Khaaaa!!Kwani ni lazima?

Eiyer

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2011
Posts
28,259
Reaction score
20,891
Inawezekana labda natakiwa nikaishi sayari ya Mars.Hivi ni lazima ukiwa na mahusiano na mwanamke umhudumie kama mwanao(sizungumzii ndoa).Leo nimekasirikiwa na dada mmoja baada ya kunilalamikia kuwa rafiki yangu ni mbahili.Mi nikamwambia,sasa unataka akupe hela kwani wewe ni mwanae au mkewe?Yule dada alisonya akanyanyuka kitini na kuniangalia kwa shari kisha akaniambia,"kumbe na wewe ni wale wale",kisha akaondoka.Hivi kwani ni lazima upewe hela?Mtu una kazi,au uko kwa baba na mama yako halafu unataka hela!Za nini?Unaweza kusaidia lakini inapoonekana kuwa unaanzisha mahusiano na mwanamke shida zote anahamishia kwako huo ni ujinga.Tujuane inapotokea dharula sio ndo nakua dingi!!
 
Mwambie akatafute kazi.

Teh,teh,teh,teh!Ngabu u made ma night!Sidhani kama atanisemesha maana baada ya kumwambia akakasirika sana!Akirudi nitamwambia atafute kazi ya kufanya!
 
Girlfriend anayeomba omba ela hana sifa huyo...Hakuna mabinti ninao wa admire kama walio independent...Huwezi kufanikiwa kimaisha kama unajua kuna mjinga mjinga wa kunipa ela pindi ninapohitaji.

Sikuwahi maishani kumuomba mwanaume ela..hata nilipokuwa nina shida kimbilio langu lilikuwa ni dada na kaka zangu. You know why...Nilikuwa najua nikimwomba kaka atakuwa free kunambia kama hana...nikimuomba boyfriend ela hata kama ni kweli nina shida itamuwia vigumu kunambia hana pindi akiwa hana...na itamfanya ajione mdogo.

Hayo ndio mapenzi. Siku hizi tatizo kila mtu amekaa kimaslahi. Utasikia discourses za hajabu..ananitumia...ananichezea...lazima nimchune...yule mjinga bwana ake hamnunulii hata chupi...Lol. hivi mtu unawezaje kuwaza kuchezewa na kutumiwa na umpendaye? Kwani anakubaka?
 
So sio lazimaeee . . . . . . . !!!!

Kama dada anajiona yupo kazini basi ataona ni lazima alipwe kwa huduma anayo itoa, na nadhani itakua fair kwa kaka kum-evaluate na ikibidi kum-replace ikiwa huduma hiyo haimridhishi. ila kama ni mapenzi sioni haja ya kumpa hela zaidi ya zawadi za hapa na pale (zawadi go both ways).
 
Nyumba Kubwa unakunywa bia gani vile?Nataka nikupongeze kwa hilo li post la ukweli hapo juu!
 

No walikua katika mapenzi tu!Ndo maana nikajiuliza sababu ya yeye kununa.Lakini mabinti wengi wapo kama huyu!
 
Hiyo aliyo nayo sasa siyo full time. Akatafute kazi full-time halafu hiyo ya kupiga mizinga wanaume aibakishe kama part-time.

This way she'll hardly ever be broke.
Kuna aina nyingi ya relationship (just like kuna aina nyingi ya wanawake, aina nyingi ya wanaume na endless combinations). Hiyo based on money ipo sana, na ikiwa muhusika wa kiume anashindwa ku-suply hela za kutosha anatafutwa msaidizi wake (ikibidi wawili watatu) na maisha yanakwenda. wanaume nao wanasuscribe kwa wasichana wawili watatu na wanapeleka maisha kwa mtindo huo. and they all believe they are in a relationship.
Kwangu mimi sio sawa, na sio lazima wapenzi kupeana hela za matumizi. Ila this is based on my definintion of a relationship. they have theirs.
 
Bia sijawahi kujaribu mdogo wangu naogopa kitambi. Natumia wine ya aina yoyote...sichagui brand wala rangi mradi wine.

Haya,nakutumia "jet"sasa hivi ije ikuchukue ikulete Malaika Hotel ugonge kisha urudieeee!
 
Hiyo hotel iko Mwanza eeh...Jina si geni. Ngoja nikae mkao wa kunywa.Lol. Afu sasa ungejua mwisho wangu ni glasi moja...sasa hiyo gharama ya jet si asavali ungetuma hiyo ela kwa M-Pesa.


Haya,nakutumia "jet"sasa hivi ije ikuchukue ikulete Malaika Hotel ugonge kisha urudieeee!
 

Be that as it may it is shameful for any able-bodied grown ass man or woman to be hitting up others for some money.

My philosophy on people like that is 'go get a job, dammit'.
 
Hiyo hotel iko Mwanza eeh...Jina si geni. Ngoja nikae mkao wa kunywa.Lol. Afu sasa ungejua mwisho wangu ni glasi moja...sasa hiyo gharama ya jet si asavali ungetuma hiyo ela kwa M-Pesa.

Usijali gharama,ni katika kuonesha nimeikubali post yako.Yes Malaika iko Mwanza.Lakini if u like nitakutumia kwa M-pesa,namba yako si ileile?Naikumbuka ni 0769 000 001!!Hebu ni-DIPU sasa hivi!
 
Una kumbukumbu nzuri. You must be genius! Ni yenyewe kabisa.

Usijali gharama,ni katika kuonesha nimeikubali post yako.Yes Malaika iko Mwanza.Lakini if u like nitakutumia kwa M-pesa,namba yako si ileile?Naikumbuka ni 0769 000 001!!Hebu ni-DIPU sasa hivi!
 
Mwanamke anayejitambua hua haombi pesa kwa mpenzi wake hata siku moja....mwanaume anayejielewa hua hasubiri kuombwa pesa hua anatoa tu kwa kujua wajibu wake!! Wanaume acheni ubahili jamani hebu toeni kwa wale mnaowapenda mbarikiwe lol! Simaanishi uwe unamuhudumia kwa kila kitu wala sio umpe kila siku but where necessary at least once per three month sio mbaya! Sometimes unakuta hana kazi by that time, ukimuona kavaa vizuri anavutia unadhani anapata wapi hela ya kujikeep smart kama wewe hujawahi mpa hata siku moja??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…