Kibu Denis anapaswa kulaaniwa na kila mpenda soka

Kibu Denis anapaswa kulaaniwa na kila mpenda soka

PakiJinja

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2012
Posts
11,689
Reaction score
25,848
Bila ya kujalisha upo timu gani, bila kujali ni wakina nani waliopo nyuma ya Kibu Denis, wapenda soka wote wanapaswa kumlaani kwa alichowafanyia Simba.

Simba wamemtoa Kibu huko walipomtoa, wakampambania katika changamoto alizozipitia, wakampa nafasi lakini hakuwapa chochote cha maana zaidi ya kuifunga Yanga, Simba wakasimama naye, wakamuimba na akaimbika.

Striker, aliyeimbwa na kutegemewa na akapewa kila mechi lakini mwisho akaumaliza msimu kwa kuifungia Simba goli moja tu, lakini bado Simba waliendelea kumuamini, wakamuimba, wakawa tayari kumrekebishia maslahi yake, lakini akawaanzishia vituko vya kipumbavu kabisa na mwishowe akawatoroka.

Mpira wa Tanzania unazidi kukua na kupewa heshima, kadili unavyokua inapaswa wachezaji wajifunze sana kuhusu elimu ya mikataba, pia wajitambue kuwa wao ni wadau muhimu sana na upumbavu wao unaligharimu soka la Tanzania pakubwa na huenda ikapelekea lirudi likikokuwa.

Simba inafahamika kwa jinsi ilivyo na ushirikiano pale wachezaji wake wanapopata malisho mapya nje, huwa haiwang’ang’anii. Kuna wakati Simba huonekana kama Soca Academy badala ya Professional footbal club sababu tu wakati wowote wachezaji wake wakionekana huko nje huwa ipo tayari kuhatarisha mipango yake na kuruhusu wachezaji kuondoka.

Angekuwa ni Chama amewafanyia haya ningemuelewa, lakini siyo Kibu Denis.

Soma=> Kibu kuisumbua Simba, Taswira mbaya kwa timu
 
Mpira wetu unaongozwa na busara,maswala ya sheria na kanuni za usajili kwetu sio muhimu.Inabidi Mama kizimkazi aingilie Kibu hana furaha kabisa.
 
Bila ya kujalisha upo timu gani, bila kujali ni wakina nani waliopo nyuma ya Kibu Denis, wapenda soka wote wanapaswa kumlaani kwa alichowafanyia Simba.

Simba wamemtoa Kibu huko walipomtoa, wakampania katika changamoto alizozipitia, wakampa nafasi lakini hakuwapa chochote cha maana zaidi ya kuifunga Yanga, Simba wakasimama naye, wakamuimba na akaimbika.

Striker, aliyeimbwa na kutegemewa na akapewa kila mechi lakini mwisho wa akaumaliza msimu kwa kuifungia Simba goli moja tu, lakini bado Simba waliendelea kumuamini, wakamuimba, wakawa tayari kumrekebishia maslahi yake, lakini akawaanzishia vituko vya kipumbavu kabisa na meishowe akawatoroka.

Mpira wa Tanzania unazidi kukua na kupewa heshima, kadili unavyokua inapaswa wachezaji wajifunze sana kuhusu elimu ya mikataba, pia wajitambue kuwa wao ni wadau muhimu sana na upumbavu wao unaligharimu soka la Tanzania pakubwa na huenda ikapelekea lirudi likikokuwa.

Simba inafahamika kwa jinsi ilivyo na ushirikiano pale wachezaji wake wanapopata malisho mapya nje, huwa haiwang’ang’anii. Kuna wakati Simba huonekana kama Soca Academy badala ya Professional footbal club sababu tu wakati wowote wachezaji wake wakionekana huwa ipo tayari kuhatarisha mipsngo yake na kuruhusu wachezaji kuindoka.

Angekiwa ni Chama amewafanyia haya ningemuelewa, lakini siyo Kibu Denis.

Soma=> Kibu kuisumbua Simba, Taswira mbaya kwa timu

Acha ujinga futa hii. Utamlishia wewe watoto wake?
 
Mpira wetu unaongozwa na busara,maswala ya sheria na kanuni za usajili kwetu sio muhimu.Inabidi Mama kizimkazi aingilie Kibu hana furaha kabisa.
Arudi kwao Burundi alileta dharau kwenda Timu ya Taifa hana hata shukurani amepewa uraia kwa sababu ya mpira .
 
Acha ujinga futa hii. Utamlishia wewe watoto wake?
Kwa hiyo ili kuilisha familia yake anatakiwa ku abuse makubaliano?
Wakati Simba wanamuokota kabla ya kumpatia maisha mazuri alikuwa anawalisha nini?
Kwa hiyo eatoto wake wanayakiwa kulishwa kihuni? Angewaaga Simba angepungukiwa kitu gani?
 
Ahmedy amesema kibu ni kijana wao mwenye nidhamu!
Mpaka nguvu zikaniishia
 
Kwa hiyo ili kuilisha familia yake anatakiwa ku abuse makubaliano?
Wakati Simba wanamuokota kabla ya kumpatia maisha mazuri alikuwa anawalisha nini?
Kwa hiyo eatoto wake wanayakiwa kulishwa kihuni? Angewaaga Simba angepungukiwa kitu gani?

Wewe toa ushabiki. Maslahi binafsi hutangulia kuliko chochote. Kazini kwako wewe huenda ushaacha kihuni tu kisa umepata kibarua kinacholipa zaidi.
 
Baada ya mechi tano za ligi mtajikuta mnaanza kumuomba radhi 😀😀.......mnachonifurahisha mnadai hata kama hafungi ana mikimbio mizuri kiwanjani
 
Baada ya mechi tano za ligi mtajikuta mnaanza kumuomba radhi 😀😀.......mnachonifurahisha mnadai hata kama hafungi ana mikimbio mizuri kiwanjani
Na ndiyo hiyo hiyo iliwafanya mumtamani hadi kumuingiza chaka mrundi wa watu, watu wabaya sana nyie sasa mnamcheka ujinga tu.
 
Bila ya kujalisha upo timu gani, bila kujali ni wakina nani waliopo nyuma ya Kibu Denis, wapenda soka wote wanapaswa kumlaani kwa alichowafanyia Simba.

Simba wamemtoa Kibu huko walipomtoa, wakampania katika changamoto alizozipitia, wakampa nafasi lakini hakuwapa chochote cha maana zaidi ya kuifunga Yanga, Simba wakasimama naye, wakamuimba na akaimbika.

Striker, aliyeimbwa na kutegemewa na akapewa kila mechi lakini mwisho wa akaumaliza msimu kwa kuifungia Simba goli moja tu, lakini bado Simba waliendelea kumuamini, wakamuimba, wakawa tayari kumrekebishia maslahi yake, lakini akawaanzishia vituko vya kipumbavu kabisa na meishowe akawatoroka.

Mpira wa Tanzania unazidi kukua na kupewa heshima, kadili unavyokua inapaswa wachezaji wajifunze sana kuhusu elimu ya mikataba, pia wajitambue kuwa wao ni wadau muhimu sana na upumbavu wao unaligharimu soka la Tanzania pakubwa na huenda ikapelekea lirudi likikokuwa.

Simba inafahamika kwa jinsi ilivyo na ushirikiano pale wachezaji wake wanapopata malisho mapya nje, huwa haiwang’ang’anii. Kuna wakati Simba huonekana kama Soca Academy badala ya Professional footbal club sababu tu wakati wowote wachezaji wake wakionekana huwa ipo tayari kuhatarisha mipsngo yake na kuruhusu wachezaji kuindoka.

Angekiwa ni Chama amewafanyia haya ningemuelewa, lakini siyo Kibu Denis.

Soma=> Kibu kuisumbua Simba, Taswira mbaya kwa timu
Msimsagie Kunguni kwa Uhamiaji, atanyanganywa uraia wake wa kupewa.
Huyu M'bemba wa Kalemia ameota mapembe.
 
Back
Top Bottom