Kibaka Ajaribu Kuchomoka na Zawadi za Harusi ya Mtoto wa Sumaye

Kibaka Ajaribu Kuchomoka na Zawadi za Harusi ya Mtoto wa Sumaye

Pdidy

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2007
Posts
57,951
Reaction score
32,619
Kibaka Ajaribu Kuchomoka na Zawadi za Harusi ya Mtoto wa Sumaye
2075494.jpg

Wananchi wenye hasira wakijaribu kumuadhibu kibaka aliyejaribu kuchomoka na zawadi za harusi ya mtoto wa SumayeMonday, May 25, 2009 4:31 AM
Katika kuonyesha kwamba vibaka wa Tanzania wanatumia mbinu mbali mbali za ajabu, kibaka mmoja aliyejifanya mgeni mualikwa katika harusi ya mtoto wa Sumaye alipewa kipigo cha nguvu baada ya kukamatwa akijaribu kuchomoka na zawadi za maharusi.Wizi katika kumbi za sherehe hasa katika hoteli kubwa jijini Dar es Salaam umezidi kushamiri kwa kasi ya ajabu.

Katika harusi ya mtoto wa Sumaye iliyofanyika jumamosi kijana mmoja ambaye alijifanya kuwa ni mmoja wa wanandugu wa waziri mkuu wa zamani Fredrick Sumaye alipata kipigo cha nguvu baada ya kukamatwa akiwa amebeba kifurushi kilicho kuwa kimejaa zawadi za maharusi akijaribu kuondoka nazo kutoka katika ukumbi wa Hoteli ya Ubungo Plazza.

Katika kumbi nyingi hivi sasa kumekuwepo na vijana wasichana kwa wavulana ambao huwa wanavalia kinadhifu na bila kujua utadhani ni miongoni mwa wageni waalikwa, na pindi unapofika wakati wa kwenda kuchukua chakula wengi wa wageni huacha simu zao na zawadi zao mezani na vibaka hutumia nafasi hiyo kuzichukua na kuondoka nazo.

Kijana huyu aliyekamatwa alikuwa tayari kishaanza kutafuta tax kwa ajili ya kuondoka na mizigo aliyoiba.

Mizigo aliyoiba ilikuwa ni zawadi za maharusi na kama angefanikiwa kutoweka nazo basi angefaidika sana maana kulikuwa na vitu vingi vya thamani sana.

Katika sakata hilo hata walinzi wa Ultimate Security hawakumshitukia kibaka huyo kwani walidhani ni miongoni mwa wahusika katika sherehe hiyo.
 
Karibu kwa picha zaidi
 

Attachments

  • 1948.jpg
    1948.jpg
    32.4 KB · Views: 217
  • 1949.jpg
    1949.jpg
    30.5 KB · Views: 224
  • 1951.jpg
    1951.jpg
    28.8 KB · Views: 214
  • 1952.jpg
    1952.jpg
    33.1 KB · Views: 218
Na mambo ya siku hizi zawadi huachwa mlangoni. Hata wanandugu au marafiki wetu tunaowaamini wanaweza kutokomea na mojawapo ya zawadi inayoonekana kuwa ya thamani. Kwani utajuaje ilikuwepo zawadi kama hiyo ikikumbukwa kwamba huambiwi aksante kwa zawadi aina.....uliyotoa. Tuwe makini.
 
Hiyo inawaonyesha sherehe za wakubwa hazina ubaguzi hata vibaka ruksa
 

Attachments

  • 1956.jpg
    1956.jpg
    26.8 KB · Views: 135
4679d1243348494-kibaka-ajaribu-kuchomoka-na-zawadi-za-harusi-ya-mtoto-wa-sumaye-1955.jpg


Namwona mzee wa Lupaso na tabasamu la nguvu! Hongera kijana kuvuta jiko
 
Mtu na shemeji yake (Yo Yo en Masa)
Oeni na nyie tuje kuwachambua hapa vimwana wenu, isije ikawa mna flatscreen hamjijui..ha ha
Hongera kwa maharusi, mwanaume karidhika na mwanamke wake mwacheni aenjoy maisha ya ndoa esp. ya awali..
 
Hivi huu ukumbi wa ubungo plaza kuukodi kwa harusi kama hivi ni kiasi gani?
 
Mtu na shemeji yake (Yo Yo en Masa)
Oeni na nyie tuje kuwachambua hapa vimwana wenu, isije ikawa mna flatscreen hamjijui..ha ha Hongera kwa maharusi, mwanaume karidhika na mwanamke wake mwacheni aenjoy maisha ya ndoa esp. ya awali..

Duu Flat Screen ...... am afraid theres no space to keep it.....labda Yo Yo!
 
Back
Top Bottom