Khaaaa!!Kwani ni lazima?

nyumba kubwa, hapa tutatofautiana kidogo. sina mabinti wakubwa lakini ninao, na MUNGU akinipa pumzi nikaanza kuona wanavyoanza ku-date nitafanya hivi.

kwanza nitawafanya my friends, hiyo nimeshaanza kuijenga am sooo kloz kwao, kuna umri ukifika nimeona mabadiliko i mean kwenda mbalamwezini nitaanza kuwapa pesa kidogo ya matumizi kila mtu mwisho wa mwezi inshaallah nikipata tu mshahara, nakumbuka my mum used to do this na ilitusaidia sana! nitawaambia jamani chonde chonde dont ask of anything from a boy friend, NEVER! nipo hai kam to mama/papa. pesa ninayowapeni each of u ni kwa matumizi yenu madogo madogo, yale makubwa plz report kwangu! hii itawajengea itikadi ya kwamba NO MIZINGA FROM GUYS, parents can do. na kama una biashara anza kumshirikisha mapema ili aanze kujifunza kujitegemea na ku-save. kwamba anaweza akawa anakaa shop weekends na unamlipa end of month!

by the time anamaliza a-level anajua wapi pa kuingilia, wapi pa kutokea, bila kuwa na kasumba ya MIZINGA, na mzazi ukiwa provider! wapeni magari pia kama wapo above 18, hawatadanganywa huko nje, wala kuwa na tamaa za kijinga kwa guys!

mjengee misingi ya dini, AWE NA HOFU YA MUNGU, ongea naye kuhusu mimba, HIV, etc, nenda naye mazoezi, mshirikishe mambo yako, mwambie mume mwema si yule mwenye pesa HAPANA! ni yule MWENYE UPENDO WA DHATI KWAKO AND VICE VERSA! poleni nimewachosha! malezi yanamatter! THANX TO MY PARENTS!
 
Last edited by a moderator:
Kama ni utukufu mwambie basi atowe yeye kwa huyo rafiki yako ili awe mtukufu!
 

umenigusa hapo pekundu haha nicheke mie , pole zao karolite mie vaseline mwanzo mwisho
 
Nakwambia ndio maana wanaume wanakufa upesi kuliko sisi wanawake...ni kwa sababu tumekuwa mizigo.

Navyompenda mume wangu siwezi kumuachia jukumu la kutunza familia eti kisa mimi mwanamke. Asije kwaa BP bure. Maisha yenyewe magumu bila kushirikiana kwa nini mtu asipate BP au kisukari.

 
Yaani tukifika hapo, ni hatari sana...there is more to spice up love than pesa jamani...pesa is not the ultimate spice to love and if u subscribe to that, hapo ujue kuna tatizo tena kuuubwa kabisa! kha



HAPANA Kaizer! pesa si kila kitu! ila pesa ina mhimili mkubwa sana kwenye relationship! kila kitu kinahitaji pesa, kila kitu my dear! ila point ni how u provide kwake and vice versa!, kwamba ni vipi unamjali huyo mwenzi wako! alipokuwa na wewe aliujua uwezo wako, na wewe waujua wake. huwezi kuomba beyond his limit and vice versa! hata kama unalipwa 50,000, elf 10,000 mpe kila mwezi! bby hii yako ya salon! hata kama anafanya kazi, she will b more than happy kujua kwamba my hubby/sugar wangu shares with mi hicho hicho kidogo alicho nacho!


na usithubutu kumwambia mkeo SINA! inakupunguzia UANAUME WAKO! coz tumejijengea kwamba men can do, no matter what, mwambie NIMESIKA NAKUTAFUTIA BBY WANGU, JUS GIVE 2 DAYS! anaona partner wangu ni fighter ni mwanaume


kwamfano: mimi nipo hivi nikimuona mwanaume anakunywa wine, cjui namuonaje?? lakini nikimuona mwanaume anakunywa guiness, au nyagi, yaani nasikia raha hata kukaa naye, nafeel nipo secured! hata nikimaliza mizimnga miwili ya wine, my man IS THERE FOR MI! COZ ANAONYESHA HUYU NI KICHWA! ni mimi tu jamani mtazamo tu!
 
Last edited by a moderator:
Ninakubaliana na wewe asilimia 150

Wakati wengine wazazi wanachangia watoto wao kuwa kupe. Hata ndugu pia. Kuna siku boyfriend wangu ambaye sasa ni mume wangu alipanda basi akakutana na room mate wangu akiwa na dada zake kama watano. Yule mate wangu si akawa anatia story na boyfriend wangu...eeeh dada zake konda alipoanza kuomba ela wakasemaje..shemeji hapo atalipa

Huo ni mfano wa familia za hovyo...huyu mate wangu kwao ni wachunaji wazuri...akiwa na boyfriend basi atapigwa mizinga kuanzia na huyu mdada mpaka ndugu zake. Walikuwa ni washenzi kweli kweli na ni walevi kupindukia. Kutokana na hiyo tabia yake na ndugu zake..huyu dada ana date mtu kama ana cash ....nothing more or less


Mimi wazazi wangu hawakunilea kunipa kila ninachotaka...baba yangu alikuwa anatoa matumizi ya lazima tu...kwa ufupi sijuhi niseme alikuwa mbahili. Lakini japo nilikuwa most of the times nimechacha...nilikuwa nakufa na tai shingoni...kuomba siwezi kabisa.

 

you are very intelligent aisee. Mimi aisee hadi nimpie mr mzinga ama nimwachie eti alise atunze familia hata ubuyu na karanga nauzaga darasani na ice craem na maji ya condom nauza home pasi aibu ili kukwepa hii fedhea lol!

mimi pesa yak nipe ila sikuombi aisee. hata kama ni buzi hela yako sitaki kabisa mimi natafuta zangu zako peleka kwa mkeo huko sisi tupeanepo raha tu.
 
Point nilotaka kuzungumzia hapo ni kuwa hakuna mwanaume atakaye ona rahisi kumwambia mwanamke sina ela (labda kama ni husband and wife) kwa hiyo unasababisha embarrassment kumuomba ela boyfriend wako.

Ni sawa na tabia ya baadhi ya wadada kwenda kukopa ela kwa wanaume (say office mates) knowing kwamba wataona vigumu kuwadai.

Kaka au dada yako kama hana anakupa live (za uso)

Si unaona mdau mmoja hapo juu amesema mwanaume akiombwa ela kama hana yuko tayari kukopa ili asikunyime. Sasa uoni vibaya kumpa umpendae wakati mgumu. Ndo maana nasema where money is involved hakuna cha penzi.

Anayemuomba kaka ni more likely kuwa independent kwani for sure huwezi kumuomba kaka yako ela kila siku...lazima uwe na genuine reasons...kwani atakubali kuwa buzi la dada yake?



kwahiyo nyumba kubwa binti anayemuomba hela kaka au dada ni independent ila akimuomba mwanaume ni dependant au sijaelewa?
 
Utakuta demu anakuzungusha hakupi K alafu anakupigia simu kabana sauti yuko mme nna shida na elfu 50.

Yaani huyu hataniona kamwe!
 
cacico shemeji, huu mtizamo mbona sio ambao ungependa kuwajengea mabinti zako? I mean uko soooo diffferent na ulichokisema hapa chini lol hebu nijibu hapo kwanza....




 
Last edited by a moderator:

baby gfsonwin namwona Nyani Ngabu kagonga like sasa sijui ni kipengele kipi kimemfurahisha apo...lol

 
Last edited by a moderator:
Last edited by a moderator:

Furaha when it comes my monay eeeh!
 
My sweet love Eiyer, nitafutie basi kishughuli ili nisikuombe pesa. Maana mama yangu siwezi mtegemea kwani yeye ndio ananitegemea!

Twende tukauze ile nyumba ya urithi iliyopo Nyamanoro ili uanze mama ntilie!!
 
Naomba nikupinge ndugu yangu...wake za mamilionea ndio mabingwa wa kuchiti...kwa hiyo kumgharimia mwanamke haina maana kuwa kunaongeza uaminifu dear.

 
If you aren't in rltn better not get involved.Otherwise you will be categorized as among the employers.worse enough,Girlz have made this as one their basic RIGHTS.Cheers.
 
yaani mkubwa hii tabia imevuka mipaka,wanawake wanahisi kupewa hela ni haki yao ya kimsingi kwny katiba,hata p**d wanataka wanunuliwe na wanaume,ndio maana hata kiwango cha kufikiri kimepungua coz they are like floating logs

Yaani mpaka wanakera aahh!!
 
Kiukweli umegusa NYOYO za wanaume wengi...ila mi binafsi napenda mwanamke anipe yeye pesa ila simuombi...!ila mimi kutoa ningumu...bora niende Kona bar!!!
'Mali uongeza furaha ya mwanamke katika maisha'-Shaban Robert
"vox populi 'vox dei"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…