Wanasheria na serikali nisaidieni kujibu hii hoja.
1. Ni kwa nini kesi zinazohusu mambo ya siasa zinaharakishwa kusikilizwa na kutolewa hukumu ndani ya kipindi kifupi. Mfano wa kesi za uchaguzi zimesikilizwa kwa muda mfupi na sasa ni karibu zote zimeisha. Pia kesi zinazohusu uchochezi wa mambo ya kisiasa nazo pia hufanyiwa upelelezi haraka na kusikilizwa haraka na hukumu kutolewa ndani muda mfupi. Ila inasikitisha kuona kuwa kesi ambazo za jinai ambazo sio za kisiasa, upelelezi wake unachukua muda mrefu sana na hata upelelezi ukishakamilika usikilizwaji wake unachukua muda mrefu sana. Hata kama mashahidi wote wapo lakini waendesha mashtaka wanaleta shaidi mmoja kila mwezi na wakati mwingine hawafiki mahakamani kwa sababu zisizo za msingi.
2. Kesi nyingi za watumishi wanapokuwa wameshtakiwa na serikali au mwajiri mahakamani zinachukua muda mrefu sana kufanyiwa upepelezi. Na pia pale ambapo upelelezi wa kesi umeshakamilika waendesha mashtaka wa serikali hawafanyi haraka kukamilisha usikilizwaji wa kesi husika jambo ambalo linawagharimu sana watumishi husika na pia serikali yenyewe.
1. Ni kwa nini kesi zinazohusu mambo ya siasa zinaharakishwa kusikilizwa na kutolewa hukumu ndani ya kipindi kifupi. Mfano wa kesi za uchaguzi zimesikilizwa kwa muda mfupi na sasa ni karibu zote zimeisha. Pia kesi zinazohusu uchochezi wa mambo ya kisiasa nazo pia hufanyiwa upelelezi haraka na kusikilizwa haraka na hukumu kutolewa ndani muda mfupi. Ila inasikitisha kuona kuwa kesi ambazo za jinai ambazo sio za kisiasa, upelelezi wake unachukua muda mrefu sana na hata upelelezi ukishakamilika usikilizwaji wake unachukua muda mrefu sana. Hata kama mashahidi wote wapo lakini waendesha mashtaka wanaleta shaidi mmoja kila mwezi na wakati mwingine hawafiki mahakamani kwa sababu zisizo za msingi.
2. Kesi nyingi za watumishi wanapokuwa wameshtakiwa na serikali au mwajiri mahakamani zinachukua muda mrefu sana kufanyiwa upepelezi. Na pia pale ambapo upelelezi wa kesi umeshakamilika waendesha mashtaka wa serikali hawafanyi haraka kukamilisha usikilizwaji wa kesi husika jambo ambalo linawagharimu sana watumishi husika na pia serikali yenyewe.