Khaa! ..Hebu na Tujitambue...

Khaa! ..Hebu na Tujitambue...

kwani Eiyer COLD WAR NI UJINGA!??? hebu nifafanulie hapo ujinga unakujaje, kama nimeamua kuwa SILENT! lengo ni ujiulize mwenyewe, ujikalishe kikao mwenyewe, ujijibu mwenyewe, na kutafuta solution mwenyewe, Sababu kubwa ni kwamba, wakati unaanza ulianza mwenyewe na huyo nyumba ndogo yako, sasa iweje leo nimejua TUSHIRIKISHANE??? ulianza mwenyewe, basi MALIZA MWENYEWE! mimi ni MKEO na nitabaki MKEO MILELE!

cacico, nimeipenda hii post yako, hasa pale anapoona kaharibu kisha aja na kuanza kukuomba mshirikiane kuificha aibu kwa kuwa nyie ni familia!! Ila hapo kwenye red mpenzi utabaki hata kama kamleta kitandani mwako? achilia mbali umejua kuwa anakucheat?
 
Natamani kuielewa hii thread lakini nashindwa....

Kwamba kutembea na mme wa mtu siku hizi haikwepeki?
Kwakuwa haikwepeki basi mbanjuano huu ufanyikie gesht haush?
Kwamba ukifanyikia kwenye kitanda cha wanandoa ni kuvunjiana heshima na kudharauliana?

Sisi watumishi wa Mungu tunajiuliza tukishangaa.... Hivi kuvunjiana heshima tena too much ni mbaya zaidi kuliko kutenda dhambi?

Hapa sisi wazee tunasema, ukiamua kula nguruwe chagua aliyenona. Unapoamua kucheat, cheat responsibly..... Iwe Maporini, mahotelini, gesht haush, kwenye magari, maofisini, nyumbani au popote pale ili mradi tu MSIFUMANIWE mkawaumiza spouses wenu....... Hilo la Dhambi Mungu wetu atajua la kuwafanya, ndo kazi aliyojipangia.

Baada ya kusema hayo napenda kuwasalimu MwanajamiiOne, Kongosho, Kipipi. gfsonwin popote pale mlipo. Nimewasoma sana na nimewaelewa. Nasahihisha mitihani yenu. Wazee wenzangu TIMING, Dark City na Mbu ntawasalimu baada ya kumaliza kuwasomeni.
 
Last edited by a moderator:
SMU aksante nakubaliana na wewe kwa asilimia zote zilizomo lakini ndo amlete nyumbani, kitandani kwa mkewe/mumewe?

Kuna rafiki yangu ameniuliza kuwa tunaichukuliaje pia kima mama wanaotembea na vijana wao wa kazi, shambaboy au gardener katika vitanda vyao vya ndoa. Nadhani the feelings, blames are the same!

Tumeambiwa ndoa na ziheshimiwe siku zote, lakini kwa kuwa hali halisi inaonyesha kuwa hii imekuwa ngumu, basi hata vitanda vya ndoa tunaviabuse?

gfsonwin amesema cheat but nisijue wacheat!
MJ1, kwani kitanda kina thamani gani katika maisha ya ndoa? Kina thamani kubwa kuliko 'mitambo' yenyewe? Na kama 'mitambo' ina thamani kubwa kuliko kitanda (cha ndoa), na mtu yupo tayari kuruhusu mitambo hiyo 'kutumiwa' na mtu baki itakuwa kitanda.

Nimekumbuka maneno ya mke wangu miaka ya nyuma kidogo alikuwa anasafiri kwa muda mrefu (zaidi ya mwaka!), moja kati ya nasaha zake kwangu ilikuwa ni kutokuleta hawara hapo nyumbani (kwenye kitanda cha ndoa)......hakusema nisiwe na hawara! Nikabaki najiuliza thamani ambayo kitanda cha ndoa kinapewa.

Kwa vyovyote vile, cheating popote inapofanyika mimi naamini haikubaliki.
 
Huo ndio ukweli wenyewe,wapashe wanawake wenzio walijue hilo,huko nje tunatembea ili kupunguza mihemko tu siyo kama tunawapenda kihiiivyo.
 
Soulmate bana hebu nisome tena hapo kwa uzuri. Hiyo ya fungasha mabegi ni tafsiri niipatayo mie toka kwa mwanaume afanyaye hayo. Kuwa akifikia hatua ya kumleta mwanamke mwingine kwenye matrimanial bed yetu atakuwa ananifikishia ujumbe wa ............Mama Chanja, sikuhitaji tena hebu fungasha vyako usepe.

Eti akili si zake, zaziazima?

.....mwanajamiiOne bana.....hebu zunguka pande hii uangalie tena hapa nazungumzia 'half empty, au half full!'...

Iwapo mume huye (assumptions) wewe ulimfungulia 9alfajr na hata 11alfajr....ukajikubalisha. Mume huyo huyo akiwa huko 'vikaoni' kuna wanawake/mwanamke unajua anakuwa nao mpk alfajr hizo.....ukajikubalisha. Ni lipi la ajabu usijikubalishe nalo akija 'kutembea' kwako?

E bana nyie hamtaki kunielewa. Mambo haya ni kama jipu,....unalea kipele na usaha, mwisho waugulia donda ndugu. Mlijikubalisha wenyewe, mka ignore the signs....iweje mjithaminishe kwa kitanda cha ndoa pekee? Angefanyia sitting room je? Siwaelewi aisee 😎
 
MJ1, kwani kitanda kina thamani gani katika maisha ya ndoa? Kina thamani kubwa kuliko 'mitambo' yeneyewe? Na kama 'mitambo' ina thamani kubwa kuliko kitanda (cha ndoa), na mtu yupo tayari kuruhusu mitambo hiyo 'kutumiwa' na mtu baki itakuwa kitanda.

Nimekumbuka maneno ya mke wangu miaka ya nyuma kidogo alikuwa anasafiri kwa muda mrefu (zaidi ya mwaka!), moja kati ya nasaha zake kwangu ilikuwa ni kutokuleta hawara hapo nyumbani (kwenye kitanda cha ndoa)......hakusema nisiwe na hawara! Nikabaki najiuza thamani ambayo kitanda cha ndoa kinapewa.

Kwa vyovyote vile, cheating popote inapofanyika mimi naamini haikubaliki.

Ni kweli kabisa SMU cheating sehemu yoyote haikubaliki na ndio maana ninashangaa wale wanaofikia kuamua kucheat na kama haitoshi kuiweka hadharani namna hii. Kwa wanaume am sorry to say kuwa ninalazimika kuamini kuwa mmeumbiwa kuexplore (nadhani nimeathirika na mauwongo ya Men are from Mars and Women from Venus kama sijakosea). Ndio maana nikaangalia upande wa wanawake wenzangu, inakuwaje unapokuwa tayari kucheat na mume wa mwenzio (tuassume unafahamu) na kama haitoshi unakubali akulete nyumbani kwake juu ya kitandan chake na mkewe.

Hata hivyo majibu niliyoyapata hapa jamvini yamenisaidia sana maana na-unaive wangu nimejifunza mengi.

Na hata wifi yangu alipokuwa anakuhusia juu ya safari yake ni wazi naye ameathirika kama MwanajamiiOne hapa kuwa wanaume ni hulka yao kucheat, kitu ambacho baada ya kuja JF nimegundua kuwa si wote na si kweli!
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Ndugu yangu hakuna sababu yoyote ya msingi inayowapush kuamua kufikia hapo,
basi tu wame za watu (wengi wao) siku iz kama wamewehuka, macho juu juu kama wanachambua mchele wako na matamanio yasiyozuilika sijui aisee wanashindwa kujizuia kwa lolote nadhan wana mapepo kwa sababu hali zao ni tete, hawaheshimu ndoa zao, si wake zao wala familia zao.
My darling and dear obsesd, unawazungumziaje wanawake wanaokubali kumegwa na waume za watu? Mnatulaumu waume wa watu lakini mnasahau kuwa huwa hatuwabaki bali chup.i mwazivua wenyewe ilhali mkijua tuumeoa. Tunyimeni basi tukabake mitetea na mbuzi mee....khaa!
 
Last edited by a moderator:
.....mwanajamiiOne bana.....hebu zunguka pande hii uangalie tena hapa nazungumzia 'half empty, au half full!'...

Iwapo mume huye (assumptions) wewe ulimfungulia 9alfajr na hata 11alfajr....ukajikubalisha. Mume huyo huyo akiwa huko 'vikaoni' kuna wanawake/mwanamke unajua anakuwa nao mpk alfajr hizo.....ukajikubalisha. Ni lipi la ajabu usijikubalishe nalo akija 'kutembea' kwako?

E bana nyie hamtaki kunielewa. Mambo haya ni kama jipu,....unalea kipele na usaha, mwisho waugulia donda ndugu. Mlijikubalisha wenyewe, mka ignore the signs....iweje mjithaminishe kwa kitanda cha ndoa pekee? Angefanyia sitting room je? Siwaelewi aisee 😎

.....Sawa hapa nimekuelewa suppose hakukuwa na signs zozote? Supposed he pretended kula na kipofu, so silent the so-called perfect hubby and then umesafiri akajifungua makucha na kumleta nyumbani ...................Bado utasema nilijikubalisha? Mie ambaye hata kufikiri kuwa anawezakuwa anacheat sikuwahi?
 
My darling and dear obsesd, unawazungumziaje wanawake wanaokubali kumegwa na waume za watu? Mnatulaumu waume wa watu lakini mnasahau kuwa huwa hatuwabaki bali chup.i mwazivua wenyewe ilhali mkijua tuumeoa. Tunyimeni basi tukabake mitetea na mbuzi mee....khaa!

Aksante Asprin hili haswa ndilo shina la swali langu, i wapi nafasi ya mwanamke kujitetea na waume za watu? Wengi wameona kama ninamwonea mwanamke na kuwa wa kupambana naye ni mume wangu nakubali but hii ninaiona kama ni sawa na kusema kuwa wanawake wanaotongozwa hawana utashi wa kuamua. Yaani yeye akitongozwa, ni sawa, akipelekwa nyumbani kwa Bibi ni sawa, vichakani ni sawa......yeye hana utashi wa kujua hii ni kuvuka mipaka? Amecheat na mume wa mtu, ni kosa analijua na bado anakubali kumalizia kabisa kwa kurisk kupelekwa kwa mwenye mali!! hapa tena si kuiba bali kunyang'anya kwa kutumia nguvu.

Hivi nikimkuta ndani mwangu, kitandani mwangu mwanamke wa aina hii ambaye najua fika kuwa anajua kuwa huyu mwanaume ameoa na hapo alipoletwa ni nyumbani, kitandani mwao na mkewe, nisimmwagie mafuta ya moto usoni kwa nini?
 
By MwanajamiiOne<br />
SMU aksante nakubaliana na wewe kwa asilimia zote zilizomo lakini ndo amlete nyumbani, kitandani kwa mkewe/mumewe? <br />
<br />
Kuna rafiki yangu ameniuliza kuwa tunaichukuliaje pia kima mama wanaotembea na vijana wao wa kazi, shambaboy au gardener katika vitanda vyao vya ndoa. Nadhani the feelings, blames are the same!<br />
<br />
Tumeambiwa ndoa na ziheshimiwe siku zote, lakini kwa kuwa hali halisi inaonyesha kuwa hii imekuwa ngumu, basi hata vitanda vya ndoa tunaviabuse?<br />
<br />
gfsonwin amesema cheat but nisijue wacheat!
MJ1, kwani kitanda kina thamani gani katika maisha ya ndoa? Kina thamani kubwa kuliko 'mitambo' yenyewe? Na kama 'mitambo' ina thamani kubwa kuliko kitanda (cha ndoa), na mtu yupo tayari kuruhusu mitambo hiyo 'kutumiwa' na mtu baki itakuwa kitanda.<br />
<br />
Nimekumbuka maneno ya mke wangu miaka ya nyuma kidogo alikuwa anasafiri kwa muda mrefu (zaidi ya mwaka!), moja kati ya nasaha zake kwangu ilikuwa ni kutokuleta hawara hapo nyumbani (kwenye kitanda cha ndoa)......hakusema nisiwe na hawara! Nikabaki najiuliza thamani ambayo kitanda cha ndoa kinapewa.<br />
<br />
Kwa vyovyote vile, cheating popote inapofanyika mimi naamini haikubaliki.

...THANK YOU kwa herufi kubwa
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Dahhhh
nashindwa kuelewa , Hivi kama unajua fika huyu ni mume wa mtu anafamilia yake,
unamfuata wa nini? Hii ya kwenda mpaka kitandani kwake imepita kiasi (disgusting)
ni aibu kwa kweli ..

Eti wanasema mapenzi yanasababisha upofu wa macho na akili...especially wakati muhusika ameshikwa na kukunwa "pabaya".
 
Eti wanasema mapenzi yanasababisha upofu wa macho na akili...especially wakati muhusika ameshikwa na kukunwa "pabaya".

Ndahani bwana jiulize ni kwa nini mtu anaRUHUSU kushikwa na kuanza kukunwa in the first place?? Sababu ziko nyingi na nyingine ni genuine kabisa !!
 
Ndahani bwana jiulize ni kwa nini mtu anaRUHUSU kushikwa na kuanza kukunwa in the first place?? Sababu ziko nyingi na nyingine ni genuine kabisa !!

Mi naona social interactions zetu zimeondoa barriers ambazo zilikuwepo miaka ya nyuma. Kazi,elimu na kipato jinsi ilivyo sasa hakuna tofauti kati ya wanaume na wanawake. Kama wote tuko sawa, na ubinadamu unatusukuma tuwe na mahitaji sawa, kwanini nijizuie kula ile chakula roho inapenda?? Kuanza inaweza kuonekana ni kitu cha kawaida...ila mahusiano yanaweza kukolea endapo ukaribu wa wahusika utaongezeka halafu wakaanza kupeana mambo waliyokuwa wanayaotaota.
Kulala kwenye nyumba ya mwanaume aliyeoa sidhani kama itaanza mara moja tu kwenye uhusiano...itakuwa ni kitendo cha kuonyesha sasa nimefikia fainali na wewe mwanamke mwenzangu kama unafikiri ndo mwenye nyumba wajidanganya. Maana haiingi akilini utaanza vipi kulala kwenye nyumba yenye mwanamke ndani ambaye ndiye aliyeolewa....
 
Mi naona social interactions zetu zimeondoa barriers ambazo zilikuwepo miaka ya nyuma. Kazi,elimu na kipato jinsi ilivyo sasa hakuna tofauti kati ya wanaume na wanawake. Kama wote tuko sawa, na ubinadamu unatusukuma tuwe na mahitaji sawa, kwanini nijizuie kula ile chakula roho inapenda?? Kuanza inaweza kuonekana ni kitu cha kawaida...ila mahusiano yanaweza kukolea endapo ukaribu wa wahusika utaongezeka halafu wakaanza kupeana mambo waliyokuwa wanayaotaota.
Kulala kwenye nyumba ya mwanaume aliyeoa sidhani kama itaanza mara moja tu kwenye uhusiano...itakuwa ni kitendo cha kuonyesha sasa nimefikia fainali na wewe mwanamke mwenzangu kama unafikiri ndo mwenye nyumba wajidanganya. Maana haiingi akilini utaanza vipi kulala kwenye nyumba yenye mwanamke ndani ambaye ndiye aliyeolewa....

Yaani.............. umenikumbusha forum moja nliwahijoin wakati nasoma, watu walikuwa wanakuwa wawazi hadi unaogopa. Maswali ya why unacheat, kwa nini unatoka na mume/mke wa mtu, why uliipindua ndoa ya mwenzio yalikuwa yanajibiwa wazi wazi tena kwa shuhuda hadi mtu unatetemeka na am telling you kulikuwa na mengi sana ya kujifunza.

Kwa JF kidogo nadhani na kufahamiana nako kunachangia watu kujifichia moyoni yaliyono moyoni mwao. Matokeo yake tunakwepesha ukweli wa mambo ambayo yanatendeka. Wengi tunasema cheating haikubaliki, ni kweli haikubaliki lakini inatendeka kwa kiwango kikubwa na inavunja mahusiano mengi tu. Laiti tungepata forum kama ile ambapo watu wanafunguka why wanacheat, n.k pengine ingetusaidia sana.
 
Yaani.............. umenikumbusha forum moja nliwahijoin wakati nasoma, watu walikuwa wanakuwa wawazi hadi unaogopa. Maswali ya why unacheat, kwa nini unatoka na mume/mke wa mtu, why uliipindua ndoa ya mwenzio yalikuwa yanajibiwa wazi wazi tena kwa shuhuda hadi mtu unatetemeka na am telling you kulikuwa na mengi sana ya kujifunza.

Kwa JF kidogo nadhani na kufahamiana nako kunachangia watu kujifichia moyoni yaliyono moyoni mwao. Matokeo yake tunakwepesha ukweli wa mambo ambayo yanatendeka. Wengi tunasema cheating haikubaliki, ni kweli haikubaliki lakini inatendeka kwa kiwango kikubwa na inavunja mahusiano mengi tu. Laiti tungepata forum kama ile ambapo watu wanafunguka why wanacheat, n.k pengine ingetusaidia sana.

Cheating sasa hivi hivi ni kama order of the day. Ila pengine kuficha tatizo kunatufanya tusijijengee uwezo wa kulitatua na kuona kama ni kitu cha kawaida. Kwa JF as you say, kuna ugumu kidogo....ila hiyo forum kama ipo kwanini usiipigie debe. Ntajiunga nayo lakini si kama Ndahani...you will see really me.
 
Dah kweli JF MMU ni kisima cha elimu. Haya kwa ninavyowasoma hapa ni kama vile mnanilazimisha niamini kuwa fate ya mwanamke kutongozwa na kuletwa nyumbani kwa mwanamke mwenzie iko mikononi mwa mwanaume!!! Yaani mwanamke hana jinsi wala uwezo wa kujithamini bali anasubiri kuthaminiwa na mwanaume hata kama ni kwa unafiki!
QUOTE]

Toa au badilisha assumption zifuatazo:-
1. Wanawake siku zote ni victims
2. Wanawake wote wanataka kuolewa (ultimate goal ya mwanamke ni kuolewa)
3. Kwa mwanamke kufanya ngono lazima kuna motive fulani na sio kwasababu anataka kufanya ngono
4. Moral issues ni universal, meaning unachoona wewe immoral na mwingine lazima aone hivyo (hii kwa case ya kujithamini kwa mwanamke)

Mwisho waweza kuniona mimi naenda kinyume na vitu vingi; lakini ni kwamba, uzoefu umenifanya niache kuimpose my moral standard to others kwani nimeona haifanyi kazi mara nyingi (imagine wengi tunahudhuria ibada mbali2 lakini bado tunatenda kinyume na tunayoambiwa); trick ninayoitumia hasa pale ninapofanya kazi ya kufundisha kitu kwa au community au audience niliyo nayo ni kuwork with what they believe. Hapo ni upande wa kuimpose what l believe.

Otherwise, as a scientist; nimejifunza kuanalyze na kutafuta root cause ambayo naweza deal nayo directly au nina access nayo. For this case ni mume wangu; in as much as l wish hao wadada wangeacha kuchukua wanaume wa wengine, l know siwezi kuimpact sana so why waste my time and energy?
 
Ndahani bwana jiulize ni kwa nini mtu anaRUHUSU kushikwa na kuanza kukunwa in the first place?? Sababu ziko nyingi na nyingine ni genuine kabisa !!

MJ1,hebu rudi unihabarishe hii kitu tafadhali,siijui sababu kabisa!
 
imenikumbusha msukuma na kigaloni chake walivyonitimulia vumbi, but mdada alihofu tu nilikuwa cna shida nae hata kidunchu, yani cku zile kwa msukuma ningeharibu mazima, familia yake ingemweka kikao asinirudie aisee, sasa hiyo ya kuwakuta ndani tena nasema ipitie kando mana hiyo dharau haielezeki kabisa, chaaaa, mie nilivyowakuta niliona ni dharau tosha sasa hii ya ndani cjui nitafanyaje, huyo mdada yeye ajiondokee tu aniachie msala wangu.....wanaume vichomi hawa.
 
huku kujichimbia kuna hasara sana, ona sasa nimekaribia kupitwa hapa.
Naona habari ni nzito hapa........................... ila nadhani tatizo siyo kukosa hela ya gesti, nadhani hawa wote wanakuwa wezi, na wanakuwa na status fulani hivi.............. so, safe place ni home, either husband au wife akisafiri, period!
 
Back
Top Bottom