Kidumu Chama cha Mapinduzi-zife fikra na vizazi

Kidumu Chama cha Mapinduzi-zife fikra na vizazi

escapee

Senior Member
Joined
Feb 1, 2020
Posts
175
Reaction score
302
Chama cha mapinduzi kimejengwa katika misingi ya Utu na Uzalendo,toka kuasisiwa kwake. Look
Dunia ya sasa, Geopolitics na mienendo ya dunia inahitaji kila taifa kujiimarisha haswa ktk uchumi,siasa na elimu(intelligence)

Taifa lolote ili liweze kutekeleza hayo linahitaji mkuu wa nchi aliye imara. Atakaye simamia uwajibikaji wa mifumo yote ktk kutekeleza majukumu ya kujenga taifa.

Kwa bahati mbaya viongozi wengi wa CCM wamepoteza mwelekeo na uzalendo wao siyo wa vitendo,wao kazi yao ni kumtukuza rais tu! Kila rais ashikaye madaraka wimbo ni hakuna kama yeye.

Sera za CCM ni thabiti ila wafuasi wao sasa! Ndiyo hao kila mmoja kama Luca si mshamba.

SAMIA:
Leo kalalama kinyama !! utasema rais si ndiye huyu….

Sasa! alivyo lipuka leo ndivo alipaswa kuwalipukia watendaji na wateule wake ,wanaoshindwa kutekeleza majukumu yao. Ndivyo alivopaswa kuwalipukia mafisadi,wala rushwa na viongozi wazembe. Ndivo alipaswa kuwa mkali ktk kutetea rasiliamali za taifa.Watu wanalalamika dhidi ya mauaji…yeye kakerwa na wanao lalamika na si yale mauaji. Anadai eti kwa nini hawakupaza sauti kwa mauaji mengine? ni vema atambue kuwa huo ndiyo mwanzo wa kupaza sauti kwa mauaji yanayoendelea. Na si kwa sababu ya Ali Kibao.

Duniani kote ni kweli uhalifu na mauaji hutokea….lakini washukiwa hukamatwa!

Sasa yeye anawachimba mkwara watasha….ambao hawana cha kupoteza,yaani ukali na hasira zake ni kuwabwekea mwewe! Alafu wala rushwa,ufisadi na uwajibikaji mbovu “hilo tukalitazame”
Rangi aliyo ionesha leo ndiyo iwe uwajibikaji wake ktk kuwatetea wanae wa kitanzania.
Aiseee! aya bwana… kwa sauti ya unyonge “kidumu chama cha mapinduzi”
 
Back
Top Bottom