Ochu
JF-Expert Member
- May 13, 2008
- 976
- 47
Kiama cha mafisadi chafikia ukingoni
2008-10-20 11:29:33
Na Simon Mhina
Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk. Edward Hoseah, ametangaza kiama cha vigogo wanaotuhumiwa kwa rushwa kwa kusisitiza kuwa taasisi hiyo itawashukia na kuwaburuza kortini kwa kasi inayozidi ya mwewe.
Akizungumza na Nipashe katika mahojiano maalum baada ya kufunga warsha ya siku mbili iliyohusu rushwa katika chaguzi, Mkurugenzi huyo, alisema siku ya kuwaburuza vigogo hao mahakamani, imekaribia.
Alisema kama ambavyo kiama hakifahamiki kitakuja lini na kitamkuta binadamu akiwa wapi, ndivyo taasisi hiyo itakavyowadokoa mmoja baada ya mwingine, kisha kuwaburuza mahakamani.
``Kama ambavyo watu watashtukia tu baragumu au parapanda limelia na kiama kimewadia, ndivyo ambavyo vigogo hao watashtuka kujiona wapo kizimbani muda mfupi kuanzia sasa,`` alisema na kuongeza kuwa:
``Najua mna wasiwasi, lakini napenda kuwahakikishia Watanzania kupitia kwenu (vyombo vya habari) kuwa, hatuna masihara kwa jambo hili, hatuwezi kusema tutawafikisha watu mahakamani halafu tusiwafikishe...mambo yameshaiva, kesi zipo tayari watajikuta tu wapo kizimbani.``
Alipoulizwa kama kesi hizo zitafunguliwa mwezi huu au ujao, alisema kilichofanya mambo `yasilipuke` ni maandalizi ya kongamano hilo, lililoandaliwa na ofisi yake pamoja ya Msajili wa Vyama vya Siasa.
Alipohojiwa ni kwanini watuhumiwa hao washukiwe ghafla, Hosea alisema inatokana na ukweli kwamba, sheria inamzuia kuzungumzia kesi ambayo hajaifikisha mahakamani.
Hivi karibuni, Dk. Hoseah alinukuliwa akisema kwamba kuna kesi tano zinazohusu mafisadi na muda wowote wangeweza kufikishwa kortini.
Hata hivyo, zaidi ya siku 20 zimekwishapita bila taasisi anayoiongoza kufanya hivyo.
``Siwezi kutaja hapa kwamba mtu fulani amefanya hivi au vile, nitakuwa nakiuka sheria iliyounda Takukuru, hawa watafikishwa mahakamani tu, hatuwezi kutania,``alisema.
Naye Mbunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Jimbo la Maswa, John Shibuda, alisema taasisi hiyo hivi sasa inaonekana kama chafya cha mtoto mchanga, ambayo haiwezi kumuamsha baba mlevi usingizini.
Ili kuondokana na dhana hiyo, ameitaka Takukuru kuchukua hatua kali dhidi ya wala rushwa wote kwani kufanya hivyo itajisafisha kwa Watanzania.
Alisema hakubaliani na watu ambao kila mara wanaishutumu taasisi hiyo na Mkurugenzi wake, kwa vile imezingirwa na sheria mbovu.
``Takukuru inabanwa sana, wakisema wanaonekana kama chafya ya mtoto mdogo ambaye hata akipiga chafya mara tano chafya hiyo haiwezi kumuamsha usingizini baba mlevi aliyelala kitandani,``alisema na kuongeza kuwa:
``Tunaimba wimbo wa rushwa kila siku, lakini lazima tujiulize nani katufikisha hapa. Rushwa imeota mizizi kwa vile kuna viongozi wanaifuga na kuitunza kuliko familia zao.``
Naye Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba, alisema kwa sasa haihitajiki utafiti, maazimio au ngonjera yoyote kuhusu rushwa, bali kinachotakiwa ni vitendo.
``Ukisoma tafiti, sheria na mipango ya kupamba na na rushwa ni kubwa kuliko msahafu, hatuhitaji maneno maneno sasa tunataka vitendo. Tunahitaji watu wanaowachukulia hatua wala rushwa,``alisema.
Warioba, alisema kuna malalamiko ya kweli ambayo yamejitokeza kwamba wakubwa wakila rushwa, wanaundiwa tume kuchunguzwa, lakini wadogo wanapelekwa moja kwa moja polisi.
Alisema Takukuru ina nafasi ya kujisafisha juu ya tuhuma hizo kwa kuwaburuza Mahakamani wala rushwa wote bila kujali nyadhifa na uwezo wao.
* SOURCE: Nipashe
2008-10-20 11:29:33
Na Simon Mhina
Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk. Edward Hoseah, ametangaza kiama cha vigogo wanaotuhumiwa kwa rushwa kwa kusisitiza kuwa taasisi hiyo itawashukia na kuwaburuza kortini kwa kasi inayozidi ya mwewe.
Akizungumza na Nipashe katika mahojiano maalum baada ya kufunga warsha ya siku mbili iliyohusu rushwa katika chaguzi, Mkurugenzi huyo, alisema siku ya kuwaburuza vigogo hao mahakamani, imekaribia.
Alisema kama ambavyo kiama hakifahamiki kitakuja lini na kitamkuta binadamu akiwa wapi, ndivyo taasisi hiyo itakavyowadokoa mmoja baada ya mwingine, kisha kuwaburuza mahakamani.
``Kama ambavyo watu watashtukia tu baragumu au parapanda limelia na kiama kimewadia, ndivyo ambavyo vigogo hao watashtuka kujiona wapo kizimbani muda mfupi kuanzia sasa,`` alisema na kuongeza kuwa:
``Najua mna wasiwasi, lakini napenda kuwahakikishia Watanzania kupitia kwenu (vyombo vya habari) kuwa, hatuna masihara kwa jambo hili, hatuwezi kusema tutawafikisha watu mahakamani halafu tusiwafikishe...mambo yameshaiva, kesi zipo tayari watajikuta tu wapo kizimbani.``
Alipoulizwa kama kesi hizo zitafunguliwa mwezi huu au ujao, alisema kilichofanya mambo `yasilipuke` ni maandalizi ya kongamano hilo, lililoandaliwa na ofisi yake pamoja ya Msajili wa Vyama vya Siasa.
Alipohojiwa ni kwanini watuhumiwa hao washukiwe ghafla, Hosea alisema inatokana na ukweli kwamba, sheria inamzuia kuzungumzia kesi ambayo hajaifikisha mahakamani.
Hivi karibuni, Dk. Hoseah alinukuliwa akisema kwamba kuna kesi tano zinazohusu mafisadi na muda wowote wangeweza kufikishwa kortini.
Hata hivyo, zaidi ya siku 20 zimekwishapita bila taasisi anayoiongoza kufanya hivyo.
``Siwezi kutaja hapa kwamba mtu fulani amefanya hivi au vile, nitakuwa nakiuka sheria iliyounda Takukuru, hawa watafikishwa mahakamani tu, hatuwezi kutania,``alisema.
Naye Mbunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Jimbo la Maswa, John Shibuda, alisema taasisi hiyo hivi sasa inaonekana kama chafya cha mtoto mchanga, ambayo haiwezi kumuamsha baba mlevi usingizini.
Ili kuondokana na dhana hiyo, ameitaka Takukuru kuchukua hatua kali dhidi ya wala rushwa wote kwani kufanya hivyo itajisafisha kwa Watanzania.
Alisema hakubaliani na watu ambao kila mara wanaishutumu taasisi hiyo na Mkurugenzi wake, kwa vile imezingirwa na sheria mbovu.
``Takukuru inabanwa sana, wakisema wanaonekana kama chafya ya mtoto mdogo ambaye hata akipiga chafya mara tano chafya hiyo haiwezi kumuamsha usingizini baba mlevi aliyelala kitandani,``alisema na kuongeza kuwa:
``Tunaimba wimbo wa rushwa kila siku, lakini lazima tujiulize nani katufikisha hapa. Rushwa imeota mizizi kwa vile kuna viongozi wanaifuga na kuitunza kuliko familia zao.``
Naye Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba, alisema kwa sasa haihitajiki utafiti, maazimio au ngonjera yoyote kuhusu rushwa, bali kinachotakiwa ni vitendo.
``Ukisoma tafiti, sheria na mipango ya kupamba na na rushwa ni kubwa kuliko msahafu, hatuhitaji maneno maneno sasa tunataka vitendo. Tunahitaji watu wanaowachukulia hatua wala rushwa,``alisema.
Warioba, alisema kuna malalamiko ya kweli ambayo yamejitokeza kwamba wakubwa wakila rushwa, wanaundiwa tume kuchunguzwa, lakini wadogo wanapelekwa moja kwa moja polisi.
Alisema Takukuru ina nafasi ya kujisafisha juu ya tuhuma hizo kwa kuwaburuza Mahakamani wala rushwa wote bila kujali nyadhifa na uwezo wao.
* SOURCE: Nipashe