Kiepe kimeisha, faida 10! Nakosea wapi?

Biashara ya chipsi inalipa ukiwa eneo ambalo unaweza kuuza walau gunia 2 kwa siku vinginevyo ni moja kati ya biashara pasua kichwa.
Aise! Hii yako ni point ya kuizingatia sana. Kijana wangu kasukuma siku6 kumaliza kigunia cha ndoo 4 na kishtobe, mweh!
Nadhan ndo tatizo lilipo, mzunguko mdogo
 
Hapana. Sio elf 10 kwa siku. Hii elf kumi ni baada ya kuuza chips kwa siku 6. Ni kile kigunia kidogo cha nadhan ndoo nne na ushee cha viaz
Nahisi unaibiwa siku sita 10 tu?
 
Mkuu samahani naomba uniambie maxmum ulianza na mtaji wa kiasi gani na maeneo ni yapi mazuri ya kuanzisha biashara hiyo.
Kweli jamani hili suala la muhimu sana kwamba mtaji wa kiasi gani wa kuanza kufungua banda la chips nzuri sanaa
 
Hhaaaa vident hapana boss, ila labda kwa vile nachomoa hela kidogo ya msos, sasa jee nisile ili tu nipate faida?
Hahaha mkuu hilo swali lako ulivyoliuliza duh!hahah.
 
Kweli jamani hili suala la muhimu sana kwamba mtaji wa kiasi gani wa kuanza kufungua banda la chips nzuri sanaa
Mkuu, mtaji ni 1 Mil. Hyo ni aggregate ikijumuisha kodi ya frame na vitendea kazi ila nimeanza na viazi nusu gunia la 50, 000/- ili kucheck upepo. Tatizo ndo hapo sasa hicho kigunia kinachukua 6 days kuisha
 
Mkuu samahani naomba uniambie maxmum ulianza na mtaji wa kiasi gani na maeneo ni yapi mazuri ya kuanzisha biashara hiyo.
1Mil mkuu. Inajumuisha na pango ya space ya biashara
 
Mkuu kazi yako inaku-keep busy sana?

Kama unaweza pata muda kaa nao vijana chupi-tako uone hasa kama kuna faida au laa
 
Mkuu, mtaji ni 1 Mil. Hyo ni aggregate ikijumuisha kodi ya frame na vitendea kazi ila nimeanza na viazi nusu gunia la 50, 000/- ili kucheck upepo. Tatizo ndo hapo sasa hicho kigunia kinachukua 6 days kuisha
Mtaji huo kwa faida ya bei gani Kwa siku
 
Hapana. Sio elf 10 kwa siku. Hii elf kumi ni baada ya kuuza chips kwa siku 6. Ni kile kigunia kidogo cha nadhan ndoo nne na ushee cha viaz
Umenyaji, kama unavichimba sana viazi, pia upimaji (kama unajaza sana), ...! Hizi zaweza kuwa sababu za kupungua faida.
 
Ongezea vikorokoro ukuze wateja wako.

Weka huduma ya

1. mihogo ya kukaanga kuanzia kipimo cha sh 500+
Nb: iwekee maujanja ya ukwaju,Chilli na chachandu.

2. Ndizi mshale za kukaanga na kuchoma.
-kipimo kuanzia sh.500+
Nb: chachanda&chilli/tomato ni muhimu.

3.Mishkaki ya kukaanga ya Bei chee.
Hapa unachoma mishkaki ya miwili/tsh.500 kwa ajili ya watu kurefresh.

Unakata vipande vidogo vidogo sana angalau vitatu kila stick.

Mishkaki wengi sahv hawauzi/hawanunui kutokana na Bei kubwa ya nyama,

Ila wewe ikate vipande vidg vidg uweze kuteka soko LA mishkaki.

Kila mwenye senti from sh.200 aweze kufurahisha tu mdomo.

NB: Usisahau pilipili,chachandu

Aisee,utapiga sana ela.
Hizi menu sahv, sahv zNAPENDWA SANA SKUHIZI.

Hata sisi tusiopenda kula chips, tunajua tukipita kwa flan kuna kitu tofauti tutapata.

KUNA MPWA WANGU ANAFANYA HII BIASHARA YA CHIPS KWA STYLE HIYO.

KIUKWELI,
NAONA JINSI ANAVOJAZA UMATI PALE KIMARA
 
Aisee ume eleza mambo mazuri huyo mpwa wako yupo kimara maeneo gani niende mwenyewe au niwa tume vijana wangu akawape shule ya kutengeneza chachandu ya ukwaju..
 
Goli bado watu hawajalizoea.
Banda la chips lina hitaji mwaka ndio uone matunda, au utoe huduma nzuri zaidi ya wenzio kwa gharama ileile
 
Mkuu kazi yako inaku-keep busy sana?
Kama unaweza pata muda kaa nao vijana chupi-tako uone hasa kama kuna faida au laa
Hheheh 'chupi-tako' daaaaah... mkuu sina waswas na kijana kwan uangaliz ni wa kiwango cha juu
 

Nimewahi kuwekeza ktk hii biashara nikiwa na rafiki yangu na baada ya mda fulani tuligundua tulimweka kuuza alikua akipiga hela ....
 

Neno lenye hadhi juu ya mchanganuo wako huu ni "ahsante"
 
Reactions: Cyb
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…