Fabian the Jr
JF-Expert Member
- Aug 4, 2012
- 756
- 751
Naona hili neno limekuwa likitumika sana katika kutoa faraja kwa watu, utasikia mtu anamwambia mwenzake, "Pole sanaa ni mipango ya Mungu" ikiwa ni njia ya kumfanya mtu aone hilo jambo ni la kawaida na ni mipango ya Mungu mtu huyo kufa.
Siamini kwamba kila kifo ni mpango wa Mungu.
Imani yangu ni kwamba Mungu katuumba tuishi na tuzeeke tufe.
Mifano ya watu wote walioishi katika njia za Mwenyezi mungu kwenye vitabu vitakatifu inaniambia walizaliwa wakaishi wakazeeka wakafariki wakiwa wenye umri wa kutoendelea kuishi tena. Vifo vya namna hiyo hata mimi naamini ndio mpango wa Mungu.
Mtoto wa miaka minne, ameugua maralia, wazazi wamechelewa kumpeleka hospital au amepelekwa madakatar wakakosea katika vipimo akafa, watu wanasema ni mpango wa Mungu.
Juzi ajali ile ya mabasi ya city boys, dereva badala ya kuendesha kwenye njia yake, kapita njia ya mwenzake watu 42 wakafa tunasema ni mpango wa Mungu kwamba alipanga watu wale 42 wafe siku hiyo.
Unajenga nyumba kizembe zembe mtu anakaa anaangukiwa na ule ukuta unasema ni Mpango wa Mungu.
Nilikuwa naangalia records za vifo vya watoto chini ya miaka 5 kwa upande wa marekani na Tanzania, nikazifanyia comparison, Marekani wana idadi ndogo sanaaaa ya watoto wanaokufa chini ya miaka 5 wakati Tanzania idadi hiyo ni kubwa sana, kwanini? Marekani uangalizi wa watoto wadogo ni mkubwa sana na hata matibabu yake ni ya uhakika wakati Tanzania uangalizi kwa watoto wadogo na matibabu yake ni ya kubahatisha. Je vifo vya hawa watoto ni mpango wa Mungu?
Hivyo hivyo ukiangalia hata hapa kwetu, vifo vya watoto wadogo Masaki na vifo vya watoto wadogo Mbagala utaona kuna ratio ya 1:10 au zaidi ya hapo, Je ni mpango wa Mungu kwamba watoto wengi wafe Mbagala na sio Masaki?
Unaendesha bodaboda kwa speed unaanguka unakufa unasema ni mpango wa Mungu, Mtu katoka huko anaendesha gari lake bila kuwa makini anamgonga raia mwema aliyesimama pembezoni mwa barabara tunasema ni mpango wa Mungu,
Hapana, huo sio mpango wa Mungu, Ni mpango wa binadamu.
Hata katika biblia na Qur'aan ukisoma kama kuna kifo ambacho kilitokea kabla mtu hajazeeka basi fuatilia kuna UZEMBE aliufanya mahali fulani au yeye au wazazi wake wakapelekea akafa.
Kwa kusema hayo, ni imani yangu na ninaomba niwashawishi kwambaa, vifo kabla ya uzee vinaepukika, kutokana na mazingira, kulinda afya yako, namna unavyoishi na watu unaweza kuepuka vifo ambavyo sio mpango wa Mungu.
Siamini kwamba kila kifo ni mpango wa Mungu.
Imani yangu ni kwamba Mungu katuumba tuishi na tuzeeke tufe.
Mifano ya watu wote walioishi katika njia za Mwenyezi mungu kwenye vitabu vitakatifu inaniambia walizaliwa wakaishi wakazeeka wakafariki wakiwa wenye umri wa kutoendelea kuishi tena. Vifo vya namna hiyo hata mimi naamini ndio mpango wa Mungu.
Mtoto wa miaka minne, ameugua maralia, wazazi wamechelewa kumpeleka hospital au amepelekwa madakatar wakakosea katika vipimo akafa, watu wanasema ni mpango wa Mungu.
Juzi ajali ile ya mabasi ya city boys, dereva badala ya kuendesha kwenye njia yake, kapita njia ya mwenzake watu 42 wakafa tunasema ni mpango wa Mungu kwamba alipanga watu wale 42 wafe siku hiyo.
Unajenga nyumba kizembe zembe mtu anakaa anaangukiwa na ule ukuta unasema ni Mpango wa Mungu.
Nilikuwa naangalia records za vifo vya watoto chini ya miaka 5 kwa upande wa marekani na Tanzania, nikazifanyia comparison, Marekani wana idadi ndogo sanaaaa ya watoto wanaokufa chini ya miaka 5 wakati Tanzania idadi hiyo ni kubwa sana, kwanini? Marekani uangalizi wa watoto wadogo ni mkubwa sana na hata matibabu yake ni ya uhakika wakati Tanzania uangalizi kwa watoto wadogo na matibabu yake ni ya kubahatisha. Je vifo vya hawa watoto ni mpango wa Mungu?
Hivyo hivyo ukiangalia hata hapa kwetu, vifo vya watoto wadogo Masaki na vifo vya watoto wadogo Mbagala utaona kuna ratio ya 1:10 au zaidi ya hapo, Je ni mpango wa Mungu kwamba watoto wengi wafe Mbagala na sio Masaki?
Unaendesha bodaboda kwa speed unaanguka unakufa unasema ni mpango wa Mungu, Mtu katoka huko anaendesha gari lake bila kuwa makini anamgonga raia mwema aliyesimama pembezoni mwa barabara tunasema ni mpango wa Mungu,
Hapana, huo sio mpango wa Mungu, Ni mpango wa binadamu.
Hata katika biblia na Qur'aan ukisoma kama kuna kifo ambacho kilitokea kabla mtu hajazeeka basi fuatilia kuna UZEMBE aliufanya mahali fulani au yeye au wazazi wake wakapelekea akafa.
Kwa kusema hayo, ni imani yangu na ninaomba niwashawishi kwambaa, vifo kabla ya uzee vinaepukika, kutokana na mazingira, kulinda afya yako, namna unavyoishi na watu unaweza kuepuka vifo ambavyo sio mpango wa Mungu.