Kiama cha CCM ni halisi kitaondoka na watu

Posho anayolipwa Bungeni jumulisha usumbufu na vitisho vya kumvua uanachama vimemfanya Gwajima ajitoe fahamu ili afukuzwe CCM abakie na injili kanisani kwake kwani inamlipa zaidi kuliko akiwa Bungeni
Duuuuuuuuh, Mkuu umewahi kupitia mapato na matumizi ya ofisi ya Mbunge wa Kawe na kanisa la ufufuo na uzima na kuyajua hayo?
 
 
Ukitaka wananchi wakupigie kura kwa wingi fanya kazi njema na yeye kuonekana machoni pao ili baadaye usije kulia. Hauwatumikii wananchi unashinda kupiga propaganda halafu unategemea upate kura?
Mkuu muda ni rafiki mzuri sana, subiri uone.

Dhalimu alijifanya anafanya kazi, dakika ya mwisho ilibidi anajisi uchaguzi ili atangazwe mshindi. Kibaya zaidi alifanya uporaji wa kishamba mpaka kila mtu akajua.
 
Gwajima yupo tayari hata akose ubunge kwani anaona kanisa kila week linamlipa pesa nyingi lina faida kubwa kuliko kukaa Dodoma kusubiria posho za bunge
Ahadi namba 5 ya mwanachama wa CCM inasema "Cheo ni dhamana, sitatumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu."

Hivyo Gwajima anatakiwa kujua kuwa ahadi namba 5 inasisitiza kuwa uongozi ni utumishi kwa wananchi na sio manufaa kwa mtu binafsi hivyo hatakiwi kutumia vibaya au kumshawishi kiongozi mwingine aitumie vibaya dhamana hiyo.
 
Akina Dialo na wengine waweza kuwa hofu lakini Gwajima yeye kaamua kutengeneza mazingira afukuzwe ili awe huru afanye kazi zake binafsi kwenye makanisa yake
Aliomba uongozi kwa sababu gani?
 
Wanadai pia Chalamila aliomba kuacha kuwa RC Mbeya wakamkatalia wakamuamisha Mwanza kwa lazima ndi akaanza vituko maksudi ili afukuzwe
Mkuu aliyekuambia alikulisha matango pori 😂😂😂😂
 
Ukitaka wananchi wakupigie kura kwa wingi fanya kazi njema na yeye kuonekana machoni pao ili baadaye usije kulia. Hauwatumikii wananchi unashinda kupiga propaganda halafu unategemea upate kura?
Mkuu muda ni rafiki mzuri sana, subiri uone.
Kura gani? Kama unazungumzia hili kura wazoiba Ccm kwa kushirikiana na tume ua uchaguzi na polisi haziitaji hayo uliyoyasema
 
Dhalimu alijifanya anafanya kazi, dakika ya mwisho ilibidi anajisi uchaguzi ili atangazwe mshindi. Kibaya zaidi alifanya uporaji wa kishamba mpaka kila mtu akajua.
Kazi iliyofanywa na Chama Cha Mapinduzi ilikuwa ni kubwa sana na wananchi waliikubali. Baadhi ni
  1. Usambazaji wa umeme vijijini uliongezeka kutoka 16.4% mwaka 2015 hadi 67.1% mwaka 2020.
  2. Elimu bila malipo; idadi ya wanafunzi wa sekondari iliongezeka kutoka wanafunzi 1,648,359 mwaka 2015 hadi 2,185037 mwaka 2019.
  3. Vituo vya kutolea huduma za afya (zahanati, vituo vya afya na hospitali) viliongezeka kutoka 7,014 mwaka 2015 hadi 8,446 mwaka 2020.
 
Kura gani? Kama unazungumzia hili kura wazoiba Ccm kwa kushirikiana na tume ua uchaguzi na polisi haziitaji hayo uliyoyasema
Lissu na Sugu walikiri wazi kuwa uchaguzi ulienda vema na upigaji kura ulikuwa unaendelea vizuri siku husika.
Tafadhali weka vituo ambayo kulitokea hayo madai unayosema.
 

Kama hivyo ulivyotaja vinatoa kura, basi makaburu wa Afrika kusini wangekuwa madarakani mpaka leo maana walifanya mara elfu ya hayo ya ccm.
 
Lissu na Sugu walikiri wazi kuwa uchaguzi ulienda vema na upigaji kura ulikuwa unaendelea vizuri siku husika.
Tafadhali weka vituo ambayo kulitokea hayo madai unayosema.

Ule ushenzi, ukatili na uhayawani wa wazi tuliuona kwa macho yetu na wala hatuhadithiwi. Ingia kwenye tovuti ya tume ya uchaguzi kama matokeo ya ule uchafu wamethubutu kuyaweka.
 
Kama hivyo ulivyotaja vinatoa kura, basi makaburu wa Afrika kusini wangekuwa madarakani mpaka leo maana walifanya mara elfu ya hayo ya ccm.
Mkuu tofautisha CCM na makaburu. CCM ni Chama kiongozi na mfano kwa vyama vyote vya Afrika; historia yake ya kuhakisha uhuru wa Afrika Kusini na nchi nyingine inafahamika.
 
Ule ushenzi, ukatili na uhayawani wa wazi tuliuona kwa macho yetu na wala hatuhadithiwi. Ingia kwenye tovuti ya tume ya uchaguzi kama matokeo ya ule uchafu wamethubutu kuyaweka.
Tume ilitangaza na wananchi ndiyo tuliochagua.
 
Majambazi yakifarakana ni furaha kwetu, na katika mfarakano huo sisi tunajiandaa kuwapelekea moto mpaka tuwamalize wote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…