zumaridi hana kesi yoyote ile ya kujibu.

Kama akina Mwamposa na Masanja Mkandamizaji wanaruhusiwa kupiga hela za wajinga, iweje nongwa kwa mfalme Zumaridi?

Huu ni uonevu wa wazi kabisa! Serikali iache hawa wajinga waliwe, ili akili ziwakae sawa.
Kosa lake aliitukana kamati ya amani ya mkoa wa Mwanza alafu mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo ni mchungaji alafu alikuwa General kule mabakamabaka alafu baadae akawa boss wa mkoa wale majamaa watulivu na wakimya huku ni koboko (elewa)
 
Kinachofanyika hapo, ni kumsumbua tu mfalme wa watu, na pia kumpotezea muda wake. Ila kiukweli mfalme Zumaridi hana kesi yoyote ile ya kujibu.

Kama akina Mwamposa na Masanja Mkandamizaji wanaruhusiwa kupiga hela za wajinga, iweje nongwa kwa mfalme Zumaridi?

Huu ni uonevu wa wazi kabisa! Serikali iache hawa wajinga waliwe, ili akili ziwakae sawa.
Kule kwenye mpira tutataniana mkuu Tate Mkuu ila kwenye imani nikiri kwamba ukatoliki umekufumba macho kiasi kwamba hata ukristo wenyewe, ulivyoanza na unavyoenea limekuwa fumbo kwako.

Huyo zumaridi ni dhahiri yupo nje ya neno la Mungu lakini hao wengine uliowataja sijawahi kuona ushahidi wowote kuonesha kwa vipi wapingwe.
 
Back
Top Bottom