Kifo cha Kanumba: Ni uzembe tu? Sio Lulu!

Kifo cha Kanumba: Ni uzembe tu? Sio Lulu!

Wabe, to be honest, binti yangu ni 18!, namshukuru Mungu, japo mimi ni binadamu, nimeumbwa na tamaa, hata kuwafakiria watoto wa Chuo, I've never!, itakuwa hivi vibinti!. Nimepiga UDSM, miaka 4, with single room Block F pale Mabibo hostel, na hiyo room yangu ndio was the one and only iliokuwa na net!, mabinti walipishana na wengine wali kill ningt,na sikuwahi hata kuwawazia, itakuwa haka!.

Simaanishi mimi ni malaika, labda ungezungumzia wa "mamas" hapo labda tungeelewana!.

Kiukweli msiba wa Kanumba umenigusa jinsi alivyo "gone too soon in such a manner" lakini serious concern yangu kwa sasa ni haka kabinti. Kupitia blog ya Sinta, ndio nemesoma kalitoka kama kalivyozaliwa with bruises all over her face!. Kutokana na mapenzi kwa Kanumba, very few gives a dam what really happened!.

I am with you!!! utani tu unaendelea...nani aliyemkamilifu asiyevutwa na uzuri wa Lulu?? hata mimi nimo

ila haka kabinti kana vuna kalichopanda......mimi sikaonei huruma hata chembe..honestly
 
Uwiiiiiiiiiiiii, toba!! Lakini uwongo mbaya, kabinti kanavutia aisee!!!
Sasa hebu nijuze, unachotaka kusema ni kwamba, kitakachofuata kwa Pasco ni kuomba kazi ya ubwana jela au ataanzisha documentary ya magereza yetu?!
NazDaz, kinachofuata ni mimi kufanya petition niwe registered nitoe msaada wa kisheria nisaidie watu kama hawa!. Kama brother Ditto (rip) aliyafanya aliyoyafanya na akapewa dhamana, wako mamia kwa maelfu wanaoozea jela kwa kukosa huduma hizi. Ukiimagine haka kabinti kalivyo na akili za ki 'wema sepetu", halafu ukawafikiria wana jela wetu!, kanahitaji serious rescue efforts soonest!.
 
NazDaz, kinachofuata ni mimi kufanya petition niwe registered nitoe msaada wa kisheria nisaidie watu kama hawa!. Kama brother Ditto (rip) aliyafanya aliyoyafanya na akapewa dhamana, wako mamia kwa maelfu wanaoozea jela kwa kukosa huduma hizi. Ukiimagine haka kabinti kalivyo na akili za ki 'wema sepetu", halafu ukawafikiria wana jela wetu!, kanahitaji serious rescue efforts soonest!.

kweli mkuu baada ya tukio hili utaweza tu

ila mpaka sasa kuna wengi sana wameishajitokeza kumsaidia huyu ,mtoto kuna laywer yuko south afrikca jana kasema wazi humu...atajitolea bure!!! pasi na shaka wengi wameishajitokeza atapata kazi sasa ya kuchagua!!!

Pasco rudi kwenye aadili kwanza utaona makosa lukuki ya Lulu..Lulu jina tu..she is just a little b.i.t.c.h

umesema una mtoto wa miaka 18 sidhani kama anafanya kama ya Lulu...huwezi ukamruhusu hivyo

ushauri wangu ni acha kakulie jela..
 
sio yeye tu..natamani kama ningekuwa lawyer nijitolee kukatetea ,baada ya kushinda kesi singekuwa na haja ya mahari...ningekachukua na KUKAFARIJI kwa sababu automatically kameishakuwa excommunicated na society -OUTCAST

Hii tunaita ni opportunity

mwisho wa siku paka uzuri wake unaweza ku-influence mahakimu...wakaamua isivyo..sijui sheria inasemaje...

aisee Pasco wangu!
Wabe, huna haja ya kutamani kuwa lawyer ukisaidie, kwa wenzetu ma best lawyers ni wale waliosoma something else halafu ndio wakasomea sheria, mfano wewe na Eng. yako halafu ukapiga law, jaji angepindisha haki kama ile kesi ya Lema, ungejikuta unatumia Engeneering kumnyoosha. Wanasheria waliosoma science ndio no-nonsense lawyers!. Hivi unajua kila deal ya Epa ili ipite lazima iende na deed iliyopitia kwa lawyers, sasa zile deed za good lawyers, zote zime go through, hizo kesi mnazoziona ni wale wabahili waliiona 5% legal fees ni too much!.

Pia nimekosoma hukahurumii haka kabinti!, asiyekuwepo machoni na moyoni hayupo, utaingia huruma only if ukikaona kako katika hali gani, na kalivyoumizwa!.
 
NazDaz, kinachofuata ni mimi kufanya petition niwe registered nitoe msaada wa kisheria nisaidie watu kama hawa!. Kama brother Ditto (rip) aliyafanya aliyoyafanya na akapewa dhamana, wako mamia kwa maelfu wanaoozea jela kwa kukosa huduma hizi. Ukiimagine haka kabinti kalivyo na akili za ki 'wema sepetu", halafu ukawafikiria wana jela wetu!, kanahitaji serious rescue efforts soonest!.

Hapo kwenye red, inauma sana!!!
....Sipati picha watakavyokuwa wanakadanganya kwamba watamsaidia
....sipati picha watakavyomrubuni kwa kumpa no torturing life hapo mahabusu/gerezani
....sipati picha watakavyomdanganya kwamba wanavutiwa na uigizaji wake
....sipati picha watakavyojifanya wapo so concerned na tatizo lake
Kumbe yote hayo yatakuwa ni unafiki wa kiume wenye kulenga kumvua nguo ya ndani!!
 
Mimi sio mshabiki wa Kanumba na wala sio mshabiki wa bongo movies na maigizo ya bongo
Mkuu umekurupuka, kwa kuwa walikuwa wawili chumbani you have nothing to comment labda uwe umeona picha za security camera kama ilikuwepo chumbani. Yaliyotokea chumbani hata mdogo mtu hajui tofauti na kusikia sauti za kujibizana hivyo hata kama Lulu ndio alimsukuma mahakama inaweza kuprove otherwise,
La msingi ni kushirki msiba na sio kusema ni uzembe ulitokea, UZEMBE!!!!!! upi???? utaje? wewe unaamini hearsay kuwa dokta aliiitwa? kinakchokufanya uamini kuwa dokta aliitwa tofauti na kusikia maneno ya watu ni nini?
Umesema mdogo mtu alisema mlango umefungwa! hivyo hakuwa kwenye scene of crime utajuaje kama maneno yake ni mawazo tu kwani huyo aliyefariki ni ndugu yake? wewe ingekuwa ni ndugu yako amefariki kwa mazingira hayo ungetetea upande upi? si ungekuwa upande wa ndugu yako.
Mtu kuwa na daktari wake sio lazima awe na matatizo fulani, Kanumba ni msanii hivyo ana marafiki na among those friends inawezekana mmoja wapo akawa daktari na akawa ndio anawasiliana nae wakati anaona ana ugonjwa, hii ni kawaida sana, kwa wabongo tunasema ni daktari wangu kumbe ni rafiki tu.
Wewe umekuja na mawazo yako kama ingekuwa wewe ungefanyaje. Kumbuka mawazo yako sio ya mwenzio, hivyo yaliyotokea sio uzembe ni mipango ya mwenyezi Mungu, na sioni uzembe uliofanyika labda kama wewe ulikuwepo eneo la tukio toka mwanzo na kushuhudia kila kilichotokea ndio useme kuna uzembe uliotokea.
Haya ni mawazo yangu.
 
Naimani kuwa tuliowengi tunasahau kuwa "Kila nafsi itaonja mauti" kifo cha ndugu yetu bwana Steven Kanumba kimetuhuzunisha sana lakini haiyumkini Mungu ndo mpangaji wa yote,nimeona post za wengi waliochangia katika uzi huu wameegemea kwenye uzembe wa kutokumpatia Kanumba huduma ya kwanza,hapa ndo tunasahau uweza wa Mungu! Niwakumbushe jambo matukio mawili makubwa, baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alipokwenda St Thomas Hospital baada ya kuzidiwa sana aliwekwa kwenye Life Support Machine lakini uweza wa Mungu ulizidi akafariki pia Kiongozi wa Wapalestina Yasser Arafat nae aliwekwa kwenye machine kama hiyo kwa muda mrefu na alifariki. My Take:Kifo chochote kinapotokea cha mtu ambae ni maarufu na pia ni kipenzi cha watu kila jambo tutalisikia oohoo mara huyu mzembe hakutoa huduma ya kwanza mara huyu kwa nini hakumuita Dakitari tunasahau kuwa Mungu ndiye anaetupa uhai na ni yeye mwenye uwezo wa kusitisha uhai wetu!
 
Uzembe unaanzia kwa Steven na Lulu. Aidha baada ya Steven kuzidiwa ilimpasa lulu aseme huyu kiongozi nimemtwanga/ kajitwanga na a b c... au kanywa sumu kwa hiyo shemeji tufanye a b c d's... tuokoe maisha yake. Kalijua nini kimefanyika then kakatimka. Upuuzi huu. R.I.P SK.
 
umesema una mtoto wa miaka 18 sidhani kama anafanya kama ya Lulu...huwezi ukamruhusu hivyo

ushauri wangu ni acha kakulie jela..
Wabe, hawa watoto wetu wa .com kuna vitu huwezi amini. Mimi nimeanza kunywa pombe five years baada ya kuanza kazi na mpake leo sivuti hata sigara japo nilishajaribu kuvuta kila kitu.

I'm now a father of 6, 4 teens na two minors. Hawa teens wakubwa akiwemo huyo binti wa 18, wameshafanya almost everything!. With such a team. you have to be friends na watoto wako, nani miongoni mwao watakuambia mwenzao amewahi kufanya nini!. Nimeshaitwa kwenye kesi kibao za shule mpaka sasa niko kwenye kamati mbili za shule tofauti!.

Nakubali mwana umleavyo ndivyo akuavyo, ila amini usiamini, unajitahidi to give the best to your kids, halafu mtoto anakuja kuwa na tabia za ajabu kwa kufanya mambo ya ajabu na kushangaza mpaka kushindwa kuamini!.

Ziko baathi ya tabia za ajabu za watoto wetu mpaka zinatishia kuhatarisha ndoa zetu, kwa kuhisi au "umesingiziwa nini?"!

Unaweza kukuta kwenye hiki kisa cha Lulu, kiLulu chenyewe wala hakijali kihivyo wala hakijui kimefanya nini wala consequenses ni nini, utakuta anaetesema na kulia zaidi ni mama yake!
 
Pasco, umegusia jambo la muhimu saana uliposema unataka kusaidia wengine wajue haki zao...

Kwa kweli hili ni tatizo hasa pengine zaidi ya wengi wanavyodhani...(kuna mahala mtu anasema utaratibu wa PF3 uko wazi na unafahamika...nimesikitika sana)

eneo hili la huduma linahitaji saaana msaada wa wataalam husika. Umechagua njia iliyo njema kwa kweli kama uyasemayo utayaweka kwenye matendo.
 
Mkuu Pasco,
Katika hili mie sina haja ya kutafuna maneno!! Hata kama nimehuzunishwa na kifo, bado napinga kwa nguvu zote huyu binti kuhusishwa na hiki kifo! Ikumbukwe kwamba, Kanumba kwa Lulu ni Kama Daud kwa Golliath…..!! Sina shaka yoyote kwamba, kutokana na wivu wa kimapenzi, Marehemu alianza kumshushia kisago Lulu! Bila shaka, kwa jinsi wanaume tulivyo, asilimia kubwa ya wengi wetu tungechukua uamuzi wa marehemu wa kuanza kumshushia binti kipigo!
Kwa upande mwingine, Lulu alikuwa na haki ya kujitetea! Kama nilivyosema hapo awali, Lulu kwa Kanumba ni sawa na Daud kwa Golliath! Ninachomaanisha, asingeweza kuchapana nae hivyo suluhisho pekee kwake ilikuwa ni kujinasua toka mikononi mwa marehemu! Kama chumba kisingekuwa kimefungwa (may be kilifungwa ili kichapo kitolewe sawasawa na asiwepo wa kukimbia) basi suluhisho la Lulu lingekuwa kutimua mbio! Lakini kwavile mlango ulikuwa umefungwa, Lulu alilazimika kwanza ,kumsukuma marehemu ili apate nafasi ya kutimua mbio na kufungua mlango! Jambo hili, lingefanywa na yeyote yule with exception of very few! Hata ningekuwa mimi, nisingekuwa na njia mbadala zaidi ya hiyo ya kumsukuma Kanumbe ili nipate uchochoro wa kutimua mbio! Hivyo, vyovyote iwavyo, Lulu hakuwa na namna zaidi ya hiyo ingawaje ni bahati mbaya hatua yake ya kujiokoa imezaa mauti kwa mwenzake!

Tukija kwa mdogo wake Kanumba, huyo ndie mpuuzi kuliko wote….!!! Nazani ujinga kama sio upumbavu aliofanya ni kutaka kujaribu kuifunika hii issue kwavile aliona ingekuwa skendo kwa kaka yake!! Bila shaka, wakati akichelea kuchukua hatua ya kumpeleka hospitali au kuita majirani (ili kuficha skendo) kumbe ndo alikuwa anakaribisha kifo kwa kaka yake! Na hata hiyo hatua yake ya kuanza kwanza kumuita “daktari” wa Kanumba ilikuwa na lengo lile lile la kuficha skendo!
WASWAHILI WANASEMA, MFICHA MARADHI KIFO UMUUMBUA……hiki ndicho kilichotokea kwa Mpendwa wetu Kanumba!!


so far, this is best analysis for me.
 
pasco,you are not into their shoes ndio maana unasema hivyo.yakikukuta hata kama unajua mengi,ila unajikuta una panic,kwani ni jambo ambalo hukulitarajia.na kama uzembe,tanzania mambo mengi hufanywa ki enyeji enyeji tu.
 
Pasco sehemu zote nimeona umemtetea sana Lulu (polisi kwa sasa wanamuita muuaji) Tueleze uhusiano wako nae hapa jukwaani maana aisifiaye mvua.....
Nina shaka na wewe tena sana au mambo flani tayari mkuuu......huyo mtoto anavutia eti!!!
 
Wanabodi,

Kwanza tuendelee kupeana pole kwa msiba wa mpendwa wetu Stephen Kanumba.

Leo nimeisikia taarifa ya awali ya polisi ikielezea mwili wa marehemu umekutwa na jeraha kichwani na kushikiliwa kwa binti Lulu mwenye umri wa miaka 18 kuisaidia polisi katika uchunguzi huo!. Taarifa ya daktari kuhusu kilichosababisha kifo bado haijatolewa!.

Hili ni jukwaa la jamii inteligence likijikita zaidi kwenye facts na sio hisia na hoja hapa sio kupeana pole za msiba wala kumtetea huyu binti Lulu ambaye anataka kibebeshwa msalaba wa kifo cha Kanumba kama mhusika mkuu wakati ukweli halisi kuna kila dalili zinazoonyesha Kifo cha Kanumba japo kimesababishwa na ajali ya kuanguka na kujigonga, kinaweza kuwa kimesababishwa na uzembe wa watu fulani na sio huyu binti Lulu!.(kwanza nilipost kule jamii inteligence ikagoma)

Hoja hii inafuatia maswali mengi bila majibu ya ni nini haswa kilichotokea hiyo jana!.

Wewe kama uu mmoja wa mashabiki wa Kanumba na mpaka sasa una uchungu mkubwa na kifo hiki, nakishauri usichangie uzi huu maana utakosa objectivity na impartiatility kutokana na huzuni.

Hoja za msingi ni hizi.
1. Ugomvi ulitokea saa 6 usiku na mpaka majirani walisikia kelele. Mwili umefikishwa hospitali ya Muhimbili saa 11 Alfajiri, nini kilitokea hapo kati?.

2. Mdogo wa marehemu aliyekuwa nyumbani wakati huo ameongea kwenye TV kuwa aliposikia ugomvi akaenda kutoka kuingilia mlango ukafungwa kwa ndani, akaendelea kusikia vishindo ambavyo na majirani walivisikia, what did he do?, au mlango ukishafungwa basi ni kujiachia tuu liwalo na liwe, hapa sio kuna uzembe fulani?!.

3. Baadae Lulu akaufungua mlango na kutoka kama alivyozaliwa na kumweleza huyo kijana Kanumba ameanguka hiyo ilikuwa ni around saa 6 usiku, huyo kijana ulikwenda chumbani na kumkuta Kanumba kama alivyozaliwa anagalagala chini huku povu likimtoka mdomoni, what did he do first?.

4. Anasema alimpigia simu daktari wake!. Hivi kweli unaitwa chumbani na kumuona mtu ameanguka anavuja damu anatapatapa, wewe utamtafuta kwanza daktari wake au kazi ya kwanza ni kumkimbiza mgonjwa hospitali ya karibu?. Pale kwa Kanumba mpaka hospitali ya Sinza Palestina ambayo ni 24/7 ni only 5 minites away!. Tukio limetokea saa 6 usiku mwili wapelekwa Muhimbili 11 alfajiri!. Kulitokea nini hapo?!. Hapo sio uzembe fulani huu?!.

5. Hivi ni kweli Kanumba alikuwa na daktari wake?. Jee alikuwa ana suffering something kiasi kwamba kuna daktari maalum ndio huwa anamhudumia hali iliyolazimisha lazima atafutwe huko aliko ndipo Kanumba apate huduma ya kwanza!. Kama tukio ni saa 6, daktari alipigiwa simu saa ngapi?, na alifika saa ngapi?, kumbukeni muda wote huo Kanumba anagalagala na kuvuja damu nyingi kumsubiria daktari wake afike?!. Huu sio uzembe fulani?.

6. Tunaelezwa daktari alipofika ndipo juhudi za kumkimbiza Muhimbili zikafuatia, huku kukipatikana tarifa za baadhi ya wasanii kufika hapo kwa Kanumba within minutes na wengine kukiri walimkuta mwili umeshaanza kuwa baridi, muda gani ulishapita toka tukio mpaka hao wasanii/majirani waliofika mwanzo and what did they do?!. Hapa kweli hakuna uzembe fulani?.

7. Tumeonyeshwa picha na TBC zikionyesha umati mkubwa wa wasanii ukiandamana kuupeleka mwili Muhimbili, ikumbukwe wakati tukio alikuwa kama alivyozaliwa ila mwili ulionekana umevishwa, hivyo emergence ya aina ile mgonjwa huwa anafunikwa tuu shuka na kuwahishwa hospitali, kupatikana muda mpaka kumvisha huu sio uzembe fulani?!.

8. Kama tukio ni la dharura tulitegemea watu wa kwanza ni majirani iweje wasanii wajazane kivile usiku huo mpaka na waandishi wa TBC?. Haiwezekani baada ya kutokea ajali hiyo ya kuanguka, badala ya kumpatia mgonjwa huduma ya kwanza ya kujaribu kuokoa maisha ya Kanumba, watu walikuwa bize kuwatafuta masuper star na waandishi wawahi tukio lile huku wengine wakiendelea kuhangaikia kuupiga picha mwili wa Kanumba licha ya kujua tayari ni dead body?!.

9. Kama hao waliofika wakanshika na kuona mwili umeanza baridi, ni muda gani daktari alifika?. Ni muda gani walijua Kanumba ameshafariki?, kama alifia nyumbani hawakujua hiyo sasa at that poit ni police case badala ya kuitana makundi ya wasanii na kuidramatise scene ya kifo cha Kanumba?!.

10. Mwisho kwa sababu ripoti ya daktari kutaja chanzo cha kifo haijatoka, naombeni tusimbebeshe mtoto Lulu msalaba wa kifo cha Kanumba!. Inawezekana ni Kanumba mwenyewe aliteleza, na hata kama ni kweli alimsukuma, kama alimsukuma in self defence, Lulu hana hatia yoyote kwa sababu kifo kitakuwa kimetokea kwa bahati mbaya bila kusudio la kutenda jinai ya mauaji!.

RIP SK The Great

Pasco.

Mambo Lulu.Pole kwa matatizo ila usiwe na shaka wala usipate shida.ni mipango ya Mungu na ninakuombea sana kikombe hicho kikuepuke kwa mapenz ya Mungu.najua halikua kusudi lako ila limetokea.Mungu na akutangulie na akutie Nguzu kwa kipindi chote hiki kigumu.tupo Pamoja kiushauri jamani huyu mtoto tumuacheni kwanza.
 
Mimi sio mshabiki wa Kanumba na wala sio mshabiki wa bongo movies na maigizo ya bongo
Mkuu umekurupuka, kwa kuwa walikuwa wawili chumbani you have nothing to comment labda uwe umeona picha za security camera kama ilikuwepo chumbani. Yaliyotokea chumbani hata mdogo mtu hajui tofauti na kusikia sauti za kujibizana hivyo hata kama Lulu ndio alimsukuma mahakama inaweza kuprove otherwise,
La msingi ni kushirki msiba na sio kusema ni uzembe ulitokea, UZEMBE!!!!!! upi???? utaje? wewe unaamini hearsay kuwa dokta aliiitwa? kinakchokufanya uamini kuwa dokta aliitwa tofauti na kusikia maneno ya watu ni nini?
Umesema mdogo mtu alisema mlango umefungwa! hivyo hakuwa kwenye scene of crime utajuaje kama maneno yake ni mawazo tu kwani huyo aliyefariki ni ndugu yake? wewe ingekuwa ni ndugu yako amefariki kwa mazingira hayo ungetetea upande upi? si ungekuwa upande wa ndugu yako.
Mtu kuwa na daktari wake sio lazima awe na matatizo fulani, Kanumba ni msanii hivyo ana marafiki na among those friends inawezekana mmoja wapo akawa daktari na akawa ndio anawasiliana nae wakati anaona ana ugonjwa, hii ni kawaida sana, kwa wabongo tunasema ni daktari wangu kumbe ni rafiki tu.
Wewe umekuja na mawazo yako kama ingekuwa wewe ungefanyaje. Kumbuka mawazo yako sio ya mwenzio, hivyo yaliyotokea sio uzembe ni mipango ya mwenyezi Mungu, na sioni uzembe uliofanyika labda kama wewe ulikuwepo eneo la tukio toka mwanzo na kushuhudia kila kilichotokea ndio useme kuna uzembe uliotokea.
Haya ni mawazo yangu.
Mkuu Mwandiga, kwanza nashukuru kwa mchango wako very objective. Mimi sijasema ni uzembe, bali nimeuliza sii uzembe?, na kuna alama ya kuuliza pale!, kilichofuata ni kuainisha mazingira ya uzembe!.
 
kweli mkuu baada ya tukio hili utaweza tu

ila mpaka sasa kuna wengi sana wameishajitokeza kumsaidia huyu ,mtoto kuna laywer yuko south afrikca jana kasema wazi humu...atajitolea bure!!! pasi na shaka wengi wameishajitokeza atapata kazi sasa ya kuchagua!!!

Pasco rudi kwenye aadili kwanza utaona makosa lukuki ya Lulu..Lulu jina tu..she is just a little b.i.t.c.h

umesema una mtoto wa miaka 18 sidhani kama anafanya kama ya Lulu...huwezi ukamruhusu hivyo

ushauri wangu ni acha kakulie jela..

Waberoya,
Upo sahihi kabisa kuhusu tabia chafu za Lulu! Udhaifu huo, at least kwa kupitia magazeti ya udaku kila mmoja anaufahamu!! Nasisitiza, wengi wetu tuna-rely kupitia magazeti ya Udaku!!! Tukichukua watu 100 wanaoamini kwamba binti ni full mapepe halafu ukawaomba ushahidi, hawatafika 10 watakaokupatia ushahidi huo…..!!

Kimsingi, hata kama siyatetei maovu ya Lulu lakini endapo patatokea wa kuniuliza ni nani hasa anayepaswa kulaumiwa kuhusiana tabia za Lulu, basi Lulu mwenyewe ningempa nafasi ya tatu kwa Lawama!
Kwa anayefuatilia burudani ya maigizo hapa TZ, anafahamu kwamba Lulu ameanza kuigiza akiwa mdogo sana, I think akiwa chini ya miaka 10!! Unakuta jitu zima lenye akili zake anapoanza kuwa maarufu anakuwa mshenzi, what du expect kwa mtoto ambae amekua akishuhudia ushenzi huo?!

Tofauti na watoto wengine ambao walianza sanaa wakiwa wadogo na baadae kupotea; Lulu aliendelea kuwa nyota kwa kipindi chote hicho, tangu akiwa kinda hadi anabalehe! Hivyo basi, kama kuna mtu wa kwanza ambae anastahili lawama kuhusu tabia za Lulu basi si Lulu mwenyewe, bali wasanii wenzake ambao walikuwa watu wazima wenye kujua baya na zuri!! Wala sitashangaa nikisikia kwamba mwanaume wake wa kwanza tangu aanze kujitambua ni msanii mwenzake tena ambae bila shaka ni mtu mzima mwenye kujua baya na zuri!!

Ni bahati mbaya sana wazazi wake inaelekea hawakufahamu ubazazi uliomo kwenye tasnia ya burudani; si hapa nchini tu bali duniani kwa ujumla! Na kama walifahamu, inaelekea walihadahika na umaarufu aliokuwa anaupata binti yao bila kujua kwamba ni umaarufu uliokuwa unapelekea kaburi lake!

All in all, endapo patatokea wa kuniuliza endapo Lulu ni kicheche au sio kicheche; jibu langu ni kwamba sio kicheche kwa sababu mie sijawahi gonga yule mtoto!!! Siku nikija piga, nita-conclude kwamba, SURE….mtoto hajatatulia!!!
 
Wabe, hawa watoto wetu wa .com kuna vitu huwezi amini. Mimi nimeanza kunywa pombe five years baada ya kuanza kazi na mpake leo sivuti hata sigara japo nilishajaribu kuvuta kila kitu.

I'm now a father of 6, 4 teens na two minors. Hawa teens wakubwa akiwemo huyo binti wa 18, wameshafanya almost everything!. With such a team. you have to be friends na watoto wako, nani miongoni mwao watakuambia mwenzao amewahi kufanya nini!. Nimeshaitwa kwenye kesi kibao za shule mpaka sasa niko kwenye kamati mbili za shule tofauti!.

Nakubali mwana umleavyo ndivyo akuavyo, ila amini usiamini, unajitahidi to give the best to your kids, halafu mtoto anakuja kuwa na tabia za ajabu kwa kufanya mambo ya ajabu na kushangaza mpaka kushindwa kuamini!.

Ziko baathi ya tabia za ajabu za watoto wetu mpaka zinatishia kuhatarisha ndoa zetu, kwa kuhisi au "umesingiziwa nini?"!

Unaweza kukuta kwenye hiki kisa cha Lulu, kiLulu chenyewe wala hakijali kihivyo wala hakijui kimefanya nini wala consequenses ni nini, utakuta anaetesema na kulia zaidi ni mama yake!

Hapo kwenye red hapo mkuu,

1.Sigara a.k.a sigareti
2.......?
3.......?
4.......?
5.......?

Ni kujuzana tu mkuu....sina lingine!!!!
 
msimlaumu mama yake lulu,huyo mama ameshamuonya sana mtoto wake,ila mtoto hasikii.sifikirii kama mzazi unapenda mtoto wako aharibikiwe.sometimes unajitahidi vya kujitahidi.lakini mtoto anakuwa hasikii,matokeo yake,mama anaonekana mkosaji.halaumiwi baba,atalaumiwa mama.
 
Several Search engines fail to convince me that MTU ANATOA POVU AKIGONGWA KICHWANI SHINGONI AU HATA MGONGONI! KAMA KUNA DOKTA ANAFAHAMU HII KITU ANISAIDIE JAMANI
 
Back
Top Bottom