Kesi ya ZZK ina makosa mengi

Kesi ya ZZK ina makosa mengi

Kawaulize waliokuwepo kwanza ndo uje upya.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
kama jk alivyoaibishwa na kagame alivyomwambia ana tabia za kujipendekeza kwa wazungu!

Huyo Kagame kaishiwa kama alivyoishiwa Slaa, achana nae ni mfa maji haishi kutapatapa, wakati yeye analalamika alikuwa anajuwa kinachoendelea Kongo, matokeo si unayajuwa?
 
Jana kamati kuu imesimamishwa kuongelea kumfukuza uanachama Zitto, leo uzi uleule mpaka Jumatatu. Mpaka sasa mshindi ni Zitto.

Huyo Tundu mpaka Rais kamponda kwa kubabia kwenye sheria tena mbele ya halaiki ya watu na mbele ya watazamaji wa TV mamilioni waliopo ndani na nje ya Tanzania wamejionea alivyopigwa madongo live. Na kimya, mpaka leo hajajibu, unajuwa kwanini? upigwe madongo na Mwenyekiti wa chama unachokipinga halafu ukae kimya? unajuwa kwanini?

Hivi Rais wa JMT kujibizana na raia wa kawaida mwenye cheo cha Ubunge kama alivyo Prof Maji Marefu inamaanisha nini? Rais kajishusha hadhi yake au mbunge huyo atakuwa tishio?

Na ile kauli ya Rais kuwa ni heri Slaa aingie ikulu kuliko Lissu aingie bungeni huoni kuwa rais wetu anakiri Lissu ni tishio zaidi kwa chama chake?
 
Pole sana Ndugu yangu Zitto Kabwe. Tamaa yako imekufikisha pabaya. Utakosa Ubunge, Posho, mshahara na tambo zako za kila siku. You are completely finished. CHADEMA hakikisheni anafukuzwa Chama na kunyang'anywa kadi.
 
Tatizo hujui sheria ndo maana unakimbilia kufungua thread mpya na kutumia maneno ya Mh. Tundu Lissu!!

Wewe mwenyewe umeandika kwa hisia bila kuwa na facts, halafu una washangaa waliofungua kesi!! Kweli Nyani haoni kundule.

Weka hizo facts wewe unayejua sheria kama unakumbuka maneneo ya wakili wa zitto ni kuwa anahofia unawanchama wake na anajua akiondolewa uwanachama hana maslahi tena si ya kibunge wala ya kamati ya bunge hicho ndicho anachopigania basi kwani mapenzi na CDM hana tena huyu kijana.
 
WW MPUUZI SANA IVI UMEONA HIYO KAULI YA MPUUZI MWENZIO KAGAME NI YAMAANA SANA NANI ALIE MUABISHA MWEZIE KATI YA JK NA KAGAME? NENDA RUANDA,UGANDA NA DRC CONGO UWASIKIE WANAVYOMZUNGUMZIA JK JINSI ALIVYO WATIA ADABU WANYARUANDA(kagame) KWA KUWATWANGA M23 NA KUWARUDISHA KWAO WANYARUANDA WAHAMIAJI HARAM
mpuuzi ni wewe mnahangaika na operasheni tokomeza majangili wakati hizo pembe za ndovu zinakamatiwa karibu na ikulu lakini kikwete wako yuko kimya! kwa nini asiwabinye hao wachina wake wakawarudisha tembo wetu? hata ukimtetea lakini majangili yana connection na ikulu!
 
Hivi Rais wa JMT kujibizana na raia wa kawaida mwenye cheo cha Ubunge kama alivyo Prof Maji Marefu inamaanisha nini? Rais kajishusha hadhi yake au mbunge huyo atakuwa tishio?

Na ile kauli ya Rais kuwa ni heri Slaa aingie ikulu kuliko Lissu aingie bungeni huoni kuwa rais wetu anakiri Lissu ni tishio zaidi kwa chama chake?

Kulikuwa kuna kujibizana pale. Mtu kapigwa dongo akabaki kujichekesha ulisikia kajibu mpaka leo? ana uwezo huo?
 
Sijasema CCM kuna demokrasia,ninachosea CHADEMA walitakiwa kuonyesha Demokrsia ya kweli.Ndo maana nasema hawana tofauti na CCM,tena nikaongenza bora hata CCM,CHADEMA ndo wanaharibu kabisa.Nyerere aliachia kura ziamue kati na Jakaya na Benjamin,ingawa Nyerere alimnadi Benjamin.Mtei yeye alichokifanya ni kumtoa kabisa Zitto kenye kugombea.

Demokrasia huanzia kufuata taratibu za chama husika. Kama mwanachama ana mawazo tofauti ni wajibu wake kuwashawishi wenzake wazibadilishe, akishindwa ni lazima azifuate taratibu ambazo wenzake walio wengi wanazitaka. Akiona hawezi ana hiari ya kwenda chama kingine chenye taratibu anazozitaka. Mnaodhani Zitto anapigania demokrasia, jiulizeni anafuata taratibu zipi? Na kila mwanachama akifanya kama Zitto itakuwaje? Hakuna demokrasia kama hakuna kanuni!
 
Jamaa hataki kabisa ku appear kwenye hearing kwa vile anajua atavuliwa nguo kama kale ka katuni niliwahi kukaona humu jamvini.
Akishindwa kwenye rufaa yake atasema kwenye hearing siji amueni mtakavyotaka maana jamaa mbishi balaa
 
Mkuu Mkwawa, wengi wameliongelea suala hili na nadhani wengi watakuwa wameshalielewa pia. Kwa jinsi ulivyoandika ni wazi umetumia lugha nyepesi na rahisi kiasi kwamba hata mtu mgumu kiasi gani kuelewa basi kwa uandishi wako ataelewa.
 
na wewe unaweweseka kama mwanamke aliyepewa talaka bila kutarajia! si wewe ndiye uliyekuwa unabwabwaja humu kuwa chadema hawawezi kumfukuza zitto? madrasa zinawaharibu akili, zitto kwa sasa ameisha: he is like a rotten potatoe! yeye si ni jembe lenu bana mwambie binamu yako mheshimiwa dr rais khalfani mrisho jakaya kikwete ampe uwaziri wa fedha si dr mgimwa kavuta box!

Madrasa inahusikaje hapa, kenge we
 
Sijasema CCM kuna demokrasia,ninachosea CHADEMA walitakiwa kuonyesha Demokrsia ya kweli.Ndo maana nasema hawana tofauti na CCM,tena nikaongenza bora hata CCM,CHADEMA ndo wanaharibu kabisa.Nyerere aliachia kura ziamue kati na Jakaya na Benjamin,ingawa Nyerere alimnadi Benjamin.Mtei yeye alichokifanya ni kumtoa kabisa Zitto kenye kugombea.
unongopa sana wewe Benjamin Mkapa aliokotw kwenye kapu hapakuwa

na demokrasia alitumia rungu lake
 
Weka hizo facts wewe unayejua sheria kama unakumbuka maneneo ya wakili wa zitto ni kuwa anahofia unawanchama wake na anajua akiondolewa uwanachama hana maslahi tena si ya kibunge wala ya kamati ya bunge hicho ndicho anachopigania basi kwani mapenzi na CDM hana tena huyu kijana.

Akili za Alinacha at work!
 
Hivi Zitto analalamika kujadiliwa asifukuzwe au analalamikia utaratibu na tuhuma dhidi yake kuwa si za kweli,mana nimeona majibu yake kwa katibu mkuu mwenyewe anaita utetezi huku ukipinga(defence underprotest),kwa madai yake ni kwamba tuhuma zote ambazo zimetokana na waraka ulioandaliwa na Dr.mkumbo na mwigamba,yeye anakana kuhusika na kwakuwa hatua zote za kinidhamu zimechukuliwaa kutokana na waraka huo yeye anaona anaonewa na ndio mana akaomba mahakama kuu kuzuia kamati kuu kujadili lolote juu yake hadi pale rufaa yake itakapokuwa imeamuliwa.
Na mahakama kuu imeizuia chadema kumjadili zito hadi maamuzi ya rufaa yatakapotolewa.
Binafsi nafikiri yuko sahihi,kwamba atashindwa au kushinda hili ni jambo jingine na kwa mwanasheria yeyote yule huwez kushangaa hili,kwa mfumo wetu wa sheria kwenye kila kesi lazima mmoja apoteze na mmoja ashinde.
 
Mchezaji wa simba sports club akihisi coacher hatampanga kwenye mechi anaweza kwenda mahakamani kuzuia mechi isichezwe kwasababu ya hisia kuwa hatapangwa na atapata loss kwa washabiki wake, na fedha ya mechi ya siku.

Jaji atasaidia wengi sana kwenye vyama vya siasa wana hisi vikao vikikaa hawawezi kutendewa haki. Itakuwaje kwenye kura za maoni ambapo kuna wengi huwa wanakatwa majina na vyama vyao, Je hukumu hii si italeta kasheshe kwenye utendaji wa kila siku wa vyama vya siasa, makampuni, na taasisi mbalimbali?

Kesi hii ni kesi ya kipuuzi kabisa kuwahi kufunguliwa kwenye uwanja wa sheria? Sioni ni jinsi gani Jaji wa mahakama kuu atatoa hukumu kwa hisia. Sheria ni pamoja na material evidence, huwezi kuwa na hisia ukashinda kesi.

Kesi hii hata kama ina mkono wa Ikulu labda jaji awe mwehu kabisa. Kweli unazuia kikao cha chama kisikae eti unahisi utafukuzwa chama? Unazuia usijadiliwa kwa hisia utanyang'anywa kadi? Ni vipi mahakama inazuia chama kisisimamie maadili na sheria, kanuni na kanuni zake. Je Ni lazima kuwa mwanachama wa chama fulani is it enforceable by law kuwepo kwenye siasa? Kweli hii ni sababu ya kwenda mahakamani? Kwanini usisubiri ufukuzwe ndio uende mahakamni.

Posho, mshahara, ajira ndio vinapiganiwa sasa. Wasiwasi wangu ni kuwa wakili wa ZZK amemwingiza ZZK choo cha kike bila ya zito kujijua. Ajira Hapa TZ ngumu, Zito katangaza dau kubwa wakili kasema twende mzigo. Ushauri wa kisheria haujazingatiwa zaidi ya panic na kukurupuka.

Naamini kesi hii itatupwa.

hivi mtu kutetea masilah yake ni kosa? Siasa ndo kazi yake na ndo inampa riziki kama alivyo mwalimu daktari au mwanasheria pale unapoona mtu anacheza na masilahi yako ni lazima uoneshe kustuka.tatizo watanzania wengi ni waoga mno na ndo mana, wengi haki zao hupotea na mwisho wa siku utasikia namwachia mungu. Ni kazi ya mahakama kutoa hukumu kama atashinda au atashindw ni kitu kingine
 
Back
Top Bottom