Lady Whistledown
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,147
- 2,008
Kwa Miaka 3 Wakazi wa Kata ya Mpigi Magoe, eneo la Torino-Kibamba wanadaiwa kutumia Maji ya Visima na Madimbwi ambayo si salama kwa Afya zao, licha ya eneo hilo kupimwa Miundombinu ya kupitisha Maji.
Mkazi wa eneo hilo, Irene Makea amesema kwa Miaka Mitatu wamekuwa wakijaza fomu lakini hawaletewi maji, amesema “Tumeambiwa tukifika watu 50 tutaletewa Maji, lakini hatujaletewa. Matokeo yake tunategemea kununua lita 20 kwa Tsh. 800”
Hata hivyo, Meneja wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam ( DAWASA) wa Kibamba, Elizabeth Sankere amesema bado wanashughulikia changamoto hizo kwa kuwa Miundombinu bado haijakamilika na kuna tanki la Msongamano linaloendelea kutengenezwa.
Chanzo: Mwananchi
Mkazi wa eneo hilo, Irene Makea amesema kwa Miaka Mitatu wamekuwa wakijaza fomu lakini hawaletewi maji, amesema “Tumeambiwa tukifika watu 50 tutaletewa Maji, lakini hatujaletewa. Matokeo yake tunategemea kununua lita 20 kwa Tsh. 800”
Hata hivyo, Meneja wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam ( DAWASA) wa Kibamba, Elizabeth Sankere amesema bado wanashughulikia changamoto hizo kwa kuwa Miundombinu bado haijakamilika na kuna tanki la Msongamano linaloendelea kutengenezwa.
Chanzo: Mwananchi