DOKEZO Kibaha kwa Mfipa kuna vibaka wanaopora na kujeruhi watu, Vyombo vya Ulinzi vikomeshe hali hii

DOKEZO Kibaha kwa Mfipa kuna vibaka wanaopora na kujeruhi watu, Vyombo vya Ulinzi vikomeshe hali hii

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Huku kwetu maeneo ya Kibaha hasa Kibaha Kwa Mfipa kuna matukio ambayo ni hatari sana kwa usalama, kwani kuna vibaka wanatusumbua na wanafanya matukio yao majira ya Saa 11 alfajiri wakiwalenga wale watu wanaodamka asubuhi mapema kwenye kwenye majukumu yao.

Vibaka hao wanakaba na kuwapora kwa kutumia mapanga Wananchi wanaopita na hata wale wanaopanda Bodaboda, tunaomba ujumbe huu ufike kwa Jeshi letu la Polisi, hao watu wanaelekea kutuzidi nguvu Wananchi na kutukosesha amani.

Wengi wao wanatumia Pikipiki huku wakiwa na silaha za jadi ikiwemo mapanga, bisibisi na marungu.

Kinachouma zaidi ni kuwa viongozi wa Serikali za Mitaa wengi nao ni kama wanaogopa kuwachukuliwa hatua watu hao, kwani ukizungumza na baadhi ya Bodaboda wema wanasema wanawajua wanaofanya matukio hayo ila hawawezi kuwataja kwa kuwa nao wanahofia usalama wao.

Hili jambo linatakiwa kuchukuliwa hatua kabla mambo hayajafika mbali na tabia kukomaa ikiwemo watu kupoteza maisha pia.
 
Sio kibaha tu, sehemu nyingi ikiwemo mbeya, sumbawanga, arusha n.k
 
Huku kwetu maeneo ya Kibaha hasa Kwa Mfipa ni hatari sana, kwani kuna vibaka wanatusumbua sana majira ya Saa 11 alfajiri.

Vibaka hao wanakaba na kuwapora kwa kutumia mapanga, tunaomba ujumbe huu ufike kwa Jeshi letu la Polisi, hao watu wanaelekea kutuzidi nguvu Wananchi na kutukosesha amani.

Wengi wao wanatumia Pikipiki huku wakiwa na silaha za jadi ikiwemo mapanga.
Orodhesheni majina kimya kimya nenda Moja kwa Moja kwa RCO kamkabidhi mpe na post code zao za makazi. Mwambie tu Hawa kuluna tunaomba mtusaidie.


Kesho tu mtaanza kuskia vijana sita wameuawa kwenye majibizano na polisi
 
Huku kwetu maeneo ya Kibaha hasa Kwa Mfipa ni hatari sana, kwani kuna vibaka wanatusumbua sana majira ya Saa 11 alfajiri.

Vibaka hao wanakaba na kuwapora kwa kutumia mapanga, tunaomba ujumbe huu ufike kwa Jeshi letu la Polisi, hao watu wanaelekea kutuzidi nguvu Wananchi na kutukosesha amani.

Wengi wao wanatumia Pikipiki huku wakiwa na silaha za jadi ikiwemo mapanga.
Hata huku Sofu kuna mtu kapigwa mapanga wiki iliopitwa na kuporwa simu...
 
Back
Top Bottom