Kifo cha Al Baghdad - De javu

Kiongozi ninacho fanya ni utafiti binafsi, ndiyo maana kwenye kazi zangu nyingi utaoana naweka vyanzo vya taarifa ambacho ndicho kitu muhimu kwenye kazi yoyote ya kitafiti, na vyanzo ninavyo weka nahakikisha ni vya uhakika,wewe sasa msomaji kama inakuap mushkeli inabidi uje na hoja zako pia useme hichi si kweli kwa sababu kadha, kadha, hichi ndicho kwa sababu hii na hii, vinginevyo itakuwa ni maoni binfsi tu.
 
Kuna watu wanasinzia bila Kulala aisee, kwahyi hakufa? Unaota
“Those who are able to see beyond the shadows and lies of their culture will never be understood, let alone believed, by the masses.”

― Plato
 
Unaujuaje uhakika wa hivyo vyanzo ?

Ushawahi kusoma namna ya uhakiki wa habari kwa mujibu wa Uislamu ?
 
Unawatambuaje hao vijana wanao jiita "New Salafism", kwamba wanajiita au wanaitwa hivyo "New Salafism" ?

Hapa nataka kujua,ya kuwa hao ISIS ndio wanatumia sana "Kuniya" si ndio maana yake au imekaaje hii ?
Unaujuaje uhakika wa hivyo vyanzo ?

Ushawahi kusoma namna ya uhakiki wa habari kwa mujibu wa Uislamu ?
Sajafaham swali lako lina lenga nini hasa, lakini kuweka mambo sawa na kurahisisha jambo ni wewe kusema au kuja na hoja kuwa hichi unacho sema si sahihi, kwa mujibu wa hichi na hichi hili si sawa, halafu mimi sasa ni kanushe kwa hoja au nikubaliane na ushahidi wako. Vinginevyo utakuwa unaniambia nikuthibitishie kitu ambacho nakikubali ni sahihi, matokeo yake kutakuwa na mlolongo wa maswali yasiyo isha yanaho hitaji ufafanuzi wa kila nukta. Basi leta ushahidi wako kupinga hili, na nadhani hiyo ndiyo lugha ya Quran, kitu kinapingwa na hoja, na ndivyo wanavyo fanya wasomi, hoja kwa hoja.
 
Hili no fanya liko sahihi,na wewe unatakiwa kunikinaisha kwa majibu,ndio maana nina hoji.

Unalolitaka kwangu ndio ambalo ulitakiwa wewe ulifanye kabla ya kiandika haya yaani kwenye huu uzi wako.

Si unakubali ya kuwa kila kitu kipowazi ndio maana naona unaweka kauli nyingi sana za Wanafalsafa wa kale wa Magharibi. Kwa maana hata katika kuujia ukweli kuna waliokutangulia katika hilo. Unaposema unalo ona wewe kuwa ni ukweli au sahihi,ndio ujibu hayo maswali na kuthibitisha ya kuwa ni sahihi kwa misingi hiyo inayokufanya ujue kwamba hayi ni sahihi,ili ndio lengo langu.

Sababu haya umesema unayaona kuwa ni sahihi kwahiyo ni wajibu wako kutuonyesha usahihi huo huku ukiwa unaulizwa maswali na kuyajibu kielimu.

Au nakosea kaka,kama nakosea niambie.
 
Sanamu itatiwa pumzi nayo itapata uhai na watu wote wataambiwa waiabudu.

Taifa kusafiri kwenda kupigana na taifa ambalo hawapakani kimipaka si jambo rahisi sana wataishia tu kufungiana balozi.
Panahitajika ushahidi kwamba taifa fulani limekuchokoza ili ikiwezekana muingie vitani. Kwahiyo njia rahisi ni kumuandaa mtu au kikundi cha watu na kukiweka katika taifa unalotaka kulipiga kisha unaingia kwa gia ya kukisambaratisha kikundi hicho hapo sasa haitajarisha umeharibu miundo mbinu ya watu kwa kiasi gani na mwenye taifa akikuzuia atakuwa amekubali kuwa kile ni kikundi chake.

Uongo=sanamu inatiwa pumzi na kuwa kiumbe hai= ukweli na watu wote tunatakiwa tuuabudu=tuukubali.

Usipo ukubali unauwawa.
 
sio kweli magaidi wapo chief sema wazungu wanatumia mwanya huo kuingiza humo interest zao. magaid ni watu wanaolalamikia mambo flan flan wanayodai ni haki yao na yasipotekelezwa hulazimisha. kwa mfano yule mtoto wa mberesero aliyekamatiwa kenya kule mombasa al shabaab walivyoenda kuua wanafunz huwez kuniambia et ni zao la wamarekan. ni kama vile unavyomuona sheikh ponda na madi yake tu akipata sapot anaanzisha nae ya kwake so usitudanganye. waarabu wanaposhindwa kutatua changamoto zao husingizia wazungu. na wazungu wanatumia mwanya huo kuwaibia.
 
Magaidi wapo, wa kila aina na namna, inategemea 'nani anamwita nani' kuwa ni gaidi, Mandela aliitwa gaidi na makaburu. Gaidi ambaye nasema hayupo ni gaini ambaye anatekeleza shambulizi kama la 9/11. waste gate, anashambulia majeshi ya marekani na kuchukua silaha zao, anateka wanawake wa kijiji kizima na msururu wa magari karibu 200 na haonekani kwenye satelaiti, na mengine kama hayo, huyo gaidi hayupo. Huyo 'ghost' gaidi ni project ambayo inaelekea tamati. Kama huku ng'amua tangu shambulio la 1994 kwenye Embassy mbili za Marekani hapa Afrika mashariki kwamba ile ilikuwa ni project up to now, I wonder where will you stand as the files for the coming project are put on order.
 
Unajua kama ninge andika toka, kichwani kwangu bila reference yoyote, hapo ungekuwa sahihi kuniambia nifanye hivyo, lakini reference zipo, na hapa kwenye huu uzi ni sehemu ndogo sana ya hadithi yote, ni kama 'tip of iceberg', mada nzima sasa, ya suala la hii 'project' inayo itwa ugaidi, tangu inazaliwa, makusudio yake, na mwisho wake ni upi, kuna uzi mrefu sana kaucheki kwenye blogi yangu,na pitia posti hizi, moja baada ya nyingine, pitia na reference zake moja baada ya nyingine, halafu sasa leta hoja zako.
Kanusha hayo maelezo, lakini kwa ushahidi kama mimi nilivyo yathibitisha kwa ushahidi.
Kanusha hivyo vyanzo kwamba labda ni feki, au vya kughushi, au vimeelemea upande mmoja kwa kutoa hoja.
Eleza upande wako wa habari na weka ushahidi.
Hivyo ndivyo mijadala inavyo fanyika.

Pitia paper nzima hapa.
1 - USICHO KIFAHAMU KUHUSIANA NA VITA DHIDI YA UGAIDI Pt 1
2 - USICHO KIJUA KUHUSU VITA DHIDI YA UGAIDI NA UISLAM Pt 2
3 - USICHO KIJUA KUHUSU VITA DHIDI YA UGAIDI NA UISLAM Pt 3
4 - USICHO KIJUA KUHUSU VITA DHIDI YA UGAIDI NA UISLAM Pt 4
 
Uislamu unakufundisha hivi kaka ?
Inanibidi nifute hicho nilicho andika kuhusu 'kupata elimu kwenye kivywa cha mbwa', naendela kupekua makabrasha yangu, na kuzungumza na watu, maana maandishi halisi ya hichi nilicho sema juu ya 'mbwa', si nayo, napenda kusimamia kile ambacho ninacho ushahidi nacho, hivyo hilo nalifuta mpaka nitakapo pata uhakika nalo. Shukran.
 
Safi kabisa,lifanyie kazi hilo.

Tuko pamoja.
 
Mwambie asome upya na mahali ambapo hajaelewa umueleweshe, nadhani ka jump into conclusion

 
Unaweza ukawa haupo Tanzania alafu upo Oman nguvu ya CIA bado hujaiona huko ilivyo tamalaki?
Wala sina shaka na uwezo wa nguvu zao ila pia nna shaka nao kama bina adam hua wanakosea ndio maana yangu

Walituaminisha IRAQ kuna silaha za sumu wakakosa

Osama walituaminisha kafa zaidi ya mara moja

Huyu baghdad cjui ndio mpuuzi gan hii zaidi ya mara mia cjui anakfa na kufuuka


Jamaa wanajua ila pia wanakosea wao sio kila ki2
 
Yaani wewe una ujua mchezo kuliko wanao ucheza?
Usituchoshe na hekaya za abunuasi mkuu
 
Yaani wewe una ujua mchezo kuliko wanao ucheza?
Usituchoshe na hekaya za abunuasi mkuu
“Those who are able to see beyond the shadows and lies of their culture will never be understood, let alone believed, by the masses.”

― Plato
 
Baghdad hayupo tena.
Osama na mtoto wake hawapo tena.
Huyu ni Trump nadhani unawajua Republicans vizuri hawabahatishi.

CIA wako kila mahala hata ndugu yako wa damu au rais wako anaweza kuwa anawafanyia kazi CIA na usiwahi kujua!
Swala sio kujua kama ndugu yang CIA Wala nn anaweza akawa TISS 2 Na nisijue

Ila cha msingi nikwamba mpaka wao pia wana false flag

Ama wanakosea hamna ki2 duniani kiko perfect kwa 100%

Japo jamaa wanazifanza kazi zao kwa uweledi mkubwa sana + Ufanisi Wahali Zajuu Mnooo
 
Unaonyesha wazi ya kuwa hujamuelewa mtoa mada. Mtoa mada hakatai ya kuwa Baghdad hajafa,anajua kweli amekufa ila sio hivi karibuni kama tulivyotangaziwa.

Mimi tu kuna swali moja tu ambalo nataka kumuuliza mtoa mada.
mtoa mada hoja yake inafutiliwa mbali na tangazo la Isis kutangaza mrithi wa baghdad kwa nini wasimtangaze mapema ?
 
Atakuelewa wapi jamaa na kazi yake kuburuzwa tu. Huyo ni "Dont ask just believe"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…