Khaa! ..Hebu na Tujitambue...

Ndio maana wanasema ndoa zinazodumu ni za wale wanandoa ambao naweza kuwaita wako interwoven, kiasi kwanza hakuna changudoa wa aina yoyote hata kama anajua kukata kiuno kama feni anayeweza kuwatenganisha. Maana kinachowaunganisha ni more than sex. Sijuhi umenipata.

Hivi hujiulizi kwa nini kuna watu ni chita lakini uwambii kitu kuhusu wake zao?
 

......mwanajamiiOne, .....jana nilipokupa pole Dark City aliniuliza pole inatosha nini katika haya.

.......aliyelazwa kitandani mwangu na aliyekuwa mke wangu alikuwa rafiki yangu. Hakuishia kulala tu, na mimba akampa,....japo mungu si athumani ikaishia kutunga nje ya kizazi (ectopic)

.....mpaka hivi leo, sina kinyongo na huyo jamaa. He was invited na kupewa heshima ajilie atakavyo. Hata ex- wangu nimeishia kumsamehe tu. Kupoteza uwezo wa kuzaa tena si adhabu ndogo kwa mw'mke.

......sijui ningewakuta ningefanyaje, but me being me naamini ningewaacha hapo nikalale hotel. Wakulaumiwa ni mke/mume, ....nilimuamini, hakujiaminisha.

Nimekujibu?
 

Dah...................I am so sorry Soulmate! umenijibu na ninaomba niishie hapa! Sina swali la nyongeza mydia.
 
Asprin you have nerves. But mind your senteces someone may fail to understand you............lol hii ya kwako kiboko. Are you real serious saying ukinyimwa utabaka mitetea na mbuzi???????????????
 
Last edited by a moderator:
Mbu you are gentleman enough, to me this is unexplainable,...............................
but kwakua umeshasamehe how do you find kurudiana na ex wako ili atleast kumsaidia kupoteza mawazo?????????????
God was good kukufanya uwe mbali but huyu mwanaume mwenye ndevu za juu na chini anayekipanda cha mwenzie ana utimamu wa mwili na akili kweli?

anyway najifunza mengi sana ktk haya maisha this is a lesson to treasure
 
Last edited by a moderator:
Mbu MwanajamiiOne leo nimekwenda kuskiliza shauri lile nililoleta uzi hapa kuomba ushauri juu ya kijana anawake wawili na wake zake wote wanacheat.

Kimsingi nilichokitoa kama ushauri ni kwamba kwakua bwana alikuwa innocent sana na hajawah kuhisiwa au kushikwa akicheat kama wakeze mm nilishauri kwamba awaache wote kwa talaka 2, sikutaka 3 manake wakitoka wataolewa tena so tupanish them awaache kwa mbili na kwasababu yy ni mwanaume anaweza kuoa tena mwanamke mwingine wa kumliwaza ila hawa wawili wabaki kwa wazazi wao bila idhini ya kuolewa.

ndipo nilipogundua kuwa sheria ya talaka kwa imani ya kiislamu siyo adhabu kama zitakuwa talaka 3 but kama ni mbili hii ni adhabu ya maisha. Nilivaa sura ya kazi pasi kuwaonea wanawake wenzangu huruma kwani kumleta mwanaume na ndevu zake kwenye nyumba ya mwanaume mwingine ni kitu kibaya sana.

na hapa hata kwa mwanaume kumleta mwanamke malaya kwenye kitanda cha mkeo halali ni dhambi mbaya sana. hii laana lazima itawamaliza tu. the best solution ni kudevorce ili kupisha wao waendelee. Asprin unaposema kucheat ni kucheat tu iwe ghouse, kwenye uchochoro kwenye gari home kwako mm nakupinga sana juu ya hili. Na sijui kwanin siku hizi imekuwa ni fasheni kwamba % kubwa kila ke au me mwenye ndoa azini. hivi ni nyege tu au kuna cha ziada?

Kweli wana jf Mungu kaikataa zinaa, tujiepushe nayo na hii no matter utafanya kwa mbwembwe gani leo iko kama njaa tu hamu haitaisha na baada ya siku mbili utataka tena. sasa hivi kuvua nguo kwa kila mwanamke au kwa kila mwanaume kwanza aibu tu jamani hatuoni? pili hatumwogopi Mungu? achilia magonjwa ambayo tutasema inzi kufia kwenye kidonda ni halali yake. lol............... natamani sana K zote zitiwe kufuli pa baki pa kutolea mkojo tu. binafsi huu uchafu si upendi kabisa na ee mungu nisaidie niish tu kama mshamba kuliko kufanya kazi ya kuhesabu govi za watu.
 
Last edited by a moderator:
gfsonwin bana .....................K tu ndo zitiwe kufuli na M je?? mwisho zitaendachimbua fukufuku wale wadudu wa mchangani ati..........

Hongera kwa kuwakilisha kwenye kesi. Sometimes naichukulia kama anguko la ma-padri na kutokuoa vile
 

.....hah? ....kosa la ngapi laachisha mke, au kosa kubwa vipi laachisha mke?.....

Hilo lilikuwa kosa lake la kwanza, nikampa 2nd chance akaharibu kwa kosa jingine, 3rd chance pia, 4th chance, 5th chance, 6th chance....the 7th was the last.

She was my 'angel'....she deserved my forgiveness....lakini hakujali thamani ya penzi langu kwake. What is lost is lost forever. No regrets.
 
Last edited by a moderator:
Nyumba kubwa,kwanini ubembeleze kuishi na mwanaume cheater?Ana nini cha maana?Kama kuna wanaume wengi wasiocheat yanini ukae na cheater?Huna sababu ya kuomba asichukuliwe jumla wakati wapo ambao hawatachukuliwa kamwe.Ukisafiri hata 3 years unarudi unakuta coni yako haijalambwa na yoyote,unajilia mwenyewe kwa raha zako.Wanaume wa aina hii ni wengi pia.Huyo wa kuchukuliwa kwa muda na aende jumla!
 
Pamoja na kuwa kinachoniweka kwenye ndoa ni pendo; bado sikubaliani na wewe kuwa watu wawe wanaachika na kuolewa kila mara; maana hao waaminifu wana lebo usoni??? Afu imagine huko niendako kwa second sijuhi forth husband nabebana na wanangu au? Mi nkiaamua kuachika wala sitatafuta huyo faithful. Ndoa itakuwa basi tena kwangu. Nta focus kwenye kulea wanagu kuliko kutafuta wa kunipenda tena.


 
Ndio maana nilikuuliza Eiyer umeoa? Na mimi nilikuwa na msimamo zaidi ya wa kwako. Ingekuwa enzi zangu tungesaidiana hapa kujenga hoja za hakuna kuvumilia chita. Kua uyaone. Ukishaoa na kukaa na mkeo miaka kumi; rudia mawazo ulonayo sasa ndio utajua nina maanisha nini.
 
Mbu, nakugongea likes 400 napenda mwanaume, kama wewe. kwamba at cost utalinda na kutetea penzi lako but if things are not coming unaachia ngazi
 
Last edited by a moderator:

......NK, .....mimi nimejiamulia kama nitaoa tena, basi atayenifaa ni ex-victim mwenzangu, ....ambaye nae keshaburuzwa vya kutosha bila kuthaminiwa huko alikotoka.

....iwapo sie wawili, tuliojaa makovu tukiamua kuishi pamoja, kuna chances pia za kuumizana japo sio kwa kiwango "kikubwa" (note the "-")...au wewe waonaje?

Maumivu ya Mapenzi siyataki tena Mbu mie. Hivi, ni kwanini Mapenzi yanauma?
 
Mbu, nakugongea likes 400 napenda mwanaume, kama wewe. kwamba at cost utalinda na kutetea penzi lako but if things are not coming unaachia ngazi

......thx bana, ....kupenda ukapendwa, kumthamini ukathaminiwa, kumuamini ukaaminiwa,....ndio "Vow" kubwa inayotusumbua kwa kutotekelezeka kwenye kizazi hiki.

Huu mkasa wa mwanajamiiOne na maamuzi ya wengi ni taswira tosha jinsi penzi linavyothaminiwa au kutothaminiwa.
 
Last edited by a moderator:

jaman unajua tukisema sijui tukatae au sijui tunahararisha! tunajidanganya tu! CHEATING ipo na ina exist kwa kiwango kikubwa mnoo..........! wa kulaumiwa ni wanawake na wanaume! sio tu huyo small house hata ww mume wa mtu una tatizo! kwa kuwa ipo na kuipinga hapa JF ni maigizo kwa kweli ndio maana unadeal na rate ya kucheat kuna waliopitilizaa yan hawajarii kbs hisia za wake na familia zao, anaonyesha hadharan hii dharau ndio mbaya mara mia! ukweli unauma bora mtu asikuonyeshe (anafanya mambo yake behind the scene ka ww babu teh........ kidin lolz)...... kuliko kukurupuka dharau nje nje hadi unamleta chumban kwako mmmh...... io too much aisee!
 
Nyumba kubwa,u may be right lakini ni kwa mtazamo wako sana.Unajua yapo mambo ambayo hata tufanye nini yapo kama yalivyo.Ninachokataa mimi ni kuvumilia ila kusamehe nakubali.Kuvumilia kuna maana kama unavyosema wewe kuwa ame cheater lakini asiende jumla,hili nalikataa.Nakataa kwa sababu nikikaa na mke wa mtindo huu nitakua nimeudhalilisha ubinadamu wangu.Binadamu maana yake ni kufikiri na kutenda kama binadamu.Kufanya ngono hovyo hovyo na bila hata kujali unafanya na nani hiyo ni tabia na matendo ya mbuzi,kuku na ng'ombe.Kusamehe maana yake ni kufanya kosa kwa bahati mbaya na kuomba msamaha na kuondshwa kukerwa na kitendo hicho,huyu nitamsamehe na ndoa itaendelea!
 

Kama hujui ni kwamba mwanaume faithfull hahitajiki awe na lebo usoni,utamvuta kama wewe ni faithfull kama yeye kwa kufikiri au kutenda.Hivyo mumeo ni zao la fikra au matendo yako.Kagua sana maeneo hayo utampata cheater au kinyume chake!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…