Kevin De Bruyne: Mpishi wa mabao ya Man City EPL asiyeimbwa

Kevin De Bruyne: Mpishi wa mabao ya Man City EPL asiyeimbwa

De Bruyne jamaa fundi sana.. Huwa sichoki kumtazama na kumfuatilia..

Ananifurahishaga huyu fundi wa kiBelgiji jinsi anavyokuwaga mwekundu baada ya mechi!!!
 
Bila shaka huyu ni kiungo mchezeshaji bora kwasasa katika EPL, huyu jamaa ndio injini ya Man City katika mabao.

Mpaka leo nashangaa ni kwanini Chelsea walikubali kumuuza kirahisi.

Kevin De Bruyne (KDB) anajua kupiga pasi za mwisho zenye macho kwenda kwa akina Aguero na Gabriel Jesus ambao kazi yao ya kupachika mabao inakuwa rahisi. Pia anajua sana kuanzisha mashambulizi ya hatari kwenda kwenye lango la adui.

KDB ndio injini ya mashambulizi katika kikosi cha Pep Guardiola kama ilivyokuwa kwa Xavi wakati Pep akiwa Barcelona. Kwasasa kama utacheza na Man City basi mtu wa kwanza kumchunga ni KDB vinginevyo utajitafutia matatizo .

Tuache unazi, tuache ushabiki ni wakati sasa wa kutambua mchango wa KDB kama mmoja ya viungo bora EPL kama si Ulaya nzima.
Yeah huyu kijana anasakata kabumbu kinoma.
Afu hata hazungumziwi kivile kama kina Labile n.k
 
huyu alikuwa mchezaji bora wa mwaka pale ujerumani baada ya kutokea pale darajani mimi nafurahi sana huyu mchezaji akipangwa namba 10 ni hatari lakini pep anampanga katikati duu naumia sana anavitu vya kutisha halafu anakitu cha ziada yaani miguu yote ni balaaa
 
Sawa, sisi washabiki tunaumia MNO alivyotua darajani, LKN mbona msimu uliopita hazard alifunika vibaya
 
huyu alikuwa mchezaji bora wa mwaka pale ujerumani baada ya kutokea pale darajani mimi nafurahi sana huyu mchezaji akipangwa namba 10 ni hatari lakini pep anampanga katikati duu naumia sana anavitu vya kutisha halafu anakitu cha ziada yaani miguu yote ni balaaa
Umemaliza kila kitu mkuu
 
Back
Top Bottom