Kifo cha Mwalimu Nyerere 14/10/1999, ulikuwa wapi?

Kumbe huku % kubwa ni watoto ?,ushauri wangu ni huu,suala la umri lizingatiwe ili uweze kuwa member wa jf,pls wahusika walifanyie Kali
 
Nilikuwa darasa la 2 shule ya msingi chemchem, Iringa mjini. Nilimuuliza mama yangu huyo Nyerere atapokelewa wapi, akanambia kaenda moja kwa moja kwa Mungu maana hana dhambi, kuskia hivyo nikafarijika. Hahahahaaa utoto raha sana haya kama wapo waliosoma chemchem enzi hizo hebu tuwasiliane.
 
Nilikua shuleni darasa la5, kengele ikapigwa ya dharura tukajulishwa msiba wa taifa tukarudishwa home

Njiani tunakutana na nyimbo za maombolezo basi tukaanza na sisi kulia hasa tulivosikia vita itakuja.,.
 
Nilikuwa Home sikwenda skonga (darasa kama sio iii basi iv) baada ya house girl wetu kuniambia nisiende ili anipe zawadi (ye mkubwa mi mdogo) nikawa nasikia vilio nje nikataka kutoka nijue kinachoendelea yule hg wetu akanivutia ndani huku ananiambia nyerere kafa na wewe hutoki humu,basi kilichoendelea wakubwa wote mnajua ni nini.
 
Kumbe watoto wadogo wengi humu la pili, la tatu???
Umeonaeee, sie wakati huyo jamaa anakufa tuwatu wazima kabisa na k tunakula. Nashangaa wengi wanasema lapili mara darasa la tatu, si bora hao walokuwa form 4. Ndo maana tunapojadili maswala ya msingi huku tunakuwa na shida sana kumbe watoto wamejaaa aghhhhhrrrri.

Natania tu bwana watotot msiogope, nyie ndo mnafanya JF isiwe boared, I like you kids.
 
Kumbe huku % kubwa ni watoto ?,ushauri wangu ni huu,suala la umri lizingatiwe ili uweze kuwa member wa jf,pls wahusika walifanyie Kali
Acha roho mbaya wewe tena si ajabu wenye umri mdogo wana hekima kuliko wenye umri mkubwa. Ukubwa wa mtu hatuangalii idadi ya miaka aliyonayo au wingi wa mvi zake bali tunaangalia busara na hekima zake katika mambo mbalimbali ya kiutendaji hata utatuzi wa shida katika jamii inayomzunguka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…