Kheri James: Kumtukana Rais sasa basi

Kheri James: Kumtukana Rais sasa basi

Wewe subiri usije ukasema hukuambiwa
Kwa hiyo mnaamini mtamdhuru Lissu jukwaani Bavicha wakiwa wanawaangalia tu? Mmesahau mlivyofanya Hai mwnzenu akazindukia hospitali? Mmekwenda kuiba fomu Ukara mwenzenu katangulizwa mbele za haki, mmebadili fomu Mbozi wenzenu 2 RIP?
 
Ha ha ha haaaaaaa......
Uhuni gani wanao zaidi ya zile risasi walizommiminia Lissu?
Ccm tafakarini kwa utulivu na mjiulize kwa nini Mungu alimkinga Lissu na risasi nyingi hivyo mwilini mwake. Kama hamjui ni ili Muumba ajitukuze katika tukio hili kwa hichi kizazi kisicho imani.
Yale ya farao katika bahari ya Shamu huenda yakajirudia miaka kama 4000 baadae.
Kazi yetu sisi ni maombi lakini hata hivyo maombi yana pande mbili, ama kukubaliwa au kukataliwa.
 
Sio lisu tu ni mtanzania yeyote kama raisi attainable na yeye atatukanwa sana tu
 
Watanzania sasa ni lazima tuseme, mgombea kutumia ukabila kutafuta kura, huku NEC ikiwa kimya, tusema SASA BASI. NEC kutumika kama taasisi ya chama, na kufanya kazi ya kuengua wagombea badala ya kusimamia mchakato wa uchaguzi sasa tuseme IMETOSHA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na yeye atashikwa pabaya zaidi. Jino kwa jino hadi itambidi arudi kwao Ubeligiji akaendelee na lockdown ya covid 19.
Hakuna mtu wa kumwondoa mtu mwingine. Nchi hii ni ya Watanzania. Watanzania ndio wanaoimiliki Tanzania. Hakuna mtu wa kuwatisha wengine wala kuwababaisha wengine.

Mmeteka, mmeua, mmepoteza watu, nmewaonea watu, SASA BASI.

Siasa zenu za kifashiti hazina nafasi tena. Tunataka watu waongozwe kwa misingi ya haki, usawa, uhuru na kidemokrasia.

Utawala wa awamu hii umedhalilisha Taifa kwa kutupeleka kwenye siasa za kishamba. Siasa za kutishana na watu kutaka kuabudiwa. Ni Mungu pekee yake ndiye ataabudiwa milele, na siyo mwanadamu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kawe Alumni , miaka yote UVCCM inakuwa na vijana werevu, wajibu hoja na wanaosaidia sana chama cha Mapinduzi, kuanzia akina Emmanuel Nchimbi, John Guninita, Nape Nnauye, Hussein Bashe, Masauni Yusuf na kadhalika, lakini sijaona kijana mpumbavu ambaye CCM imepata kuchagua kama huyu Heri James. Ni mpumbavu sana. Hakisaidii chama, zaidi ya kukiangamiza. Tangu amechaguliwa yeye ni kejeli na vitisho kwa wanaopishana naye kimawazo na mitazamo, hana constructive ideas kama hao niliowataja hapo juu. Ni shida sana. I sorry to say that, lakini ndio mtazamo wangu.
Umemaliza mkuu
 

Hahahahahaha hii pimbi inachekesha kweli,sasa itafanya nini .wao wanategemea polisy iwasaidie kupiga watu hivi wakisimama wenyewe uwanjani wataweza kupigana kweli ukizingatia kwa sasa wapinzani ni wengi kuliko ssm
 
Huyu ni aina nyingine ya uchafu ambaye hata kumsikiliza siwezi

Nani katukana?
 
Kwani huyo anayesema 'wakimugusa tu moto utakaowaka hamuna atakayeweza kuuzima' alikuwa anamtisha nani? Huyo anayesema 'mawakala wa chama chake watakapokuwa wanaenda kuapishwa kwa msimamizi wa uchaguzi wasindikizwe na umati wote uliohudhuria kwenye mkutano wake pale Ifakara' alikuwa anamtisha nani? Na kwamba umati wote huo utakapoenda kupiga kura hiyo tarehe 28 Oct 2020 ubaki hapo hapo kwenye kituo cha kupigia kura na kuhesabu kura hizo, alikuwa anamtisha nani? Na akasema maeneo yote nchi nzima wafanye hivyo, alikuwa anamtisha nani?

Arudi tu kwao Ubeligiji akapambane na covid 19, asituvurugie amani yetu. Tanzania ni kitovu cha amani Afrika.

Amani ya wapinzani kukaa kimya wakiwa wanaporwa ushindi wao?
 
Back
Top Bottom