Dj BAK
Naomba kudedicate wimbo uitwao 'Joleen' by Dolly Parton to MwanajamiiOne. Nafikiri ndicho anachowasihi wadada wote wanaochukua waume za watu!
Joleen x3
I am begging you please don't take my man.
... You can have a choice of men, but l could never love again, he is the only one for me Joleen....
Ngugu yangu gfsonwin,
Hapo umeongea kinadharia sana....Kiuhalisia, si mwanamke wala mwanamume anayeweza kuleta ukombozi wake bila kumtegemea mwenzake...Kudhani kwamba wanawake wanaweza kujikomboana peke yao ni jambo ambalo siamini kabisa kama linawezekana.
Itabidi nitawatafute wataalamu wenye shule zao wanielimishe!!
Hiyo sasa ndiyo hali halisi...Kudhani kinyume chake ni wishful thinking!
Babu DC!!
Duuuuhhhhh,
Kaka hapa naona umeamua kuhamisha magoli......Cheating haivumiliki ndiyo, ila wewe huoni tofauti kati ya kwenda kujificha kichakani (enzi zetu) na kufanyia lounge (bed room)???
Babu DC!!
umewahi sikia 'i f.u.c.k.e.d her,but i only make love to you'?????
Unasema?
Nasikitika sana lawa za baadhi ya wachangiaji zinaenda kwa wanaume pekee... sikitiko!!!
Tendo si sahihi, kufnyia ndani ndio balaa, lakini je utalaumu upande mmoja?? nini maana ya kuchagua wa kulaumu?? tafsiri yake ni ipi kwa nafasi ya mwanamke to right the wrongs that men make if we eventually end up in blaming one party in such a crime??
Taratibu za jamii na hata sheria ziko wazi, kusaidia uhalifu ni uhalifu pia, lakini nadhani in our lives women have been on the loose when it comes to accountability..........
BINAFSI NTALAUMU WOTE, EQUALLY, KIBAYA ZAIDI NI PALE BINTI UNALALA KWA BWANA WA MWENZAKO TENA KITANDANI KWAO HALAFU KESHO UNAMSALIMIA NA MACHO MAKAVU NA KUMPA HUG, YET UNALAUMU MWANAUME
Kamanda, tupo pamoja.
Halafu kama twataka hukumu kiukweli kesi hii, tu assume upande wa mwanaume nae alifikiaje uamuzi huo.
Huenda (mwanaume) nae alijionea enough is enough, potelea mbali....psychological abused na the so-called mama mwenye nyumba yake ambaye mwanajamiiOne amejipa nafasi ya kumtimua mume kwa maneno ya "chukua virago vyako kwenda!"
Assume, huyo mume kwakuwa anaishi kwa mkewe, huyo mwanajamiiOne anamkosea adabu, heshima, utii na haki zake. Assume, mke anarudi time anayotaka, mlevi, mzinzi, mwenye madharau nk....
What pushed that man to that 'extent?'
ila hao wame za watu siku izz jaman ...... mh huruma bure,
kwa haraka haraka naona walioolewa wana kazi haswaaa......
hahahahah@obsesd
kweli FL.... utasema wana pepo vile level ya matamanio yao si ya kawaida lol!
.....😱 .....mtoto wa kike hebu punguza presha bana, kunywa funda mbili tatu za maji baridi kisha uyarudie kinyume nyume uloyatamka (yaandika)....
Wajikubalisha na matokeo kiurahisi namna hiyo? Pole....halafu mbona wamtimua na mabegi yake? Ingekuwa ni nyumba yake ungeondoka? .....Soulmate, hasira hasara....mdomo huumba. Kaeni chini myazungumze, labda 'akili si zake'
eti wanasema ndivyp walivyoumbwa ....sijui sisi tumeumbwaje?:ranger:
Duuuuhhhhh,
Kaka hapa naona umeamua kuhamisha magoli......Cheating haivumiliki ndiyo, ila wewe huoni tofauti kati ya kwenda kujificha kichakani (enzi zetu) na kufanyia lounge (bed room)???
Babu DC!!
Ndugu yangu Dark City, nakubaliana na wewe ila kuna kitu napenda nikukumbushe. Hivi unajua umoja ni nguvu? kama ndiyo inamaana once women decide to be together definately huyu mwanamume hata pata nafasi ya kuingilia kati.
labda niseme to me sitak hata kuju huyu mume wangu anacheat wapi na nani, na mimi siyo kwamba sitongozwi la, tena muda mwingine na watu ambao wanauwezo na ambao they can take me anywhere, but mimi msimamo wangu unabaki kuwa kwanini nimuumize mwanamke mwenzangu?
je mwanaume huyu nitatembea naye mara ngapi, ili nipate nini na kwa wakati gani? You know ukikaa na kufikiri utagundua kuwa hata kama huna hela au kazi au chochote kile kutembea na mume wa mtu hakutamaliza kiu ya tatizo lako hata kidogo na siku ukiwa na shida ambayo hataweza kukutimizia basi utatafuta mwingine awezaye kufanya hivyo. Hapo hivyo utajiuliza tena nitatembea na wanaume wangapi, kwa muda gani, ili nipate nini?
Pia kuna kitu ambacho mimi huwa nakisema sana, yakwamba, simuonei huruma mtu anayecheat kwasababu ta tabia kama wafanyavyo wanaume walio wengi. Hawa kwao ni tabia na kama tujuavyo tabia haina dawa. On the other hand namwonea huruma sana yule afanyaye uzinzi kwasababu ya vitu anavyovikosa kama wafanyavyo wanawake walio wengi. Hawa kwao wakipatiwa wanavyovikosa basi hawata fanya hayo.
nihitimishe kwa kusema ni kitu kibaya sana kwa mwanaume au mwanamke kupanda kitanda cha mwenzio. Huu ni unyanyasaji ambao dhmbi yake lazima itakumaliza tu. Nawatia moyo akina mama wanaopitia katika hali hii jamaani msiumie zaid, hata Mungu anakubali kutalikiana iwapo mmoja atakamatwa kwenye uzinzi. So usiangalie mazingira decide from there kisha uone lazima utatoka tu. Ila siwez kukutia moyo eti uvumilie hata siku moja usiumize moyo wako kwaajilia ya jitu lisiloona thamani yako.
kwani Eiyer COLD WAR NI UJINGA!??? hebu nifafanulie hapo ujinga unakujaje, kama nimeamua kuwa SILENT! lengo ni ujiulize mwenyewe, ujikalishe kikao mwenyewe, ujijibu mwenyewe, na kutafuta solution mwenyewe, Sababu kubwa ni kwamba, wakati unaanza ulianza mwenyewe na huyo nyumba ndogo yako, sasa iweje leo nimejua TUSHIRIKISHANE??? ulianza mwenyewe, basi MALIZA MWENYEWE! mimi ni MKEO na nitabaki MKEO MILELE!Anaefanya uzinzi ni mjinga,lakini anaelipa ujinga kwa ujinga ni mjinga zaidi!
Haya mambo ni complicated sana. Ni vigumu sana ku-generalize...kila uhusiano upo tofauti! Na pia ni vema tuka appreciate kuwa mwanaume na mwanamke wanalitizama 'tendo la ndoa' kitofauti sana na hata jamii kwa ujumla suala la mwanaume kuwa na multiple partners linatazamwa kitofauti ukilinganisha na mwanamke kuwa na multiple partners.
Na kwa kadri siku zinavyokwenda, uhusiano kati ya kupenda/kupendwa na tendo la ndoa unakuwa mdogo sana. Tendo la ndoa linajifungamanisha zaidi ni suala la uchumi kuliko mapenzi. Ngono nyingi zinafanyika sio kwa sababu wahusika wanapendana bali ni biashara (mmoja anauza, mwingine ananunua) tu. Na sadly, katika hili zizungumzii machangu doa bali hata ndoa nyingi ukitizama deep down unaona zimejengwa katika msingi huu wa kiuchumi na sio mapenzi kwanza. Kwa hiyo kitendo cha mwanaume kushiriki tendo na mwanamke mwingine, si mara nyingi mke atakitafsiri kuwa hapendwi au huyo mwanamke mwingine anapendwa zaidi. Kwa wanaokumbuka manaweza kurejea ile kesi ya Clinton na Monica na comments ambazo Mama Clinton alizitoa kuhusu kadhia hiyo!