Kha! Mara Kuna Wanyonge?

Kha! Mara Kuna Wanyonge?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Duh sijui ni ugeugeu au ni ufyatu... hazikupita siku nyingi watu walisema lugha ya "wanyonge" haipo. Na kuwa ni lugha mbaya... mara hii watu wameanza kusema kuna wanyonge? kha!! Watu walikuwa wanatakiwa kuwa wazalendo na waoneshe uzalendo; sasa wanalipishwa kodi ya "uzalendo" wanang'aka! uzalendo kumbe mchungu.

Sijui kwanini isiwe kodi ya "kuwa Mtanzania"? Binafsi sijaielewa na sijataka hata kuchukua muda kuielewa... kama uzalendo unaweza kuundiwa kodi kwanini tusije na kodi ya wanaozungumza sana.. halafu ianzie Bungeni... Halafu iwepo kodi ya watu wanaosema "serikali imepanga" kila anayesema hivi analipa kodi. Au kodi ya watu wanaosema "Serikali imedhamiria kujipanga"... au "Serikali iko mbioni kuanzisha mchakato".

Labda tuwe na vikodi vingine vingine vidogo vidogo maana hatujui kama kila anayelipa mihamala hii kweli ni mzalendo na si fisadi... AAh! labda tuwe na kodi ya wasio mafisadi (hili neno sitashangaa litaanza kurudi tena). Mafisadi.

Mafisadi Wazalendo? Well!! halafu tunawalima kodi... Ila labda liwekwe punguzo la "wanyonge" kama hawa watu bado wapo Tanzania.
 
Tatizo watanzania wengi sio wazalendo, hii kodi itahamasisha uzalendo !
 
Ha ha wengi wao midomo imepinga kwa kukosa msimamo
Duh... sijui ni ugeugeu au ni ufyatu... hazikupita siku nyingi watu walisema lugha ya "wanyonge" haipo. Na kuwa ni lugha mbaya... mara hii watu wameanza kusema kuna wanyonge? kha!! Watu walikuwa wanatakiwa kuwa wazalendo na waoneshe uzalendo; sasa wanalipishwa kodi ya "uzalendo" wanang'aka! uzalendo kumbe mchungu...

Sijui kwanini isiwe kodi ya "kuwa Mtanzania"? Binafsi sijaielewa na sijataka hata kuchukua muda kuielewa... kama uzalendo unaweza kuundiwa kodi kwanini tusije na kodi ya wanaozungumza sana.. halafu ianzie Bungeni... Halafu iwepo kodi ya watu wanaosema "serikali imepanga" kila anayesema hivi analipa kodi. Au kodi ya watu wanaosema "Serikali imedhamiria kujipanga"... au "Serikali iko mbioni kuanzisha mchakato"...

Labda tuwe na vikodi vingine vingine vidogo vidogo maana hatujui kama kila anayelipa mihamala hii kweli ni mzalendo na si fisadi... AAh! labda tuwe na kodi ya wasio mafisadi (hili neno sitashangaa litaanza kurudi tena). Mafisadi...

Mafisadi Wazalendo? Well... halafu tunawalima kodi... Ila labda liwekwe punguzo la "wanyonge" kama hawa watu bado wapo Tanzania...
 
Hata nchi zilizoendelea zimekuwa hivyo kwa kuwa wananchi wake wamejibana na kukubali kutozwa matozo mbalimbali ili ziendelee.

Tukifikia pazuri kimaendeleo tutaona matunda ya tozo hizi.

Mamaaa,pigilia humo humoooooooooooooooo
 
Duh... sijui ni ugeugeu au ni ufyatu... hazikupita siku nyingi watu walisema lugha ya "wanyonge" haipo. Na kuwa ni lugha mbaya... mara hii watu wameanza kusema kuna wanyonge? kha!! Watu walikuwa wanatakiwa kuwa wazalendo na waoneshe uzalendo; sasa wanalipishwa kodi ya "uzalendo" wanang'aka! uzalendo kumbe mchungu...

Sijui kwanini isiwe kodi ya "kuwa Mtanzania"? Binafsi sijaielewa na sijataka hata kuchukua muda kuielewa... kama uzalendo unaweza kuundiwa kodi kwanini tusije na kodi ya wanaozungumza sana.. halafu ianzie Bungeni... Halafu iwepo kodi ya watu wanaosema "serikali imepanga" kila anayesema hivi analipa kodi. Au kodi ya watu wanaosema "Serikali imedhamiria kujipanga"... au "Serikali iko mbioni kuanzisha mchakato"...

Labda tuwe na vikodi vingine vingine vidogo vidogo maana hatujui kama kila anayelipa mihamala hii kweli ni mzalendo na si fisadi... AAh! labda tuwe na kodi ya wasio mafisadi (hili neno sitashangaa litaanza kurudi tena). Mafisadi...

Mafisadi Wazalendo? Well... halafu tunawalima kodi... Ila labda liwekwe punguzo la "wanyonge" kama hawa watu bado wapo Tanzania...
Haya ni matapeli ya nchi hayana lolote
 
Kweli,mfano
Tatizo watanzania wengi sio wazalendo, hii kodi itahamasisha uzalendo !
Mimi hapa sijawahi kuwa mzalendo hata siku moja, cha ajabu wananikata hiyo kodi ya uzalendo! Huu ni uonevu kabisa
 
Siku Watanzania watapovua koti la mambo ya siasa na kuangalia vitu kwa akili zao wenyewe, mambo yatabadilika overnight.

Tuendelee kunywa mtori, nyama ziko chini.
 
Back
Top Bottom