Kibao cha Aziz Ally Mtoni na Historia Yake

Kibao cha Aziz Ally Mtoni na Historia Yake

Nikajua Aziz Ki Mzee wangu nisamehe bure. Lakini pia jitahidi utuletee historia ya mabingwa WA kihistoria Dar Young African. Asante baba
 
Nikajua Aziz Ki Mzee wangu nisamehe bure. Lakini pia jitahidi utuletee historia ya mabingwa WA kihistoria Dar Young African. Asante baba
The...
Niko mbali kidogo na mpira.
Sina la kusema nikafurahisha jukwaa hili.

Labda nijaribu kukumbuka yale niliyoyaona wakati wa utoto wangu kuhusu mpira:

YANGA NA SUNDERLAND UNAZI WA ZAMANI: KISA CHA MZEE MANGARA TABU NA AYUBU KIGURU

Nina rafiki yangu anaitwa Kazua leo asubuhi kanipa kisa cha Mzee Mangara Tabu na Ayubu Kiguru.

Wakati wa ujana wake Kazua alikuwa mkoba, yaani "centre half," wa Dundee United.

Leo mimi na sahib yangu Kazua akitutokea simba ghafla tumeliwa.
Miguu hainyanyuki ardhini haitaki inatukatalia sharti tuibembeleze.

Mzee Mangara Tabu alikuwa President wa Yanga na Ayubu Kiguru alikuwa shabiki mkubwa sana wa Sunderland na unaweza kusema ndiyo Haji Manara wa enzi hizo.

Haji mwanafunzi kwa Ayubu.
Ayubu alikuwa na kipaji cha ajabu.

Mtu wa vibweka lukuki.

Sunderland ikichukua kikombe asubuhi anakujanacho sokoni anakiweka mbele ya ubao wake washabiki wa Sunderland wakija sokoni wanatunza.

Hapo Ayubu kavaa jezi no. 6 ya Hamisi Kilomoni.

Jioni soko likifungwa anahesabu fedha zilizotunzwa anapeleka club Congo na Mchikichi.

Soko zima lile limejaa wanazi wa Yanga basi Ayubu peke yake anapambananao na mwisho wa siku wanasalimu amri wanafunga virago hao wanaondoka.

Ayubu alikuwa ana ubao wa biashara Kariakoo Market.
Siku hiyo Mzee Mangara kenda sokoni kununua mahitaji yake.

Ayubu kumuona Mzee Mangara akamuamkia kisha akamwambia, "Mzee Mangara kanunue hiliki tu basi. Vingine vyote vilivyobakia njoo uchukue kwangu bure."

Yanga ilikuwa imefungwa na Sunderland.
Mzee Mangara akamshukuru Ayubu kisha akamwambi, "Tutakutana Ilala Stadium."

Ayubu akamjazia vitu Mzee Mangara kwenye jumu lake, Mzee Mangara akimshukuru Ayubu akashika njia kwenda nyumbani kwake ambako hapakuwa mbali na sokoni.

Hapo chini soko la Kariakoo kama lilivyokuwa enzi hizo na Kazua ni huyo hapo picha ya mwisho.

NB: Kazua kafariki kiasi cha miezi mitatu iliyopita.
 
AZIZ ALLY MJENZI WA MISIKITI
Aziz Ally alipofariki mwaka wa 1951 muda mfupi baada ya.kutoka hijja gazeti la Tanganyika Standard katika kueleza kifo chake liliandika "Mjenzi wa Misikiti Amefariki."

Kabla hajajenga nyumba yake mashuhuri ya Mtoni leo panaitwa Mtoni kwa Aziz Ali, Azizi Ali alikuwa anaishi Gerezani Mtaa wa Congo na Mbaruku.
Haya hapo chini aliyafanya wakati akiishi Gerezani:

KUMBUKUMBU YA RAMADHANI 7: FUTARI KWA AZIZ ALI MTAA WA MBARUKU NA CONGO 1940s

Aziz Ali alikuwa tajiri na akaupamba utajiri wake kwa ukarimu.

Yeye alikuwa mjenzi wa majumba na alikuwa akimjengea mtu nyumba na akashindwa kumlipa alimpa muda alipe kwa taratibu.

Kwa wema wake huu watu wa Dar es Salaam wakampa jina la ''Aziz'' yaani ''Kipenzi.''

Lakabu hii ikaua jina lake la Ali Kidonyo akafahamika kwa jina la Aziz Ali.

Nyumbani kwake Mwezi wa Ramadhani kuanzia tarehe mosi hadi mwisho wa mfungo ikiingia magharibi watoto wake wa kiume Waziri (Dossa), Ramadhani na Hamza na watoto wa jirani walikuwa wanajumuika kufagia uwanja na kutandika majamvi kwa ajili ya watu watakokuja kufuturu barazani kwao.

Nyumba yake ilikuwa Mtaa wa Mbaruku na Congo jirani na nyumba ya babu yangu Salum Abdallah.

Miezi ya kawaida Aziz Ali nyumbani kwake ikiingia magharib mwanae Hamza alikuwa na kazi ya kuwasha karabai na kuzitawanya katika misikiti yote ya Kariakoo.

Baada ya sala ya Isha Hamza atazipitia karabai zote kuzirejesha nyumbani kwa matayarisho ya siku ya pili.

Hii ndiyo ilikuwa kazi yake Hamza Aziz na haya kanieleza mwenyewe kwa kinywa chake.

Miaka hiyo misikiti ya Kariakoo ilikuwa haina umeme.

Misikiti mingi ya Dar es Salaam ilijengwa na Aziz Ali na alipofariki Tanganyika Standard liliandika kwa wino uliokoza: ''Aziz Ali Mjenga Misikiti Amefariki.''

Aziz Ali alikataa kumpeleka mwanae mkubwa shule Dossa kuanza darasa la kwanza hadi kwanza aingie chuoni ahitimu mashafu.

Haya kanieleza mwenyewe Dossa nyumbani kwake Mlandizi mbele ya Ally Sykes.

Mzee Dossa anasema kwa ajili hii alianza darasa la kwanza akiwa na miaka 14 na ndiyo sababu yeye kusoma darasa moja na Abbas Sykes ambae kwake alikuwa mdogo kwa umri.

Akanambia na ndiyo sababu ya urafiki wake na Abbas Sykes kuwa mkubwa kuliko urafiki aliokuwanao na kaka zake Abdulwahid na Ally.

Aziz Ally alijenga jumba la fahari la vioo na vigae Mtoni na sehemu ilipo nyumba yake hii inaitwa Mtoni kwa Aziz Ali hadi leo.

Kwa miaka ile hakuna Mwafrika alikuwa na nyumba kama ile.
Nyumba mfano wa hiyo zilikuwa Oyster Bay makazi ya Wazungu.

Aziz Ally barza yake kubwa ya maongezi ilikuwa Mtaa wa Stanley na Sikukuu nyumbani kwa Kleist Sykes na ndipo lilipokuwa duka lake la vifaa vya ujenzi.

Hii ilikuwa barza maarufu ya wazee wa Dar es Salaam.
Barza hii ilififia baada ya kifo cha Kleist Sykes mwaka wa 1949.

Aziz Ali alikufa muda mfupi baada ya kutoka safari ya Hijja mwaka wa 1951.
Picha: Aziz Ali ujanani na uzeeni.

Mzee wetu wewe bahati baya upo bongo hapa ungekuwa nchi zinazojielewa huko kwa aina ya uandishi na maandiko ya kihistoria km haya ungekimbiliwa kama dhahabu.
 
Mzee wetu wewe bahati baya upo bongo hapa ungekuwa nchi zinazojielewa huko kwa aina ya uandishi na maandiko ya kihistoria km haya ungekimbiliwa kama dhahabu.
Covid...
Nimeandika na wao sana nikiwa hapa nyumbani.

Bahati mbaya mitandao imeua magazeti mengi yaliyokuwa yakichapwa London na kusambazwa huku kwetu.
 
Mzee wetu wewe bahati baya upo bongo hapa ungekuwa nchi zinazojielewa huko kwa aina ya uandishi na maandiko ya kihistoria km haya ungekimbiliwa kama dhahabu.
Covid...
Nimeandika na wao sana nikiwa hapa nyumbani.
Bahati mbaya mitandao imeua magazeti mengi yaliyokuwa yakichapwa London na kusambazwa huku kwetu.
 
The...
Niko mbali kidogo na mpira.
Sina la kusema nikafurahisha jukwaa hili.

Labda nijaribu kukumbuka yale niliyoyaona wakati wa utoto wangu kuhusu mpira:

YANGA NA SUNDERLAND UNAZI WA ZAMANI: KISA CHA MZEE MANGARA TABU NA AYUBU KIGURU

Nina rafiki yangu anaitwa Kazua leo asubuhi kanipa kisa cha Mzee Mangara Tabu na Ayubu Kiguru.

Wakati wa ujana wake Kazua alikuwa mkoba, yaani "centre half," wa Dundee United.

Leo mimi na sahib yangu Kazua akitutokea simba ghafla tumeliwa.
Miguu hainyanyuki ardhini haitaki inatukatalia sharti tuibembeleze.

Mzee Mangara Tabu alikuwa President wa Yanga na Ayubu Kiguru alikuwa shabiki mkubwa sana wa Sunderland na unaweza kusema ndiyo Haji Manara wa enzi hizo.

Haji mwanafunzi kwa Ayubu.
Ayubu alikuwa na kipaji cha ajabu.

Mtu wa vibweka lukuki.

Sunderland ikichukua kikombe asubuhi anakujanacho sokoni anakiweka mbele ya ubao wake washabiki wa Sunderland wakija sokoni wanatunza.

Hapo Ayubu kavaa jezi no. 6 ya Hamisi Kilomoni.

Jioni soko likifungwa anahesabu fedha zilizotunzwa anapeleka club Congo na Mchikichi.

Soko zima lile limejaa wanazi wa Yanga basi Ayubu peke yake anapambananao na mwisho wa siku wanasalimu amri wanafunga virago hao wanaondoka.

Ayubu alikuwa ana ubao wa biashara Kariakoo Market.
Siku hiyo Mzee Mangara kenda sokoni kununua mahitaji yake.

Ayubu kumuona Mzee Mangara akamuamkia kisha akamwambia, "Mzee Mangara kanunue hiliki tu basi. Vingine vyote vilivyobakia njoo uchukue kwangu bure."

Yanga ilikuwa imefungwa na Sunderland.
Mzee Mangara akamshukuru Ayubu kisha akamwambi, "Tutakutana Ilala Stadium."

Ayubu akamjazia vitu Mzee Mangara kwenye jumu lake, Mzee Mangara akimshukuru Ayubu akashika njia kwenda nyumbani kwake ambako hapakuwa mbali na sokoni.

Hapo chini soko la Kariakoo kama lilivyokuwa enzi hizo na Kazua ni huyo hapo picha ya mwisho.

NB: Kazua kafariki kiasi cha miezi mitatu iliyopita.
Heshima kubwa Sana Kwako Baba yetu,Mzee wetu ndugu Mohamed said.
Wewe ni hazina kubwa kwetu Sisi vijana. Natamani kuwa kama wewe but my potentials are limited to poverty. Live long babaa
 
The...
Niko mbali kidogo na mpira.
Sina la kusema nikafurahisha jukwaa hili.

Labda nijaribu kukumbuka yale niliyoyaona wakati wa utoto wangu kuhusu mpira:

YANGA NA SUNDERLAND UNAZI WA ZAMANI: KISA CHA MZEE MANGARA TABU NA AYUBU KIGURU

Nina rafiki yangu anaitwa Kazua leo asubuhi kanipa kisa cha Mzee Mangara Tabu na Ayubu Kiguru.

Wakati wa ujana wake Kazua alikuwa mkoba, yaani "centre half," wa Dundee United.

Leo mimi na sahib yangu Kazua akitutokea simba ghafla tumeliwa.
Miguu hainyanyuki ardhini haitaki inatukatalia sharti tuibembeleze.

Mzee Mangara Tabu alikuwa President wa Yanga na Ayubu Kiguru alikuwa shabiki mkubwa sana wa Sunderland na unaweza kusema ndiyo Haji Manara wa enzi hizo.

Haji mwanafunzi kwa Ayubu.
Ayubu alikuwa na kipaji cha ajabu.

Mtu wa vibweka lukuki.

Sunderland ikichukua kikombe asubuhi anakujanacho sokoni anakiweka mbele ya ubao wake washabiki wa Sunderland wakija sokoni wanatunza.

Hapo Ayubu kavaa jezi no. 6 ya Hamisi Kilomoni.

Jioni soko likifungwa anahesabu fedha zilizotunzwa anapeleka club Congo na Mchikichi.

Soko zima lile limejaa wanazi wa Yanga basi Ayubu peke yake anapambananao na mwisho wa siku wanasalimu amri wanafunga virago hao wanaondoka.

Ayubu alikuwa ana ubao wa biashara Kariakoo Market.
Siku hiyo Mzee Mangara kenda sokoni kununua mahitaji yake.

Ayubu kumuona Mzee Mangara akamuamkia kisha akamwambia, "Mzee Mangara kanunue hiliki tu basi. Vingine vyote vilivyobakia njoo uchukue kwangu bure."

Yanga ilikuwa imefungwa na Sunderland.
Mzee Mangara akamshukuru Ayubu kisha akamwambi, "Tutakutana Ilala Stadium."

Ayubu akamjazia vitu Mzee Mangara kwenye jumu lake, Mzee Mangara akimshukuru Ayubu akashika njia kwenda nyumbani kwake ambako hapakuwa mbali na sokoni.

Hapo chini soko la Kariakoo kama lilivyokuwa enzi hizo na Kazua ni huyo hapo picha ya mwisho.

NB: Kazua kafariki kiasi cha miezi mitatu iliyopita.
Heshima kubwa Sana Kwako Baba yetu,Mzee wetu ndugu Mohamed said.
Wewe ni hazina kubwa kwetu Sisi vijana. Natamani kuwa kama wewe but my potentials are limited to poverty. Live long babaa
 
Heshima kubwa Sana Kwako Baba yetu,Mzee wetu ndugu Mohamed said.
Wewe ni hazina kubwa kwetu Sisi vijana. Natamani kuwa kama wewe but my potentials are limited to poverty. Live long babaa
The...
Sote ni masikini lakini huo umasikini ndiyo uwe kichocheo cha kutusukuma tusonge mbele.
 
Back
Top Bottom