Sikiliza nikwambie mimi ni mtumiaji mmojawapo wa kifaa hiko, hivyo vinauzwa kulingana na namba ya kifaa alichoandikiwa. Mimi mfano nilinunua kifaa cha shilingi 360000 kwa kimoja, viwili ni 720000. Ukiwa na tatizo kubwa unapewa namba kubwa zaidi, gharama pia inapanda.
Duka lake lipo Upanga ukiwa unafuata njia iendayo Muhimbili hospital kutoka makutano ya barabara jirani na shule ya msingi Muhimbili. Utakutana na njia panda jirani na Temple, ingia kulia hadi ufike jengo la Richmond tower. Hapo ulizia duka liitwalo Hear well, utaoneshwa.
Tahadhari(ukiona haina tija si lazima uichukue)
Vifaa vile haviondoi tatizo bali vinazidisha tatizo kama anao uwezo wa kusikia kidogo na si ubovu kabisa. Nakushauri usimwache akatumia, vinaharibu masikio. Vinavuta sauti kwa ulazima lakini siyo clear sound, halafu vinavuta kila aina ya sauti sehemu yenye sauti zaidi ya moja lazima atapata tabu.