The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 896
- 1,427
Idadi ya watahiniwa wanaotarajiwa kufanya mtihani wa kuhitimu kidato cha nne mwaka 2024 kuanzia kesho Novemba 11, 2024 imepungua kutoka 572, 338 mwaka 2023 hadi kufikia 557, 731 mwaka huu.
Akitoa taarifa ya maandalizi ya mtihani huo, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) Dkt. Said Mohamed amesema katika idadi hiyo wavulana ni 250, 562 na wasichana ni 278, 759.
Amesema maandalizi yote kwa ajili ya mtihani huo yamekamilika kwa Tanzania Bara na Zanzibar, katika vituo vyote ambavyo ni pamoja na shule za sekondari 5, 585 na 961 kwa watahiniwa wa kujitegemea.
Kadhalika NECTA imeonya kuchukua hatua kali za kisheria kwa wanafunzi pamoja na shule zitazobainika kuwa na viashria vya udanganyifu.
Soma pia:Wanafunzi 572,338 kuanza Mtihani wa Kidato cha 4 leo
Akitoa taarifa ya maandalizi ya mtihani huo, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) Dkt. Said Mohamed amesema katika idadi hiyo wavulana ni 250, 562 na wasichana ni 278, 759.
Amesema maandalizi yote kwa ajili ya mtihani huo yamekamilika kwa Tanzania Bara na Zanzibar, katika vituo vyote ambavyo ni pamoja na shule za sekondari 5, 585 na 961 kwa watahiniwa wa kujitegemea.
Kadhalika NECTA imeonya kuchukua hatua kali za kisheria kwa wanafunzi pamoja na shule zitazobainika kuwa na viashria vya udanganyifu.
Soma pia:Wanafunzi 572,338 kuanza Mtihani wa Kidato cha 4 leo