Wakuu salaam,
Nimeshindwa kutoa pole mapema kwa msiba wa Kanumba kwa sababu bado nilikuwa natafakari nini cha kusema. Kwa ukweli mimi ni mmojawapo wa wapenzi wa Kanumba katika filamu na kwa ukweli nilikuwa naangalia filamu zake na JB tu! wengine hawakuwahi kunishawishi labda pastor Muamba akikemea mapepo.
Kilichonisukuma kutoa pole leo ni tafakuri kwamba tutapoteza wasanii wangapi kwa uzembe?
Nilikuwa na classmate wangu NELLY. alianza mziki hip hop akaishia kufa kwa kuchomwa kisu. Leo nimempoteza Kanumba, Mr Nice kafulia hadi hatamaniki, Wema yeye ni vurugu usiku na mchana, Sinta alijiuza hadi akachokwa na sasa Lulu yuko lupango! Wasanii wetu wanaamini saa zingine kwenye umaarufu wa kuleteana mabifu! Nashindwa kuelewa kama bifu la Kanumba na Lulu lililopelekea msiba lilikuwa la kujenga umaarufu au ni lakweli!
Shida kubwa ni wasanii wetu kutokuandaliwa kuwa ma -SUPERSTARS. hatuwaandai kukabiliana na changamoto za jamii, hatuwaandai kwenye maisha bila kujulikana hadi kujulikana na wakati mwingine unakuwa maarufu sana lakini mfukoni huna kitu. Hatuwaandai kuwa mfano tunawaandaa kuwa kero. Leo Matunzo mabovu ya lulu yamemfikisha hapo alipo. Lakini kosa sio la lulu bali ni kosa la jamii! Lulu aanaamini kwamba kuwa mzuri ni kutembea uchi, Kanumba aliamini kuwa Star ni kutembea na wanawake wazuri wote! Jana WEMA leo Lulu kesho...?
Majanga kwa wasanii hayataisha tusipojipanga tutawapoteza wengi ama kwa kifo ama kwa magereza!
MYTAKE: Inatakiwa ijengwe shule (AMA BAGAMOYO INGEWEZA KUWA MAHALI SAHIHI) KWA AJILI YA WASANII WETU KUANDALIWA. HUKO WANGEJENGWA KISAIKOLOJIA NA PENGINE FAMILIA MASKINI WALIZOTOKA ZINGEWEZA KUFAIDI MATUNDA YA WATOTO WAO.
POLENI SANA KWA MSIBA WATANZANIA WOTE.